Posts

Showing posts from May 16, 2014

P FUNK AFUNGA NDOA YA SIRI

Image
BAADA ya kuishi maisha ya kisela kwa muda mrefu, hatimaye mtayarishaji nguli wa muziki Bongo, Paul Mathyasse ‘P Funk’ ameoa kwa siri. Mtayarishaji nguli wa muziki Bongo, Paul Mathyasse ‘P Funk’ wakati wa harusi yake. Taarifa kutoka kwa chanzo makini kilichoshuhudia tukio hilo, lilichukua nafasi jijini Arusha mwishoni mwa wiki iliyopita kwa usiri mkubwa. Imeelezwa kuwa, P Funk aliamua kumuoa rasmi mzazi mwenzake, Samira baada ya kuishi naye kwa miaka kadhaa kama mke na mume lakini haikujulikana mara moja sababu za kuweka usiri katika tukio hilo la kheri. Maharusi wakipongezwa na ndugu na jamaa zao baada ya ndoa. “Jamaa (P Funk) amevuta jiko rasmi kwa siri kubwa lakini ameamua kufanya siri hata sijui ni kwa nini, tukio limechukua nafasi huku Arusha na watu kadhaa walialikwa lakini mastaa siyo wengi. “Sherehe imefana, watu wamekula, wamekunywa kwelikweli maana misosi ilikuwepo ya kumwaga,” kilisema chanzo hicho. Chanzo hicho kilizidi kumwaga data kuwa, ka

HUU UJIO WA DVJ PENNY KATIKA MITANDAO YA KIJAMII NI SHIDA, TAZAMA PICHA ZA KIHASARA HASARA ALIZOZIACHIA MTANDAONI....!!

Image

ANGALIA PICHA MTOTO AFARIKI BAADA YA KUANGUKIWA NA JIWE KUBWA

Image
   Mtoto mmoja aliyefahamika kwa Jina la Malaika Jackson amefariki dunia Muda huu ( saa kumi jioni ) baada ya kuangukiwa na Jiwe  kubwa lililoporomoka wakati baba yake akichimba kokoto katika mlima Giza, maarufu  kama mlima wa Rada uliopo maeneo ya Kiseke, Wilaya ya Ilemela mkoani Mwanza  Kabla ya kufikwa na mauti hayo, Mtoto huyu alikuwa na baba yake mzazi aliyefahamika kwa jina la Jackson Ismail, mama yake mzazi na mdogo wake wakipata chakula cha mchana baada ya kuponda mawe kutwa nzima....   Huyu ni baba wa mtoto, bwana Jackson Ismail akimwangalia mwanae kwa uchungu.. Wangali wakipata chakula hicho, baba aliwahi kumaliza na hivyo kuendelea na kazi hiyo ya kuponda mawe huku mkewe na watoto wakimalizia kupata chakula....  Wakati bwana Ismail akiendelea kuyaporomosha mawe hayo,ghafla alisikia mtikisiko mkubwa na hivyo kumtaka mkewe na watoto watoke haraka.....  Mama akiwa na mtoto mchanga waliwahi kunyanyuka na kutoka,lakini kabla binti Malaika mwenye

ANGALIA MATESO ANAYOPATA MWENZETU,MSAADA WA HARAKAUHAHITAJIKA.

Image
Kijana Amos Ng’arare Sasi (21) mkazi wa kijiji cha Kizaru wilayani Musoma Vijijni   Kwa kipindi hiki kijana Amos, ambaye anatoka Kata ya Mryaza, amelazwa Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa ajili ya matibabu, lakini matarajio ya kupona kwa tiba za hapa nchini hayapo hivyo njia pekee iliyobaki ni kwenda nchini India kwa matibabu zaidi. Kijana Amos Ng’arare Sasi (21) mkazi wa kijiji cha Kizaru wilayani Musoma Vijijni amepoteza mwelekeo wa maisha baada ya ndoto yake ya kusoma hadi chuo kikuu kuishia njiani kutokana na matatizo ya ugomjwa wa ajabu ambao umemtesa kwa kipindi cha miaka 17. Kwa kipindi hiki kijana Amos, ambaye anatoka Kata ya Mryaza, amelazwa Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa ajili ya matibabu, lakini matarajio ya kupona kwa tiba za hapa nchini hayapo hivyo njia pekee iliyobaki ni kwenda nchini India kwa matibabu zaidi. Katika mahojiano na Mwananchi wiki iliyopita akiwa Wodi Namba 21, Sewahaji, Amos alionekana mwenye mawazo kupita kiasi. “Ndoto yang