Posts

Showing posts from June 4, 2014

MILLEN HAPPINESS MAGESE: ASIMULIA AMBAVYO HAWEZI KUBEBA UJAUZITO, ASEMA YUPO TAYARI KUASILI

Image
Millen Happiness Magese. (ANAJIANDAA, anaonekana kuwa ni mtu mwenye hisia sana kabla ya kuanza kuzungumza, anamuuliza jambo Lucy Ngongoseke maarufu kwa jina la Lucy Kiwele ambaye anamwambia ajikaze azungumze, baada ya sekunde kadhaa anaanza kujielezea…) Naitwa Millen Happiness Magese ni mrembo wa Tanzania na Miss Tanzania wa mwaka 2001, kwa sasa nafanya kazi za mitindo nchini Marekani, kabla sijafika huko nilifanya kazi hiyo Afrika Kusini kwa miaka takribani nane. Nipo chini ya Kampuni ya Ford Models, nilisaini mkataba wa miaka minne na baada ya hapo nikasaini tena miaka miwili na ndiyo nilipo mpaka sasa. Miss Tanzania Mwaka 2001, Happiness Millen Magese akiwa ndani ya Global. Millen Magese Foundation Hii ni taasisi ambayo lengo kubwa ni kutoa msisitizo katika elimu. Suala hili linanihusu binafsi na ndiyo maana nalifanya kwa moyo, hapa Tanzania nimeanza na Mtwara baada ya hapo nitaendelea mikoa mingine. Hata nilipokuwa Miss Tanzania nililifanyia kazi suala

SAID MECKY SADICK AONGOZA MAMIA KUAGA MWILI WA TYSON

Image
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadick akiaga mwili wa marehemu George Otieno 'Tyson' katika Viwanja vya Leaders, Dar. Said Mecky Sadick wakati akielekea kuaga mwili wa Tyson. Mwili wa marehemu George ukiandaliwa kwa ajili ya kuagwa.   Mwili wa George Tyson ukiagwa.

MKUU WA MKOA ANAONGOZA WAOMBOLEZAJI KUUAGAMWILI WA MAREHEMU GEORGE TYSON

Image
Jeneza lenye mwili wa marehemu George Otieno 'Tyson' likiwa Viwanja vya Leaders tayari kwa shughuli za kuagwa. Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadick (katikati) akiwa na Rais wa TAFF, Simon Mwakifwamba (wa kwanza kushoto) na Mwenyekiti wa Bongo Muvi, Steve Nyerere (wa pili kulia) wakisubiri kuongoza shughuli za kuaga mwili wa Tyson. Aliyekuwa mke wa marehemu, Yvonne Cherry 'Monalisa' (kulia) akilia kwa simanzi pamoja na mwanae aliyezaa na marehemu Tyson, Sonia (katikati).PICHA NA HAMIDA HASSAN WA GPL

HIZI NI FAIDA 12 ZA MACHUNGWA

Image
Kumbuka kuwa hata chungwa moja tu ukila lina kidhi yale mahitaji muhimu ya mwili ya kila siku (daily requirement), iwe chungwa lenyewe au juisi yake halisi. 1. UKOSEFU WA CHOO Kutokana kuwa na kiwango kikubwa cha kirutubisho aina ya kambalishe (fibre), chungwa husaidia usagaji wa chakula tumbuni na hutoa ahueni kwa mtu mwenye matatizo ya ukosefu wa choo. Aidha, kambalishe huondoa kolestro na huimarisha kiwango cha sukari mwilini, hivyo chungwa ni zuri kwa wagonjwa wa kisukari. 2.UGONJWA WA MOYO Kiwango kikubwa cha Vitamin C na virutubisho vya ‘flavonoids’, ‘phytonutrients’ vilivyomo kwenye chungwa, huondoa kwa mlaji hatari ya kupatwa na magonjwa ya moyo (Cardiovascular disease)! 3. SHINIKIZO LA DAMU Virutubisho vya Magnesi (Magnesium) na ‘hesperidin’ vilivyomo kwenye chungwa, husaidia kuondoa tatizo la shinikizo la damu la juu (high blood pressure), hivyo machungwa ni mazuri kwa wagonjwa wa presha. 4. UGONJWA WA MAPAFU Chungwa pia lina kiasi kikubwa

TAZAMA JINSI DIAMOND NA RAISI KIKWETE WANAVYOKULA BATA HUKO MAREKANI.

Image
Na haya Ndio maneno aliyoandika Msanii Diamond baada ya kukutana Na Rais " No where else you can get such a president who sacrifices his precious time to support his artist to get international connection than Tanzania/Home of peace and hospitality" 

INASIKITISHA SANA DUNIA IMEKWISHA...MSICHANA ABAKWA NA WANAUME ZAIDI YA 38

Image
Kuna baadhi ya binadamu wana roho mbaya zaidi ya wanyama wakali wa mwituni na ukisimuliwa matukio waliyofanya unaweza kujiuliza kama kweli ni binadamu au ‘mashetani’!  Siku mbili baada ya kuripotiwa habari ya kusikitisha ya wasichana wawili ndugu wa nchini India waliobakwa na baadae kunyongwa, mtandao wa MailOnline umeripoti tukio la ubakaji alilofanyiwa msichana mdogo mwenye umri wa miaka 15 na wanaume zaidi ya 38 nchini Malaysia.  Taarifa zinaeleza kuwa tukio hilo limefanyika Kaskazini mwa Kelantan, Malaysia, May 20 ambapo msichana huyo alienda sehemu fulani kukutana na rafiki yake mwenye umri wa miaka 17 lakini alijikuta akipelekwa kwenye jumba bovu wasiloishi watu.  Akiwa kwenye jumba hilo, msichana huyo alibakwa kwa zamu na wanaume hao ambao miongoni mwao ni kundi la watu wanaojihusisha na matumizi ya madawa ya kulevya.  Msichana wa miaka 17 ambaye ni rafiki ya msichana huyo anasadikika kuwa ndiye aliyemtenezea mazingira ya kuingia mikononi mwa watu hao w

DEVOTHA ATOA WOSIA WA KIFO CHAKE

Image
Stori: Gladness Mallya WAKATI vifo mfululizo vikitokea Mei mwaka huu miongoni mwa wasanii maarufu nchini, nyota wa filamu Bongo, Devotha Mbaga ameibuka na kusema endapo ataaga dunia, hahitaji kufanyiwa mbwembwe wakati wa msiba na mazishi yake kama wasanii wengine walivyofanyiwa. Msanii maarufu wa filamu Bongo, Devotha Mbaga. Akistorisha na gazeti hili, Devotha alisema hatahitaji kununuliwa jeneza la kifahari, bali lichongwe kwa mbao za kawaida na lisiwekwe mapambo yoyote, watu wasilie msibani kwake na kwamba endapo vitu hivyo vitakiukwa, basi mwili wake utagoma kubebeka. “Unajua duniani nimekuja uchi, sasa siku nikifa sitaki mbwembwe za kununuliwa jeneza la mamilioni wakati nimeacha watoto, ni bora hizo fedha wapewe wanangu ziwasaidie, vivyo hivyo pia sitaki watu walie kwa kuomboleza kwenye msiba wangu kwa sababu watakuwa wananiumiza tu, hata watoto na ndugu zangu nilishawaambia,” alisema Devotha. Devotha Mbaga (kulia) akiwa katika moja ya misiba ya wasanii wenzake.

ANGALIA PICHA ZA MAELFU YA WATU WAGAWANA NA KULA NYAMA YA KIBOKO TUNDUR

Image
 Wakazi wa wilaya ya Tunduru wakigawana  nyama ya Kiboko huku mmoja akimnyooshea mwenzie fimbo baada ya jamaa kutaka kuleta fujo wakati wa kugawana nyama hiyo. Na Steven Augustino wa demashonews, Tunduru WANANCHI wa Mji wa Tunduru Mkoani Ruvuma wamemuua  Kiboko aliye muua Mkazi wa Kitongoji cha Chacha katika Kijiji cha Mhuwesi katika kata ya Mhuwesi Tarafa ya Nakapanya Marehemu  Njaidi Selemani Njaidi (70) na kumla nyama yake bila kujali dini zao. Katika kuonesha kuwa Mnyama huyo analiwa na waumini wa dini zote Maelfu ya wananchi walijitokeza kumlinda asitoke hadi usiku wa saa 9 walipotokea askali wa idara ya wanyamapori na kumpiga risasi. Aidha hali ilikuwa tete baada ya Kiboko huyo kuuawa ambapo mamia ya vijana wenyeguvu walijitokeza na kujitosa katika bwawa hili na kuanza kumshambulia kwa kutakata nyama hiyo huku wakiwa wanagawana na mwisho kikaja Kivutio amakioja cha kuwatishia visu askari wa idara hiyo na kuwapora ndoo 8 za nyama hiyo ambayo ilia