Posts

Showing posts from March 8, 2016

KIVUKO CHA MV DAR ES SALAAM KUANZA KAZI HIVI KARIBUNI

Image
Rais Dk. John Pombe  Magufuli akikagua kivuko cha MV Dar es salaam.  Na Raymond Mushumbusi MAELEZO Kivuko cha Mv Dar es Salaam maarufu kama kivuko cha Rais Magufuli kipo katika matengenezo ya kawaida na kinatarajiwa kuanza kutoa huduma kama kawaida siku za hivi karibuni. Akitoa ufafanuzi juu ya madai ya kutelekezwa kwa kivuko cha Mv Dar es Salaam katika maegesho yaliyopo kigamboni Jijini Dar es Salaam ,Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Manase Le-Kujan amesema sio kweli kwamba kivuko hicho cha Mv Dar es Salaam kimetelekezwa bali kimepumzishwa kutokana na matengenezo yaliyohitajika kufanywa katika kivuko hicho ili kuongeza ufanisi katika kutoa huduma kwa wasafiri. “Sio kweli kwamba Kivuko cha Mv Dar es Salaam kimetelekezwa katika maegesho ya Kigamboni bali kimepumzishwa kwa muda kwa ajili ya matengenezo yake ya kawaida, hii ikiwa ni juhud i ya kukiwezesha Kivuko hiki kuwa katika ubora unaotakiwa katika kutoa hudumazake” “

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AKUTANA NA WAWEKEZAJI KUTOKA KOREA NA INDIA LEO

Image
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Profesa Choi Oe Chool Rais wa GLOBAL SAEMAUL DEVOLOPMENT NETWORK ya Jamhuri ya Korea, Wakati Rais huyo na Ujumbe wake alipofika Ofisini kwa Makamu wa Rais Ikulu Dar es Salaam Leo March 08,2016, kwenye mazungumzo yao Viongozi hao wamezungumzia juu ya kukuza na kuendeleza ushirikiano wa kimaendeleo katika Nyanja mbalimbali ikiwemo Uchumi. Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Profesa Choi Oe Chool Rais wa GLOBAL SAEMAUL DEVOLOPMENT NETWORK ya Jamhuri ya Korea, Wakati Rais huyo na Ujumbe wake alipofika Ofisini kwa Makamu wa Rais Ikulu Dar es Salaam Leo March 08,2016, kwenye mazungumzo yao Viongozi hao wamezungumzia juu ya kukuza na kuendeleza ushirikiano wa kimaendeleo katika Nyanja mbalimbali ikiwemo Uchumi. Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan katikati akiwa katika picha ya p

TANZANIA NA JAPAN KUANZISHA USHIRIKIANO KATIKA MATUMIZI YA TEHAMA.

Image
Mwakilishi Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Japan (JICA) nchini Tanzania Bw. Toshio Nagase akimweleza jambo Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Faustin Kamuzora (kushoto). Mwakilishi Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Japan (JICA) nchini Tanzania Bw. Toshio Nagase (kulia) akizungumza na baadhi ya watendaji wa Wizara hiyo upande wa Mawasiliano wakiongozwa na Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Faustin Kamuzora.   Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Faustin Kamuzora (kushoto) akisisitiza jambo alipokutana na  Mwakilishi Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Japan (JICA) nchini Tanzania Bw. Toshio Nagase. Bw. Toshio Nagase amekutana na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo kuhusu namna Japan na Tanzania zinavyoweza kushirikiana katika masula ya TEHAMA. Picha na Aron Msigwa –MAELEZO Na. Aron Msigwa –MAELEZO TANZANIA na Japan zinataraj

Mgombea Urais wa Marekani Donald Trump Amshukia Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta.Amwita Tapeli wa Matapeli....

Image
Just a month after endorsing former Kenyan Prime Minister Raila Odinga for President, Donald Trump has this time expressed his hate for Uhuru regime, terming it ‘A fellowship of con-men’ of con-men. Speaking to an ABC News pressman after his meeting with black pastors, the GOP said that Uhuru Kenyatta, Kenyan President has failed to lead by example. “You see I have been right all along. Uhuru Kenyatta is a dangerous conman that cannot be entrusted with the leadership of a country let alone the chairmanship of even a funeral committee. How can this man carry 23 of his relatives to Paris at the detriment of poor Kenyans? How can he take with him his daughter to a forum she has idea about? What does Guinea as – he struggled to mention Ngina – know about climate change? Can she even define the term climate? This man is simply a tourist who loves to holiday around the world. Since he went to the “white House”, he has made more trips to foreign countries compared to

WAZIRI LUKUVI HASITISHA HATI YA UMILIKI WA ARDHI HEKARI 3903 ZA MWEKEZAJI WILAYANI MBULU....

Image
  Waziri akikagua mchoro wenye eneo la mgogoro. Waziri wa Ardhi nyumba na makzi Mh. William Lukuvi jana tarehe07/03/2005  alikuwa na ziara ya kikazi Wilayani Mbulu Mkoani Manyara ambapo alienda kutatua migogoro ya ardhi inayolalamikiwa wananchi na baraza la Madiwani baina ya muwekezaji.  katika Ziara hiyo Waziri lukuvi amefuta hati za ardhi eneo la nyumba zilizouzwa na serikali kwa wananchi kutokana na ugawaji mbaya wa viwanja kwa kutozingatia sheria za ugawaji na kuwaomba idara ya ardhi kufuata taratibu za kuagwa viwanja kama walivyouzwa na kila mwenye haki ya kumiliki ardhi katika eneo hilo linagawiwa kulingana na mahitaji ya wananchi  kwani eneo hilo lina jumla ya viwanja 119 na linamilikiwa na watu wachache.  Waziri  wa Ardhi akisikiliza majibu toka kwa mtaalam wa TBA toka Makao Makuu. Aidha katika Ziara hiyo Waziri wa Ardhi nyumba na makazi amesitisha hati ya umiliki wa ardhi ekari 3,903 mali za muwekezaji wa shamba la Baragweka liliko katika kijiji cha Eshke

SEFUE AFUNGUKA KILICHOMTOA IKULU,KIJAZI ASEMA UTUMBUAJI MAJIPU UKO PALE PALE

Image
Baada ya kudumu Ikulu kwa takribani siku 127 zikiwamo 67 tangu aongezewe muda wa mwaka moja akiwa na Serikali ya Awamu ya Tano, Balozi Ombeni Sefue ameshukuru heshima aliyopewa na Rais John Magufuli kwa muda wote aliomsaidia kutekeleza majukumu yake ya ukatibu mkuu kiongozi na kueleza kuwa Serikali ya sasa ni ya mabadiliko. Wakati Sefue akiondoka, mhandisi John Kijazi amepokea kijiti cha ukuu wa utumishi serikalini na kuahidi kuwa atafuatilia mazingira ya watumishi wote pamoja na mazingira yao, ili kurekebisha panapohitajika kwa lengo la kuongeza uwajibikaji na tija kwa wananchi. Akizungumza muda mfupi baada ya kuapishwa kwa mrithi wake, licha ya kumshukuru Rais, Balozi Sefue aliwataka watendaji wote serikalini kumpa ushirikiano wa kutosha Balozi Kijazi ili kuleta ufanisi kwenye huduma za umma. “Namshukuru Rais kwa kuniamini kwa kipindi chote nilichodumu naye. Ni heshima kubwa kuwatumikia Watanzania pamoja naye. Nitampa ushirikiano wowote atakaouhitaji katibu mkuu ki

MAGAZETI YA LEO JUMANNE TAREHE 08.03.2016

Image

BREAKIN NEWZZ!!:- SERIKALI YA MAGUFULI YAZIDI KUTUMBUA MAJIPU WAFANYAKAZI 600 NIDA WAPIGWA STOP LIVE!!

Image