Posts

Showing posts from September 27, 2013

WEMA SEPETU AIPASUA KATIKATI CLUB YA BONGO MOVIE BAADA YA RAY KUWAKATAZA WASANII WASIHUDHURIE MSIBA WA BABA YAKE

Image
Wema Sepetu Klabu ya Bongo Movie ambayo inaundwa na baadhi ya wasanii wa filamu Swahiliwood imepasuka katikati kisa kikidaiwa kuwa ni lile tamko linalodaiwa kutolewa na mwenyekiti wa klabu hiyo, Vincent Kigosi ‘Ray’ kuwa mwanachama yeyote wa kundi hilo asitie miguu kwenye msiba wa baba mzazi wa mwenzao, Wema Sepetu, marehemu Balozi Isaac Sepetu. Tukio hilo la katazo lilitokea wakati wa maombolezo ya kifo cha mzee Sepetu kilichotokea Oktoba 27, mwaka huu katika Hospitali ya TMJ kwa ugonjwa wa kisukari ambapo msiba ulikuwa nyumbani kwake, Sinza Mori jijini Dar es Salaam. LAWAMA ZOTE KWA RAY Kufuatia madai hayo, baadhi ya wasanii kutoka klabu ya Bongo Muvi (majina tunayo) wamekuwa wakitoa lawama zao kwa Ray huku wengine wakidai wamejitoa kwenye kundi hilo kwa sababu halina umoja na limejaa unafiki. Maneno hayo yalianza kusambaa baada ya Wema kumaliza kumzika baba yake Oktoba 31, mwaka huu mjini Zanzibar. Wema Sepetu (katikati) baada ya kuwasil

KIZAAZAA MISS WORLD HATARINI KUSHAMBULIWA

Image
IKIWA imebaki siku moja tu mashindano ya urembo ya Dunia kufanyika katika kisiwa cha Bali yalipohamishwa kutoka mji mkuu Jakatra nchini Indonesia, Hali imeonekana kuwa tete baada ya wanachi wa nchi hiyo ambao wengi wao ni waislam kuyapinga mashindani hayo kwa maandamano huku makundi mbali mbali ya kiislam yakitishia kushambulia mashindano hayo siku ya shindano. zaidi ya asilimia 90 ya watu milioni 240 ni waislam Nchini Indonesia Waandaaji wamesema ulinzi ni wa uhakika katika milango ya kuingilia kwenda katika kisiwa hicho cha bali mashindano hayo yatakapofanyika Jumamosi Dec 28 huku warembo 129 kutoka nchi mbali mbali duniani watashiriki mashindano hayo wakati Tanzania ikiwakilishwa na mrembo Brigitte Alfred.

JE, UNAWAKUMBUKA HAWA PACHA. HAYA NI MAAJABU YA MUNGU

Image
 Hawa ni mapacha wanaoishi Tanzania  Hawa ni mapacha wanaoishi India