Posts

Showing posts from April 16, 2015

HAWAENDANI LAKINI NDO HIVYO TENA,SOMA HAPA

Image
  Aunt Ezekiel na Moze Iyobo. NImtazamo wa wengi kuwa baadhi ya mastaa ambao wapo kwenye uhusiano hawaendani kabisa kutokana na muonekano wao, tabia zao na hata fani zao kuwa tofauti. Kuna mastaa wa Bongo na wa Mamtoni ambao mapenzi yao yalivyoanza yaliwashtua watu mbalimbali na wengine kudai hayafiki mbali huku wale wanaotazamiwa kuendana kwa kila kitu wakimwagana vibaya mfano, Diamond Platnumz na Wema Sepetu, Rihanna na Chris Brown na wengineo wengi. AUNT EZEKIEL NA MOSE IYOBO Aunt Ezekiel ambaye ni staa wa Bongo Muvi alidai ‘kudate’ na dansa wa Diamond Platnumz, Mose Iyobo, hiyo ilijulikana mwishoni mwa mwaka jana baada ya Aunt Ezekiel kudai kuwa mimba hiyo ni ya dansa huyo. Uhusiano huo uliwashtua mashabiki wengi wa staa huyo ambapo mpaka sasa hawakubaliani na uhusiano huo wakidai kuwa kuna mtu nyuma ya Mose ambaye ndiye muhusika wa mimba ya Aunt kwa kigezo kuwa Mose hana jeuri ya pesa ya kuweza kumuweka Aunt mjini. .NAY WA MITEGO NA SHAMSA FORD Huu ni moja tu ya mfano wa map

SAKATA LA MTOTO WA NAY:MAJIBU DNA YATOKA!!,SOMA NDANI KUHUSU HATIMA YA NAY WA MITEGO

Image
  Baada ya utata mzito kutawala kwenye vyombo vya habari juu ya uhalali wa mtoto wa Mbongo Fleva, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ kwa mzazi mwenzake Siwema Edson, hatimaye kipimo cha vinasaba (DNA) kimetoka na kumaliza ubishi kwamba mtoto huyo aitwaye Curtis ni damu halisi ya msanii huyo. Hivi karibuni, Nay na Siwema ambao walikuwa wapenzi kisha kumwagana, waligombana na kila mmoja kuzungumza lake juu ya mtoto wao huyo ambapo Siwema alidai si damu ya Nay wakati msanii huyo alisema ni damu yake. Licha ya kupokea majibu hayo mazuri kwake, Nay aliyachukua majibu hayo kwa kuangua kilio cha furaha huku akieleza ya moyoni kuhusiana na sakata hilo. “Hili ni swala ambalo lilikuwa linaniumiza kichwa kila kukicha. Unajua kama mwanaume, mtu akwambie mtoto si wako unadhani ni maumivu kiasi gani utayapata? Inauma sana, mtu umelea kuanzia mimba hadi mtoto amezaliwa, si kitu kidogo. “Namshukuru Mungu kwa majibu kwamba ni damu yangu. Mashabiki wangu watambue tu kwamba, Curtis ni mwanangu asilim

WATU 10 WAKAMATWA MSIKITINI MOROGORO WAKIJIANDAA NA SHAMBULIZI LA UGAIDI

Image
Watu 10 wanashikiliwa na polisi mkoani Morogoro baada ya kukamatwa msikitini wakiwa na milipuko 30, sare za jeshi na bendera nyeusi inayodaiwa kutumiwa na kundi la wapiganaji wa Al Shabaab wa nchini Somalia. Katika tukio hilo, mmoja anayesadikiwa kuhusiana na watu hao waliokamatwa aliuawa na wananchi wenye hasira baada ya kumjeruhi kwa panga askari polisi aliyekuwa akipambana naye. Akizungumza na waandishi wa habari leo, Kamanda wa polisi mkoani Morogoro, Leonald Paul alisema tukio hilo limetokea jana (Aprili 14 mwaka huu) majira ya saa 3.30 usiku katika kitongoji cha Nyandero, tarafa ya Kidatu wilayani Kilombero. Kamanda Paul alimtaja mtu aliyefariki kuwa ni Hamad Makwendo ambaye umri wake haujafahamika ambaye ni mkazi Manyasini Ruaha wilayani Kilombero. Aidha alisema siku ya tukio polisi walipata taarifa kutoka kwa raia wema kuhusu watu hao na kwamba walitaarifiwa kuwa wanajihusisha na matukio mbalimbali ya uhalifu na polisi waliamua kufatilia nyendo zao. Akisimulia

SHUHUDIA ANACHOKIFANYA ZITTO HAPA

Image

MASHINE ZA BVR AWAMU YA PILI KUPELEKWA MIKOA SABA

Image
 Tume ya Taifa ya Uchaguzi Nchini Tanzania itaanza kusambaza mashine za BVR 248 katika mikoa saba nchni Tanzania Kuanzia katikati mwa wiki ijayo. Mikoa iliyopangwa kuanza kupokea mashine hizi ni mikoa ya Lindi, Mtwara, Ruvuma, Iringa, Wakati zozi likianza mikoa hiyo nyingine zitakuwa zinapelekwa katika mikoa ya Katavi, Mbeya na Dodoma. Mikoa mimgine ni Singida Tabora Geita na Kigoma. Mkuu wa kitengo cha Ufundi wa idara ya Daftrari/ICT wa NEC Dr Sisit Cariah, Akizungumza na mwandishi wetu amesema kwamba mpaka sasa wanachi wa mikoa ya Lindi, Mtwara, Ruvumna na Iringa wakae tayari kwani muda wowote watatangaziwa vituo vya kujiandikisha.  Pamoja na mshine hizo 248 Tume ya taifa ya uchaguzi imewaandaa wataalamu 248 ambao watakuwa na jukumu la kutoa elimu kwa wataalamu wengine 50 kwa kila mmoja nchi nzima kwa ajili ya kuharakisha uandikishaji kwa mfumo wa BVR. Dr Sisit Ameeleza kwamba wamefanikiwa kufanya maboresho makubwa katika mashine hizi ikiwa ni pamoja na kubadi

WATU 9 WAKAMATWA MORO WAKIWA NA MILIPUKO MIKUBWA PAMOJA NA SILAHA NZITO KATIKA MSIKITI

Image