Posts

Showing posts from August 28, 2013

KWELI HUU NI USHETANI KWA RIHANA ANGALIA HIZI PICHA ZAKE NDO UTAAMINI MWENYEWE

Image
HATARIIII...:

HATIMAYE AUNT EZEKIEL AFUNGUKA NA KUWEKA WAZI ISHU NZIMA YA KUSHAMBULIWA NA CHUPA AKIWA CLUB NA MDADA

Image
MWIGIZAJI wa  sinema za kibongo, Aunt Ezekiel Grayson ‘Gwantwa’ amenusurika kupasuliwa paji la uso kwa chupa baada ya kupigwa mkononi... Usiku wa kuamkia Jumatatu, nje ya Ukumbi wa Billicanas, mwanamke aliyejulikana kwa jina moja la Yvonne alimpiga Aunt kwa chupa tupu ya bia na kumpasua mkono wa kushoto. Watu walioshuhudia tukio hilo wamedai  kuwa, wakati Yvonne anatekeleza ukatili huo, Aunt alikuwa amesimama na marafiki zake waliotajwa kwa jina moja moja, Sajenti na Rehema.   “Ndani ya ukumbi shoo ilikuwa ikiendelea, Aunt, Rehema na Sajenti walisimama nje, ghafla alitokea Yvonne akiwa na chupa mkononi, akailenga kwenye paji la uso la mwenzake, bahati nzuri Aunt aliiona na kukinga mkono,” kilisema chanzo. Kikaendelea: Vurugu kubwa ilizuka, ilibidi shoo ndani isimame ili kushughulia suala hilo. Aunt alikimbizwa Aga Khan, Yvonne akapelekwa msobemsobe Kituo cha Polisi cha Oysterbay, Dar ambapo anashikiliwa. Baada ya taarifa hizo, juzi m

BUNGE LA AFRIKA MASHARIKI MOTO,WABUNGE WA TANZANIA WATOKA NJE KUPINGA WABUNGE WA NCHI NYINGINE KUTOKA NJE KUSHINIKIZA HOJA ZAO

Image
Spika wa Bunge la Afrika Mashariki(EALA)Magreth Zziwa akimsikiliza mbunge wa bunge hilo kutoka Tanzania,Shyrose Bhanji wakati wakielekea bungeni. Spika akiongoza kikao cha leo mchana ambacho kiliahirishwa baada ya wabunge wa Tanzania kutoka nje Wabunge wa Tanzania kwenye bunge la Afrika Mashariki(EALA)wakitoka ndani ya ukumbi wa bunge hilo leo kupinga wabunge wenzao wanaoshinikiza hoja zao kwa kutoka kwenye vikao vya bunge hali inayoshusha hadhi ya Spika,bunge na wabunge wenyewe,kutoka kushoto ni Mh.Twaha Taslima,Mh.Shyrose Bhanji,Mh.Abdula Mwinyi na Nderakindo Kessy Mbunge wa Tanzania kwenye bunge la Afrika Mashariki(EALA)akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari yalipo makao makuu wa Afrika Mashariki jijini Arusha baada ya kutoka nje na kikao kuhairishwa hadi kesho Kiongozi  wa baraza la Wawakilishi Zanzibar,Ali Mzee(kulia)akizungumza na wabunge wa Tanzania kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki(EALA)kutoka kushoto ni M

HUYU NDO JAMAA ALIEMSHIKA RIHANNA MAKALIO WAKIWA JUKWAANI AFUNGUKA UHUSIANO WAKE NA RIHANNA...!!

Image
Kufuatia rapa A$ap Rocky kuonekana katika pozi za utata na Rihanna hivi karibuni na kufikia hatua ya watu kuanza kufikiri kuwa huenda kuna kitu kimeanza kati yao, Rapa huyu ameamua kufafanua kilichokuwa kinatokea eneo la tukio. A$ap Rocky amesema kuwa hataki kujiingiza katika matatizo ya tetesi kumhusu yeye na Rihanna kwasababu hakuna kitu chochote kinachoendelea kati yao, na yeye na Rihanna ni marafiki wakubwa tu. Rapa huyu amesema kuwa anampenda Rihanna kwasababu anasapoti kazi zake na hakuna cha ziada, ingawa taarifa za chini chini zinaweka wazi kuwa, Tokea wawili hapa walipofanya tour pamoja, wamejijengea ukaribu wa ajabu ambao unazua maswali mbalimbali kila mara wanapokuwa pamoja

ANGALIA PICHA YA MDADA ANAYE DAIWA KUMJERUHI AUNT EZEKIEL KWA CHUPA

Image

HAYA NDIO MAJANGA YA SHILOLE KWA SASA ANAYOFANYA ANAPOKUWA JUKWANI, SHUHUDIA MWENYEWE

Image

RAY C AANZA KUKIRUTUBISHA KIUNO CHAKE....HIZI NI PICHA 3 AKIWA GYM

Image
Zaidi ya sauti yake na uwezo mkubwa wa kuimba nyimbo zinazoshikika kiurahisi, umaarufu wake mwingine mkubwa toka enzi hizo ni kiuno bila mfupa kwa jinsi alivyokua akicheza nacho.Huu  ni uwezo uliofanya mpaka maneno ya kiuno bila mfupa yakapata umaarufu kupitia yeye.   Siku kadhaa  baada ya kutangaza kurudi kwenye muziki kama zamani, Ray C akiwa ametoka kwenye matibabu ya matumizi ya dawa za kulevya  ameanza kujipanga kupunguza unene alionao ili awe mwepesi zaidi ya alivyo sasa ili kila kitu kiende kama kilivyokua.   Ray C akipiga story na fans wake alisema “Mauno ni nyonga si manyama” ....hii ni moja ya sababu za msingi sana zilizomfanya Rehema Chalamila kuingia gym kuanza mazoezi.    

MWONEKANO WA AUNT EZEKIEL AKIWA KALAZWA AKIPATIWA MATIBABU

Image
MWIGIZAJI wa kike katika tasnia ya filamu Bongo Aunty Ezekiel imeripotiwa kupata majeraha katika mkono wake wa kushoto baada ya kuchimbwa na chupa yenye ncha kali, sakata hilo la hatari lilitokea Club  Billicanas wakati wa show iliyokifanyika hapo chini ya Madam Wema Sepetu chanzo chetu kimetuhabarisha. Chanzo cha ugomvi hadi leo bado kitendawili baada ya kutoka fununu kuwa uenda ugomvi huo unahusishwa na kumgombea bwana yaani mwanaume ambaye waliwahi kumgombea siku za nyuma lakini kupigana kidogo ambapo mmoja alitoka nduki na kuacha msala ukitulia. Chanzo chetu bado kinafuatilia tukio hilo kwa ukaribu kisha tutakujuza kulikoni hadi nyota wetu kutaka kuharibiwa show yake ambayo ndio inapa ajira katika uigizaji, tunampa pole kwa majeraha yaliyompata , huku tukisubiri atusimulie sakata leo hakuwa tayari kupokea simu yetu.

Zitto: Sitogombea Urais wala Ubunge 2015

Image
Mbunge wa kigoma kaskazini bwana Zitto Kabwe kafichua siri nzito na kudai hana mpango wa kugombea urais mwaka 2015 na wala hatagombea ubunge ila anataka kutafuta chuo na awe mwalimu wa chuo na analenda sasa kufundisha maswala ya uchumi na mazingira ndio dhamira yake.