Posts

Showing posts from February 1, 2014

JE, NI KWELI UKIMFANYIA MSICHANA MAMBO HAYA HATAKUACHA?

Image
Habari yako ndugu msomaji? Natumaini u mzima na mwenye afya njema.     1.   KILA siku usisahau kumsifia kwa kumwambia ni kiasi gani alivyo mzuri. Kumbuka kila msichana anapenda kusifiwa hivyo unapomuambia yeye ni mzuri anaona una mthamini kuliko msichana yeyote awaye. 2. Wakati wowote ukipata nafasi muandikie barua au msg kwenye simu mueleze hisia zako kiasi gani unampenda. Kumbuka wasichana hupenda kusikia zaidi kutoka kwa wapenzi wao ni kiasi gani wanapendwa. Haitakiwi iwe tu katika kipindi cha siku ya wapendanao ndio umuoneshe kuwa unampenda. Muoneshe msichana ni kiasi gani yeye ni muhimu sana kwako. 3. Busu la ghafla na kumshika mkono wakati mkitembea pamoja itamfanya yeye kujisikia raha zaidi. Na wakati mwingine msuprise kwa kumtembelea mara kwa mara hi humfanya akuone wewe ni mtu muhimu pale usipokuwa naye karibu na kumfanya kukuhitaji zaidi ukiwa naye mbali 4. Tambua mahitaji yake. Uwe msaada kwake kipindi ambacho mpenzi wako amekasirika kuwa pale kwa aji

HAWA NDIO POLISI WATANO WALIOFARIKI DUNIA PAPOHAPO KATIKA AJALI YA GARI MKOANI DODOMA

Image
Na. Sylvester Onesmo wa Jeshi la Polisi Dodoma. Askari polisi watano mkoani dodoma wafariki dunia papohapo katika ajali ya gari iliyotokea 31/01/2014 majira ya 23.45 hrs katika barabara kuu ya Dodoma – Morogoro eneo la Mtumba Center, Kata ya Mtumba Tarafa ya Kikombo Manispaa ya Dodoma, ambapo gari namba T.770 ABT Toyota Corolla lililokuwa likiendeshwa na Askari namba H. 3783 PC DEOGRATIUS wa Polisi Wilaya ya Kongwa likitokea Dodoma mjini likielekea Wilayani Kongwa liligongana uso kwa uso na gari namba T.997AVW Scania Bus mali ya Kampuni ya Mohamed Trans lililokuwa likiendeshwa na JUMA s/o MOHAMED, miaka 38, Mkazi wa Mwanza, likitokea Dar es Salaam kuelekea Dodoma na kusababisha vifo kwa askari watano papohapo.  Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi DAVID MISIME amewataja Askari hao waliofariki katika ajali hiyo kuwa ni:- 1.          D.9084 D/CPL. ADOLF S/O MESHACK SILLA mwenye miaka 51, Mgogo. 2.          F.

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AFUNGUA MKUTANO MKUU WA MWAKA WA JUMUIYA YA ISTIQAAMA DAR

Image
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akuhutubia wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa mwaka wa Jumuiya ya Istiqaama, uliofanyika katika Ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam, leo Feb 01, 2014. Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwasili kwenye Ukumbi wa Karimjee kwa ajili ya kufungua rasmi Mkutano Mkuu wa Jumuiya ya Istiqaama, leo Feb 01, 2014. Baadhi ya Wanachama wa Jumuiya ya Istiqaama, wakimsikiliza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungani wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wakati alipokuwa akihutubia kufungua rasmi Mkutano Mkuu wa Jumuiya hiyo leo katika Ukumbi wa Karimjee. Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum, baada ya kufungua rasmi Mkuu wa Jumuiya hiyo leo katika Ukumbi wa Karimjee. Picha ya pamoja baada ya kufunguliwa mkutano huo.Picha na OM

ANGALIA NAFASI ZA KAZI CHUO CHA UHASIBU ARUSHA

Image
HUMAN  RESOURCES  AND ADMINISTRATIVE OFFICER  I - 2 POSITIONS Qualifications: Holder of Bachelor degree in Public/Business Administration,Human Resources,or Industrial Relations from a recognised university/Institution Apply: Rector Institute of Accountancy Arusha Box 2798, Arusha Details:Daily News 23 Jan, 2014 Deadline: 7 February, 2014 PUBLIC RELATIONS OFFICER I Qualifications: Holder of Bachelor degree in Business Administration,Marketing Mass Communication,Public Relations or its equivalent from a recognised university/Institution Apply: Rector Institute of Accountancy Arusha Box 2798, Arusha Details: Daily News 23 January, 2014 Deadline: 7 February, 2014 PROCUREMENT AND LOGISTICS OFFICER  I Qualifications: Holder of Bachelor degree in Procurement and Logistics Management or its equivalent from a recognised university/Institution Apply: Rector Institute of Accountancy Arusha Box 2798, Arusha Details: Daily News 23 January, 2014

ANGALIA NAFASI ZA KAZI MUHIMBILI

Image
PERSONAL SECRETARY II  - 2 POSITIONS Qualifications: Form IV Certificate with credit passes in Kiswahili and English,plus 80 shorthand and 50 w.p.m typing speed Apply:  The Deputy Vice Chancellor, Planning Finance and Administration Muhimbili University of Health and Allied Sciences Box 65001, Dar es Salaam Details: Daily News 22 January, 2014 Deadline: 04 February, 2014 LECTURER  - 2 POSITIONS Qualifications: Appropriate PhD or MMed/MDent. A Minimum GPA of 3.8 in the Undergraduate Training from recognised University Apply:  The Deputy Vice Chancellor, Planning Finance and Administration Muhimbili University of Health and Allied Sciences Box 65001, Dar es Salaam Details: Daily News 22 Jan, 2014 Deadline: 4 February, 2014 SENIOR  INTERNAL  AUDITOR GRADE II Qualifications: CPA(T),ACC/ACA OR CMA with a working experience of four years at a similar position in a reputable organisation Apply:  The Deputy Vice Chancellor,Planning Fina

ANGALIA PICHA AJALI YA BASI BARABARA YA NYERERE

Image
Kikosi cha jiji cha uokoaji na zimamoto wakishirikiana na polisi trafiki kuzima moto uliokuwa ukiteketeza basi la abiria katika eneo la Vingunguti Barabara ya Nyerere Dar es Salaam leo . (PICHA NA ROBERTOKANDA BLOG) Mizigo iliyookolewa kutoka kwenye basi hilo kabla ya kushika moto. Y

DK.SHEIN AWASILI NCHINI INDIA LEO

Image
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akipokea mashada ya mauwa   wakati wa mapokezi nyake alipowasili katika uwanja wa ndege wa Jaipur Nchini India katika Jimbo la Rajastan,akiwa na ujumbe aliofuatana nao akiwemo mkewe Mama Mwanamwema Shein katika ziara rasmi.[Picha na Ramadhan Othman, India.] Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana  na Kiongozi wa Ulinzi  wakati wa mapokezi  yake alipowasili  katika uwanja wa ndege  wa Jaipur  Nchini India katika Jimbo la Rajastan,akiwa na ujumbe aliofuatana nao akiwemo mkewe  Mama Mwanamwema  Shei.[Picha na Ramadhan Othman, India.] Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein na Mkewe Mama Mwanamwema Shein  wakisalimiana na Viongozi   wakati wa mapokezi  alipowasili katika uwanja wa ndege wa Jaipur Nchini India katika Jimbo la Rajastan,pamoja na   ujumbe  waliofuatana katika ziara rasmi nchini India[Picha na Ramadhan Ot

HADIJA KOPA AITEKA MBEYA

Image
 Malkia wa Taarab nchini Bi. Hadija Kopa akiimba mbele ya umati wa watu kwenye ukumbi maarufu wa City Pub mjni Mbeya.  Baadhi ya wanamuziki wa TOT Taarab wakiimba kwa hamasa wakati band hiyo ya muziki wa taarab ilipotumbuiza kwenye ukumbi wa City Pub mjini Mbeya.  Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akimpongeza bi Hadija Kopa kwa umahiri wake wa kuimba taarab kwenye ukumbi wa City Pub Mbeya. Umati wa watu ukiwa umefurika wakati Malkia wa Taaarab Hadija Kopa na Band ya Taarab ikitoa burudani kwa wakazi wa Mbeya mjini.

HII NDIO LISHE KWA WANAOISHI NA UKIMWI

Image
Tatizo la VVU/UKIMWI linaendelea kuwa tishio kwa maisha ya binadamu. Pamoja na jitihada mbalimbali za kitabibu, imeonekana kuwa watu wengi wanaoishi na virusi vya UKIMWI (VVU) au UKIMWI huathirika au hupoteza maisha yao mapema zaidi kwa kukosa lishe bora. Lishe bora kwa watu hawa ni muhimu ili kuimarisha kinga ya mwili, ambayo huuongezea mwili uwezo wa kupigana na magonjwa nyemelezi na hivyo kumfanya mtu anayeishi na VVU/UKIMWI kuishi muda mrefu zaidi. Vile vile lishe bora huuwezesha mwili wa mtu anayeishi na VVU/UKIMWI kustahimili dawa anazotumia. Lishe bora hutokana na kula chakula mchanganyiko na cha kutosha. Pamoja na lishe bora, mazoezi ya mara kwa mara ni muhimu vile vile katika kuimarisha kinga ya mwili na kuupa mwili uwezo wa kupigana na magonjwa nyemelezi. Watu wanaoishi na VVU/UKIMWI huweza kupata matatizo mbalimbali yanayoweza kuwafanya washindwe kula vizuri au chakula kisiweze kutumika ipasavyo mwilini na hivyo kudhoofisha zaidi k