Posts

Showing posts from September 2, 2015

Hivindivyo Watu Mbali Mbali Walivyosema Huko Facebook Baada ya Hotuba ya DR Slaa Leo

Image
'Chadema kama chama kilichokomaa na kinachojiandaa kushika dola hakina haja wala sababu ya kumjibu Dr. Wilbrod Slaa. Machungu yake tunayatambua ila kwasasa hatuna jinsi ni lazima tusonge mbele kuitoa hii nchi kwenye umasikini. Juhudi na kazi zake katika Chadema tunayatambua, tunaziheshimu na tutazienzi. Kwaheri Dr. Wilbrod Slaa   ' By Renatus Kyakalaba " Sitashangaaa kuona akili ndogo wakianza kumtukana Dr.Slaa,,,baada ya hii hotuba yake inayoweka Black and White Out,,,,, "  By Baraka Samson Chipanjilo ' Sikuwahi mpinga Dr huyu toka nianze kumuona kwenye siasa, Leo kwa mara ya kwanza nimelisikia neno rahisi sana LA kuwa ukawa wanabeba watu kwenye malori na mabasi, cheap statement! Hili nakupinga Hakuna aliyefika uwanjani usiku huo uliosema ila kulikuwa na walinzi wa jukwaa na vyombo kulikuwa na daladala mbili zilikodiwa na wafuasi kwa mapenzi yao, Dr please mdomo usiuruhusu useme yote maneno yana kawaida ya kama yakiwa marefu sana huwa baadh

Tundu Lissu: Dr. Slaa ni Muongo, Watanzania Mpuuzeni! Maneno Yote Tatizo ni Urais...

Image
Akihojiwa na redio station mh.Lissu anasema ameshangaa sana maneno aliyoyasema leo kwenye mkutano wake na waandishi wa habari. Anasema Dr.Slaa alikwisha kuteuliwa kuwa mgombea urais mwezi January na mwezi April akathibitishwa na kamati kuu, Anaendelea kusema ameshangaa Dr.Slaa kusema Gwajima ndo alimleta Lowassa jambo ambalo siyo kweli kabisa, yeye Dr. Slaa mwezi wa tano ndo alianza kumtafuta Lowassa kwa kumtumia Gwajima Anasema wakati Lowassa anapokelewa tarehe 27 July kwenye Kamati Kuu, Dr.Slaa hakulala nyumbani aliporudi nyumbani mchumba wake alimtupia mabegi nje na DR. alilala kwenye gari. Anasema dr. slaa asiwadanganye watanzania tatizo ni urais na mchumba wake. Anasema ameacha siasa tangu siku ya kikao cha kamati kuu alipoandika barua ya kujiudhuru kwa nini amepokea mshahara wa mwezi huu?? kwanini anaendelea kutumia gari la chama la katibu mkuu na nyumba aliyonunuliwa na chama muulizeni awaambie kwanini anaendelea kunufaika na hayo yote toka CHADEMA??

SOMA MAGAZETI YA LEO JUMATANO TAREHE 02.09.2015

Image

MAGAZETI YA UDAKU LEO TAREHE 2/9/2015

Image
Posted by JAFE MALIBENEKE at Wednesday, September 02, 2015

SERIKALI YASEMA HAKUNA DENI HALALI LA WALIMU AMBALO HALIJALIPWA.

Image
Na Magreth Kinabo- maelezo SERIKALI imesema kwamba imeshalipa madeni ya walimu  ya kiasi cha Sh. bilioni 5.7 ambayo yaligungulika kihalali kati ya Sh. bilioni 19.6 zilizokuwa zinadaiwa kudaiwa,hivyo  kwa  sasa hakuna  malalamiko mwalimu ambaye hajalipwa. Aidha Serikali imependekeza kwamba   halimashauri  zilizowasilisha  madeni ambayo si  halali, yenye shaka, au watumishi wasio na madai, madai ya watumishi wasio na madai, madai ya watumishi waliokwishalipwa na waliowasilisha madai ya mishahara kama madai yasiyo ya mishahara wawajibishwe. Kauli hiyo imetolewa leo na Katibu Mkuu wa Wizara ya  Fedha, Dkt.  Servacius Likwelile  wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kwenye ukumbi wa mikutano wa wizara hiyo jijini Dar es Salaam. Dkt.   Likwelile   alisema hayo wakati akitoa taarifa  ya  uhakiki wa madeni ya  walimu wa shule za msingi, sekondari na  Watumishi wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya  Ufundi Stadi.  Alisema awali wizara yake ilipokea madai ya

LOWASSA ACHANYA MBUGA,JANA ATIKISA RUVUMA

Image
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungani wa Tanzania katika mwamvuli wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa akihutubia maelfu ya wananchi wa mji wa Songea Mjini, kwenye Mkutano wa hadhara wa Kampeni, uliofanyika kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Matarawe, Songea Mjini, Mkoani Ruvuma leo Septemba 1, 2015. Picha na Othman Michuzi, Ruvuma.  Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungani wa Tanzania katika mwamvuli wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa akihutubia maelfu ya wananchi wa mji wa Songea Mjini, kwenye Mkutano wa hadhara wa Kampeni, uliofanyika kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Matarawe, Songea Mjini, Mkoani Ruvuma leo Septemba 1, 2015. Picha na Othman Michuzi, Ruvuma. Maelfu ya wakazi wa Songea wajitokeza kumsikiliza Mgimbea wa Chadema, Edward Lowassa. Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungani wa Tanzania katika mwamvuli wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia n

MAMA SAMIA ACHANJA MBUNGA LEO CHAMWINO, KONGWA NA MPWAPWA MKOANI DODOMA KUSAKA KURA

Image
Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akiwasili kufaya mkutano wakampeni leo, katika eneo la Chinolwa Nzali,katika jimbo la Kongwa mkoani Dodoma leo. Shamrashamra za ngoma zikirindima, Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akiwasili kufaya mkutano wakampeni, katika eneo la Chinolwa Nzali,katika jimbo la Kongwa mkoani Dodoma leo. Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akiwasili kufaya mkutano wakampeni leo, katika eneo la Chinolwa Nzali,katika jimbo la Kongwa mkoani Dodoma leo. Shamrashamra za mapokezi zilitia fora, Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akiwasili kufaya mkutano wakampeni leo, katika eneo la Chinolwa Nzali,katika jimbo la Kongwa mkoani Dodoma. Mmoja wa wajumbewa Kamati ya Kampeni za Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Ummy Mwalimu, akihamasisisha, wakati, Mgombea huyo Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Sami