Posts

Showing posts from March 5, 2016

YATAMBUE MADHARA YA KUTOSHIRIKI TENDO LA NDOA KWA MUDA MREFU ( WANANDOA)

Image
kwa kawaida kama wewe si mgonjwa wa aina yoyote ile, kwa maana ya ugonjwa ku-offset system ya mwili, madhara ya kutofanya tendo la ndoa kwa muda mrefu ni makubwa kuliko unavyofikiria as long as upo katika active range of age! madhara yapo ya Negative na positive. Mfumo wa fahamu (central novous system) hutumia zaidi tendo la ndoa ku-radiate energy inayowezesha ubongo pamoja na mifumo mingine ya mwili kufanya kazi zake vizuri bila msongo. Suala hapa si lazima uk*e na u*me kukutana na kuingiliana (penetration) ila tu stimulation(msisimko) inayofikisha mtu kileleni (orgasms). kwahiyo, nature(asili) inataka mke na mme kufanikisha zoezi hili maana ni jambo muhimu kama ilivyo kutoka jasho mwilini maana sio tu mwili unaondoa uchafu ndani lakini pia inacontrol joto la mwili (cooling effect). Anayesema amekaa zaidi ya mwaka na hana madhara.., well sikatai wala sikubali maana hatuna ushahidi nalo lakini zipo njia nyingi mbadala kama kutumia s*x toys, dildo(vibrant

AY AWATOLEA UVIVU TCRA

Image
Ambwene Yessaya ‘AY’ amethibitisha kupokea taarifa ya kufungiwa kwa video ya wimbo ‘ Zigo remix’ aliyomshirikisha Diamond Platnumz. Akizungumza na 225 katika kipindi cha XXL cha Clouds FM, Jumatatu hii, AY amesema alipokea barua yenye amri hiyo kutoka kwa rafiki yake ambae anafanya kazi katika chombo kimoja cha habari. “Sijaelewa maadili gani kwa sababu kama maadili niliyokosea mimi ni kushoot kwenye swimming pool, na kama kwenye swimmig pool watu nimevalisha jeans au maturubai hapo nitakuwa nimekosa maadili,” alisema AY. “Mavazi ya kwenye swimming pool yako kila mahali, hata kwenye taarifa za habari (Michezo) wanaonyesha waogeleaji, kama hiyo pia ni kukiuka maadili ni sawa. Inashangaza mamlaka zetu wanafocus kwenye kufungia nyimbo zetu na kuacha video za nje. Sijawahi sikia muziki wa Kenya, Uganda au Marekani umefungiwa, kama wanaona nyimbo za Nicki Minaj zina maadili halafu Zigo ya AY haina maadili baasi unaacha tu iwe hivyo ,” aliongeza AY. Pia AY alise

Diamond kakutana na Kanye West Marekani

Image
Yoyote ambae anaufuatilia muziki wa Kanye West akikutana nae hawezi kuacha kupiga nae picha. Diamond alisafiri kuelekea Marekani Las Vegas kwa ajili ya kufanya  show, ambapo kwenye maelezo ya hii picha, ilionekana wakati huo alikuwa Los Angeles . Kwa ninavyo fahamu Diamond anakuwa mtanzania mwingine, aliyepiga picha na Kanye West , ambapo Vanessa Mdee amewahi kukutana na Kanye West na kuongea nae. Hapa ni Vanessa Mdee kulia alipokutana na Kanye West

Fahamu vyakula vya kuondoa gesi tumboni

Image
WATU wengi wamekuwa wakihangaika sana na matumbo yao kujaa gesi na pengine kuvimba. Leo nakuletea baadhi ya vyakula vya kula ili kuondoa hili tatizo. Kwa njia moja au nyingine, unajikuta tumbo limechafuka kwa kujaa gesi, kuuma na hata kuunguruma, unahisi unahitaji kunywa dawa ili litulie. Katika makala ya leo utajifunza njia bora ya kutuliza mchafuko wa tumbo kwa kutumia vyakula badala ya dawa za kisasa ambazo hutuliza dalili na haziondoi tatizo. CHANZO Kabla ya kukimbilia kwenye tiba, ni vizuri kwanza kujua chanzo cha tatizo na katika hili unahitaji kujua ni vyakula gani ukila vinasababisha matatizo ya tumbo. Aina ya vyakula inaweza kutofautiana kati ya mtu na mtu lakini kuna aina ya vyakula vinajulikana zaidi kusababisha matatizo ya tumbo. Vyakula na vinywaji vinavyochangia tumbo kujaa na ukosefu wa choo kwa muda mrefu huwa ni soda, ulevi (hasa bia), vyakula vyenye mafuta mengi na vyenye chumvi nyingi. Vyakula hivyo vinapoingia tumboni, huwa na tabia ya kuchelewe

Benki Kuu ya Tanzania yawaka moto!

Image
Jengo la Benki Kuu ya Tanzania (BoT). Najuwa wajuwa, Lakini mimi nakujuza zaidi ASUBUHI ya Julai 5, 1984, wakazi wa Dar es Salaam waliamka kwa mshangao baada ya kusikia na kuliona jengo la Benki Kuu ya Tanzania (BoT) likiwa linaungua kwa moto uliokuwa umesambaza moshi mkubwa na mzito juu ya anga la mji  huo ulio ufukweni mwa Bahari ya Hindi. Tukio hilo lilitokea kiasi cha miaka 32 iliyopita, wakati wa utawala wa Mwalimu Julius Nyerere ambapo, kama kawaida, Watanzania waliokuwa na kazi na ambao hawakuwa na kazi,  walifurika maeneo jirani ya jengo hilo ambalo ndilo ‘mama wa fedha’ za nchi hii na kushuhudia likiwaka moto huku magari kibao ya zimamoto na wafanyakazi wake wakihangaika kuudhibiti. Kama kawaida pia, majeshi ya usalama yalikuwa yamefurika eneo hilo ili kuhakikisha hapatokei purukushani yoyote wakati wa kupambana na janga hilo. Kwa ufahamisho tu ni kwamba jengo lililoungua ni lile  ‘orijino’, yaani jengo la mwanzo kabisa la benki hiyo lililofunguliwa J

SERIKALI YAMKABIDHI CHEKA CHETI CHA PONGEZI KUTOKANA NA USHINDI WAKE.

Image
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye(kulia) akiwa ameambatana na Bondia Francis Cheka (wapili kulia) alipotembelea Wizarani leo jijini Dar es Salaam na Serikali imemkabidhi  Cheti cha pongezi. Kushoto ni Rais wa Chama cha ngumi Tanzania (TPBO) Yassin Adballah (Ustadh). Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye(katikati) akizungumza na waandishi wa Habari wakati wa zoezi la kumkabidhi Cheti cha pongezi kutokana na ushindi Bondia Francis Cheka (kushoto) leo jijini Dar es Salaam.Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo Makoye Alex Nkenyenge. Bondia Francis Cheka akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani)  wakati wa zoezi la kupokea Cheti cha pongezi kutoka kwa Serikali leo jijini Dar es Salaam. Kutoka kulia ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye,Rais wa Chama cha ngumi Tanzania (TPBO) Yassin Adballah (Ustadh) na Meneja wa Bondia huyo Chifu Ndambi

Walimu 8 Mbaroni Mwanza kwa Kujihusisha na Mapenzi na Wanafunzi

Image
Walimu hao wakipandishwa kwenye gari la polisi ili kupelekwa kituoni. WALIMU wanane wa Shule ya Sekondari Mihama, Kata ya Kitangili, Wilaya ya Ilemela Mkoani Mwanza, wamesimamishwa kazi, watano kati yao wakishikiliwa na polisi kwa tuhuma za kufanya mapenzi na wanafunzi. Pia, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Magesa Mulongo aliyetembelea shule hiyo jana, amevunja bodi ya shule hiyo baada ya kubainika kutofanya kikao hata kimoja tangu ilipoteuliwa Aprili 24, 2013. Wakitiwa pingu. Pamoja na Mkuu wa Shule, Joseph Malifedha, walimu wengine waliotiwa mbaroni jana ni Rodrick Uroki, Denis Sanga, Edmund Boaz, Steven Samuel. Walimu watatu waliokuwa wakifundisha shuleni hapo, lakini wakahamishwa na hivi sasa wanasakwa na polisi kwa tuhuma hizo ni Joseph Lamongi na Joeza Mzava waliohamia Sekondari ya Sangabuye pamoja na Abdallah Mtelwe aliyehamia Tanga. Malifedha anadaiwa kuwachangisha fedha wanafunzi wa kidato cha kwanza na cha tatu kwa ajili ya picha za kuweka kwenye vitambuli

Jide ndoa tena

Image
  Mkongwe wa muziki wa Bongo Fleva, Judith Wambura ‘Lady Jaydee’ au Jide. Na Mwandishi Wetu,  Risasi Jumamosi Dar es Salaam: Siku chache baada ya kupewa talaka na aliyekuwa mumewe, mtangazaji Gardner G. Habash ‘Captain’, mkongwe wa muziki wa Bongo Fleva anayekuja na ujio mpya alioubatiza jina la Naamka Tena, Judith Wambura ‘Lady Jaydee’ au Jide amedaiwa kupata mwanaume mwingine ambaye yupo kwenye mikakati kabambe ya kumuoa, Risasi Jumamosi lina ubuyu kamili. Jide ambaye amekuwa kimya kimuziki kwa zaidi ya miaka miwili, Februari mwaka huu alipewa talaka katika Mahakama ya Manzese-Sinza jijini Dar baada ya mvutano uliodumu kwa muda mrefu tangu wawili hao washindwe kuishi pamoja. Kwa mujibu wa chanzo makini, Jide alimpata mwenza muda mrefu tangu walipomwagana na Gardner lakini mipango ya ndoa ikashindwa kwenda haraka kwa sababu hakuwa amepewa talaka hiyo aliyoidai mahakamani. “Mbona Jide kitambo tu alishapata mtu sema alikuwa hawezi kufanya mambo ya ndoa kwani

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AFANYA ZIARA ITILIMA MKOANI SIMIYU

Image
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akikagua ujenzi wa Maabara katika shule ya Sekondari ya Budalabugija wilayani Itilima akiwa katika ziara ya mkoa wa Simiyu Machi 4, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)   Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akifungua Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Itilima mkoani Simiyu Machi 4, 2016. (P:icha na Ofisi ya Waziri Mkuu) Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua bwawa la umwagiliaji na maji ya kunywa la kijiji cha Mkoma na Mwalushu wilayani Itilima akiwa katika ziara ya mkoa wa Simiyu, Machi 4, 2016. (Picha na ofisi ya  Waziri Mkuu) Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwsalimia wananchi  baada ya kukagua bwawa la maji ya kunywa na umwagiliaji la vijiji vya Mkomana Mwalushu wilayani Itilima Machi 4, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwsalimia wananchi  baada ya kukagua bwawa la maji ya kunywa na umwagiliaji la vijiji vya Mkomana Mwalushu wilayani Itilima Machi 4, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri M

Waziri wa zamani Rwegasira afariki dunia

Image
Waziri zamani wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Joseph Rwegasira. Taarifa iliyotolewa jana na Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa ilisema Balozi Rwegasira alifariki jana katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Taarifa hiyo ilieleza mwili wa marehemu Rwegasira utaagwa leo katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Peter, Oysterbay saa 8.00 mchana kabla ya kusafirishwa keshokutwa kwenda Bukoba, Kagera kwa mazishi. Rwegasira aliyezaliwa Machi 21, 1935, aliwahi kuwa mwenyekiti wa jumuiya ya vyama vya wafanyakazi (Juwata), Mkuu wa Mkoa wa kwanza wa Pwani na baadaye Balozi wa Tanzania nchini Zambia. Pia, aliwahi kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara na baadaye Waziri wa Kazi kabla ya kuhitimisha kwa uwaziri wa mambo ya nje kati ya mwaka 1993 hadi 1995 chini ya Rais mstaafu, Ali Hassan Mwinyi.

HATARI SANA! Hili Ndio Dau la Kupata Huduma ya Mrembo Huyu Mwenye Shepu Ya Maana!

Image
Gift Stanford ‘Gigy Money’. M UUZA nyago kwenye video mbalimbali za Kibongo, Gift Stanford ‘Gigy Money’ kwa mara ya kwanza amefungukia ishu yake ya malipo kupitia video za Bongo Fleva anazofanya kama ‘Video Queen’ kuwa kwa sasa bila shilingi milioni moja humpati. Akichonga na   Showbiz   Gigy alisema kuwa, kwa sasa Muziki wa Bongo Fleva umebadilika na hata video zake zina viwango vikubwa tofauti na kipindi cha nyuma ambapo hata makampuni ya video yalikuwa machache hivyo kwa wale mastaa yupo tayari kuwafanyia kuanzia laki tano lakini kwa wale ambao hawana majina sana ‘chipukizi’ bila milioni moja hawampati. “Kwa kawaida video nyingi huwa naanzia laki tano lakini kuna video ambazo kiukweli kabisa bila milioni moja siwezi kufanya,” alisema Gigy. Gigy ametokelezea kwenye video kibao za Bongo Fleva ambazo ni Siachani Nawe ya Barakah Da Prince, Get High ya Godzilla, Shika Adabu Yako ya Nay wa Mitego na nyingine nyingi.

MKUU WA MAJESHI AONGOZA KUWAAGA MAOFISA MAJENERALI 16 WA JWTZ WALIOSTAAFU

Image
Mnadhimu Mkuu mstaafu wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Luteni Jenerali Samuel Ndomba (kwenye gari kushoto) na Mkuu wa Vikosi vya Kulinda Amani Umoja wa Mataifa, Luteni Jenerali mstaafu, Paul Ignas Meela wakitoa heshima katika hafla ya kuagwa iliyofanyika Viwanja vya Twalipo Mgulani Dar es Salaam leo mchana. Maofisa Majenerali 16 waliostaafu Utumishi Jeshini waliagwa. Mkuu wa Majeshi, Jenerali, Davis Mwamunyange (kushoto), akisalimiana na Mnadhimu Mkuu wa Jeshi hilo mstaafu, Luteni Jenerali, Samuel Ndomba. Mkuu wa Majeshi, Jenerali, Davis Mwamunyange (kushoto), akisalimiana na kumpongeza Mkuu wa Vikosi vya Kulinda Amani Umoja wa Mataifa, Luteni Jenerali mstaafu, Paul Ignas Meela katika hafla hiyo. Brigedia Jenerali mstaafu, Msangi (kulia mbele), akikagua gwaride maalumu waliloandaliwa maofisa hao wastafu wakati wakiagwa rasmi baada ya kumaliza utumishi wao jeshini. Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), mstaafu Meja Jenerali, Raphael Muhuga, a