Posts

Showing posts from September 1, 2016

Mwanzilishi wa Facebook Alivyokutana na Akina Yemi Alade Nigeria

Image
Lagos, Nigeria MWANZILISHI na mmiliki wa mtandao maarufu duniani wa Facebook, Mark Zuckerberg juzi Jumanne alianza ziara yake ya siku mbili nchini Nigeria, ikiwa ni ziara yake ya kwanza kwa nchi za Afrika, na kukutana watu mbalimbali wakiwemo wasanii maarufu wa uigizaji filamu na muziki nchini humo. Katika ziara hiyo, Zuckerberg aliwasili Lagos Jumanne na kufika kwenye kituo maarufu cha ubunifu wa masuala ya mitandao ya kijamii cha Yaba, kilichopo eneo lijulikanalo kam Silicon Valley. Zuckerberg alifanikiwa kutoa elimu ya biashara na masoko kwa watu waliohudhuria kwenye mkutano wake huku akitanua wigo wa watumiaji wa mitandao anayoimiliki ikiwemo Facebook, Instagram na WhatsApp. Baada ya somo hilo la juzi Jumanne, Zuckerberg jana aliamkia mitaani asubuhi akitembelea vijana kwenye Jiji la Lagos bila ulinzi. Alionekana akikifanya jogging kwenye daraja la Lekki Bridge na vijana. Baadhi ya wasanii wa filoamu na muziki nchini Nigeria jana ni pamoja na Richard M

Acer Yazindua Laptop Yenye Kikoo Kilichopinda

Image
Kampuni ya Vifaa vya kielektroniki ya Acer imezindua laptop ya kwanza yenye kioo kilichojipinda. Acer inasema kuwa uvumbuzi huo utaiwezesha kucheza michezo ya video. Televisheni kadhaa pia zimetumia uvumbuzi huo,lakini umezua mgawanyiko kwa kuwa una umuhimu na ubaya wake. Kampuni hiyo ya Taiwan pia ilitangaza kwamba imefanikiwa kupata teknolojia ya pet katika mkutano na wanahabari mjini Berlin. Kampuni kadhaa za kielektroniki ikiwemo Samsung, Lenovo, DJI, Sony na Huawei zinatarajiwa kuzindua sura mpya ya laptop zake katika maonyesho ya kiteknolojia ya Ifa katika Mji Mkuu wa Ujerumani wiki hii. Laptop hiyo ina kioo kikubwa ikilinganishwa na laptop ya kawaida ya Acer,lakini ni umbo lake ambalo liliifanya kampuni hiyo kudai kuwa ya kwanza kuzinduliwa duniani.

RAIS DKT MAGUFULI AFUNGUA MKUTANO MKUU WA WAHANDISI, ATEMBELEA KIKOSI CHA ANGA MAJUMBA SITA UKONGA

Image
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akifungua Mkutano Mkuu wa 14 wa Wahandisi katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es salaam leo Septemba 1, 2016  Amiri Jeshi Mkuu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akipata picha ya  pamoja na Wanajeshi wa JWTZ Kikosi cha Anga 603 KJ Majumba Sita Ukonga jijini Dar es salaam  alikotembelea kuwapongeza kwa kusherehekea miaka 52 ya Jeshi la Wananchi leo Septemba 1, 2016 Rais Magufuli awataka wahandisi nchini kufanya kazi kwa weledi na uadilifu Na Sheila Simba-MAELEZO  Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Magufuli amewataka  wahandisi nchini kufanya kazi kwa weledi na uadilifu ili kuiwezesha nchi kufikia uchumi wa kati kupitia ujezi na uendelezaji viwanda. Amesema hayo leo jijini Dar es salaam katika mkutano wa 14 wa Bodi ya Wahandisi Nchini,na kuwaasa kutumia taaluma yao kusaidia nchi kufikia uchumi wa kati ili kuleta maendeleo kwa haraka kw

MKUTANO WA 36 WA SADC UMEMALIZIKA NA TANZANIA YATEULIWA KUWA MWENYEKITI WA TROIKA

Image
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiweka saini katika moja ya makubaliano yaliofanywa na nchi za SADC kwenye mkutano wa 36 wa Wakuu wa Nchi na Serikali uliofanyika Lozitha, Mbabane nchini Swaziland.  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan (kushoto)akizungumza na Makamu wa Rais wa Angola Mhe. Manuel Domingos Vicente wakati wa kuhitimisha mkutano wa 36 wa nchi za SADC mjini Mbabane Swaziland. Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan (katikati) akiwa kwenye mkutano wa 36 wa nchi 15 za SADC uliofanyika mjini Mbabane Swaziland, kulia ni Makamu wa Rais wa nchi ya Angola Mhe. Manuel Domingos Vicente na kushoto ni Waziri Mkuu wa Madagascar Mhe.Mahafaly Solonandrasana Olivier. Mwenyekiti wa SADC Mfalme Mswati wa III(kulia) akizungumza na Katibu Mkuu Mtendaji wa SADC Dr. Stergomena L. Tax wakati wa kuhitimisha mkutano wa 36 wa SADC mjini Mbabane,Swaziland. Mw