Posts

Showing posts from August 24, 2017

NDOA YA MISS TANZANIA, MTOTO WA MAKAMBA… USIPIME!

Image
Victoria Martin na Thuwein Makamba. DAR ES SALAAM: Ni historia! Harusi ya Mrembo aliyetinga Top Five ya Miss Tanzania 2007, Victoria Martin na mtoto wa aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Yusuf Makamba, Thuwein Makamba imeacha gumzo la aina yake kutokana wawili hao kuangusha sherehe baa’kubwa. NI TANGA Wawili hao walifanya tendo hilo jema kwa Mwenyezi Mungu, Ijumaa iliyopita mkoani Tanga ambapo waalikwa waliizungumzia kama ni ndoa ya kihistoria kwani kwa kipindi hiki, haijawahi kufungwa ndoa na watu kunywa, kula hadi kusaza kwa kiasi hicho. CHANZO KINAIFUNGUKIA Chanzo makini ambacho kilianza kushuhudia sherehe za wawili hao kuanzia send off hadi harusi, kilisema matukio hayo yote yalipambwa na kufuru ya vinywaji na vyakula kiasi ambacho kila aliyeingia ukumbini alitoka akiwa nyang’anyang’a. “Yani kwa kipindi hiki cha Magu (Rais Dk John Pombe Magufuli) sherehe kubwa kuandaliwa kwa kiwango hiki ni tukio la aina yake maana watu kwa kweli hawa

MZEE MAJUTO: BADO NAUMWA JAMANI

Image
Mzee Majuto. Ikiwa ni siku chache tangu muigizaji mkongwe,  Amri Athman Amri ‘King Majuto’ kupata unafuu kufuatia upasuaji aliofanyiwa kutokana na tatizo la ugonjwa wa ngiri (hernia), hali yake bado haijatengemaa na anatumia muda mwingi kulala, Amani limezungumza naye kwa tabutabu. Jumatatu ya wiki hii, mwandishi wetu alimpigia simu mzee huyo kwa lengo la kumjulia hali na kufanya naye mazungumzo mengine, lakini King Majuto alisikika kwa shida na kudai amelala na anahitaji muda mwingi wa kupumzika na kwamba bado anaumwa na anasikia maumivu makali. Hata hivyo, mwandishi aliendelea kumdadisi kwa kina ili kujua ni nini hasa kinachoendelea kumsumbua kwani kama ni tatizo la awali alishafanyiwa upasuaji, ambapo aligoma kabisa kuendelea na mazungumzo na kugeuka ‘mbogo’ kwa muda kwa madai ya kutopenda mazungumzo na wanahabari. “Bado nimelala jamani na sijui unataka nini tena? Naumwa na ninasikia maumivu sana na sitaki kuzungumza zaidi maana nimechoka, elewa

TFF Yaomba Radhi kwa Makosa ya Uandishi Ngao ya Jamii

Image
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limeomba radhi wanafamilia wote wa mpira wa miguu nchini kutokana na makosa ya kiuandishi yaliyoonekana kwenye utambulisho wa Ngao ya Jamii iliyotolewa Jumatano Agosti 23, 2017 kwa klabu ya Simba. Ngao hiyo ilitolewa mara baada ya mchezo uliokutanisha timu za Simba SC na Yanga SC zote za Dar es Salaam kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Katika mchezo huo, Simba ilishinda kwa mikwaju ya penalti 5-4 dhidi ya Yanga na kutwaa ngao hiyo. Makosa yaliyoonekana katika ngao hiyo ya jamii ni kukosewa kuandikwa kwa neno “SHIELD” ambapo liliandikwa “SHEILD” na hivyo kupoteza maana yake ya msingi. Katika taarifa ya TFF iliyotolewa leo Agosti 24 wamesema kwamba “Watanzania hususani wanafamilia ya mpira wa miguu popote pale, TFF hatujapokea vizuri mwonekana wenye makosa kwenye Ngao hiyo ya Jamii kama ambavyo wadau hawajapokea vema suala hili.” Kuonyesha kukerwa na uzembe huo uliofanywa na baadhi ya viongozi wake, Kaimu K

MIMBA YA ‘MATAMBARA’ YAMUUMBUA HUSNA

Image
Husna Maulid. MIMBA ya Husna Maulid ilikuwa ya  kughushi.  Imemuumbua baada ya kugundulika kuwa hakuwa nayo, badala yake alikuwa akiweka matambara tumboni kuonesha ana mimba. Kwa  mujibu chanzo makini, Husna hakuwa na mimba, lakini alikuwa akiweka matambara hayo kwa ‘utashi’ wake ili aonekane tu ana ujauzito lakini hakuwahi kuwa nayo. “Nilikuwa  na MIMBA ya kughushi aliyokuwa akiiweka Video Queen wa Bongo, Husna Maulid imemuumbua baada ya kugundulika kuwa hakuwa nayo, badala yake alikuwa akiweka matambara tumboni kuonesha ana mimba. ninashangaa sana kwa nini Husna, alikuwa akiweka matambara ili aonekane ana mimba kitu ambacho wengi waliamini hivyo,” kilisema chanzo. Gazeti hili lilimtafuta Husna ili kuzungumzia ishu hiyo ambapo badala ya Husna kujibu hoja, aliangua kicheko na kusema yote ni ya walimwengu. “Daah sijui nizungumzeje hiyo ishu maana yote ni ya walimwengu bwana wee yaache si unajua tena mjini hapa,”  alisema Husna.