Posts

Showing posts from April 6, 2018

Kitwanga: Ukiwa msema Ukweli lazima wakuondoe

Image
Mbunge wa Misungwi, Charles Kitwanga amefunguka na kusema kuwa mtu ukiwa msema ukweli lazima wakuondoe katika nafasi yako kwa kuwa hawataki watu wasema kweli. Kitwanga amesema hayo bungeni alipokuwa akichangia mjadala wa kupitisha makadirio ya mapato na matumizi ya ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka wa fedha 2018/2019, mjini Dodoma na kudai hata ukiwa mtenda haki kwa kila mtu lazima wakuhamishe. "Kichwa changu na kichwa cha Jenista Mhagama ni vichwa viwili tofauti kabisaa na uwezo wetu wa kufikiri upo tofauti kabisaa, kwa hivyo ni vyema tukapima na kuhakikisha kwamba pale anapofaa Jenista Mhagama aende Jenista Mhagama, pale anapofaa Kitwanga aende Kitwanga lakini hii ya kubebe jumla jumla na wakati mwingine ndugu zetu hii tabia ife na mimi siwezi kukubaliana na hilo na bahati nzuri ukiwa msema ukweli hata ukikaa pazuri watakuondoa tu. Na ukiwa unatenda haki kwa kila mtu hata ukikaa Kolomije watakuondoa wakupeleke Mtwara" alisisitiza Kitwanga May 21, 201

Jacob Zuma amefikishwa Mahakamani

Image
Aliyekuwa rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma amefikishwa mahakamani leo katika mji wa Durban ili kujibu mashtaka ya rushwa, udanganyifu na kujitajirisha kinyume cha sheria. Kesi hii inasikilizwa kwa mara ya kwanza na inahusu biashara ya zamani ya mauzo ya silaha tangu miaka ya 1990.  Rais wa zamani wa Afrika Kusini anashutumiwa kupokea rushwa kutoka kwa Thomson CSF – jina la zamani la kampuni ya Thales – katika mpango wa mkataba wa mauzo ya silaha wenye thamani ya karibu Euro Bilioni 4 ulioafikiwa mnamo mwaka 1999. Wakati huo, Jacob Zuma alikua makamu wa rais wa nchi ya Afrika Kusini. Anashutumiwa kuwa alipokea jumla ya euro milioni 50 kutoka kampuni ya Ufaransa ya Thales. Kwa upande mwingine, aliahidi kupatishia zabuni kampuni hiyo ya Thales. Kwa jumla, Afrika Kusini iliamua kutumia zaidi ya dola bilioni 10 kurejelea upya silaha zake. Silaha ambazo nchi hiyo haikuweza kuzihitaji wakati huo na ambaz

Rais wa zamani wa Korea Kusini amehukumiwa miaka 24 jela

Image
Rais wa zamani wa Korea Kusini  Park Geun-hye, amehukumiwa miaka 24 jela baada ya kukutwa na hatia katika matumizi mabaya ya madaraka na kusababisha nchi kushuka kiuchumi. Park Geun-hye aliondolewa madarakani mwaka jana baada ya kutuhumiwa kutumia vibaya wadhifa wake na kusababisha kuanguka kwa uchumi. Rafiki yake Choi Soon-sil, anayehusishwa na kashfa hiyo, alihukumiwa wiki mbili zilizopita hadi miaka 20 jela kwa kupokea hongo iliyotolewa na makampuni ya Korea Kusini, ikiwa ni pamoja na makampuni yai Samsung na Lotte. Katika mashtaka yake, mwendesha mashtaka alimshtaki rais wa zamani kuwa “alisababisha mgogoro wa kitaifa kwa kuacha mtu ambaye hajawahi kushiriki katika usimamizi wa umma kuongoza nchi”. Kesi ya rais wa zamani Korea Kusini ilifunguliwa mwezi Mei mwaka jana. Mahakam inatarajia kutoa uamuzi wake kabla ya mwezi April mwaka huu.

Rais Magufuli atoa Shilingi milioni 100 kumtibu Mgunduzi wa Tanzanite

Image
Leo April 6, 2018 Rais John Magufuli katika Uzinduzi wa Ukuta wa Mirerani amesema serikali yake itatoa kiasi cha Shilingi milioni 100 kwa ajili ya matibabu ya Mzee Jumanne Ngoma ambaye ndiye mgunduzi wa madini ya Tanzanite . Rais Magufuli ameeleza kuwa serikali inatoa pesa hiyo ili Mzee Ngoma ambaye anasumbuliwa na maradhi ya kupooza akapatiwe tiba kwani ugunduzi wake ndio ulioweka historia ya nchi ya Tanzania kumiliki madini hayo. Takriban mwezi mmoja uliopita Mzee Ngoma alifanyiwa mahojiano na Ayo TV na millardayo.com na kueleza kuwa anatamani kuonana na Rais Magufuli ili amueleze adha anayokutana nayo na jinsi ambavyo kuona hathaminiwi wala kunufaika na chochote licha ya ugunduzi alioufanya. Mzee Ngoma anadaiwa kugundua madini hayo miaka 52 iliyopita .

Cecilia Pareso aseama kama mnataka futeni yu Vyama vya Upinzani

Image
Mbunge wa Viti Maalum Chadema, Cecilia Pareso amesema kama serikali ina lengo la kuwabana na kuwanyima haki wapinzani, basi ni bora mfumo wa vyama vingi ukafutwa ili ifahamike kwamba nchi ni ya chama kimoja. Pareso ameyasema hayo jana Aprili 5, Bungeni Mjini Dodoma wakati akichangia katika Mjadala wa Bajeti ya Wizara ya Ofisi ya Waziri Mkuu mwaka 2018/19 huku akidai kwamba vyama vya upinzani vimekuwa vikionewa ikiwemo viongozi wake kukamatwa mara kwa mara na kufunguliwa mashtaka huku wengine wakifungwa jela. Amesema vyama hivyo vimekuwa ni adui mwingine kwa kuwa kwa sasa vinapigwa vita na Serikali iliyopo madarakani, kuzuiwa kufanya shughuli za siasa majukwaani. Pia alidai chaguzi ndogo zilizofanyika hivi karibuni, zilikuwa ni kati ya Chadema na Jeshi la Polisi na kudai kwamba wabunge na madiwani walinunuliwa, wakahama vyama vyao, hivyo kukalazimika kufanyika chaguzi nyingine ndogo alizodai zimegharimu zaidi ya Sh bilioni 6. “Kama mnakataza vyama vya siasa visif

Breaking News: Wambura Ashindwa Rufaa Yake, Ataendelea na Kifungo

Image
Aliyekuwa Makamu wa Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Michael Richard Wambura. Kamati Ya Rufaa Maadili Ya TFF baada ya kupitia rufaa ya aliyekuwa Makamu wa Rais wa Shirikisho hilo,Michael Richard Wambura imetupilia madai yake yote na adhabu yake itaendelea kama ilivyoamuliwa na  Kamati ya Maadili ya TFF kwa kufungia kutojihusisha na soka maisha yake yote. Mbali na hilo pia kamati hiyo ya rufaa imeshauri, Wambura afikishwe kwenye vyombo vya dola ili suala hilo liweze kushughulikiwa zaidi na wataalam