Posts

Showing posts from December 29, 2014

LICHA YA KUSHUTUMIWA KATIKA SAKATA LA ESCROW MUHONGO AKEMEA RUSHWA TANESCO

Image
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kushoto) akizungumza na wananchi wa kijiji cha Surubu, Kata ya Komaswa wakati wa ziara yake wilayani Tarime Mkoa wa Mara. Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo amewataka wananchi wa vijiji vya wilayani hapa kutoa taarifa za mianya ya rushwa wakati wanapoomba kuunganishiwa umeme majumbani. Muhongo alisema hayo juzi alipokuwa akikagua awamu ya pili ya Mradi wa Umeme Vijijini unaoendelea kwa nchi nzima na ambao mkoani Mara unatekelezwa katika vijiji 197. Alisema katika mradi huo, Serikali haitamwonea huruma mfanyakazi yeyote wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) atakayebainika kuomba rushwa ili atoe huduma. “Msitoe hongo,” alisema Profesa Muhongo. “Kati ya vitu ambavyo Serikali haitaki kuvisikia ni rushwa. Msidanganywe kuwa mkitoa rushwa ndiyo mtarahisishiwa kupata umeme kwa haraka.” Alisema gharama zote za kuunganishiwa umeme kwa mwanakijiji zinalipwa na Serikali na kiasi cha Sh2

JESHI LA POLISI LIMELAZIMIKA KUVUNJA CHUMBA KUTOA MWILI WA MTU ALIYEKUFA SIKU NNE ZILIZOPITA.

Image
Mtu mmoja Timotheo kweka (30) mkazi wa kiwanja cha ndege manispaa ya Morogoro amekutwa chumbani kwake amefariki dunia siku nne ziizopita na jeshi la polisi limelazimika kuvunja mlango na kutoa mwili huo . Akizungumza na ITV mmiliki wa nyumba alikokuwa amepanga Leonard Benedicti amesema kwa mara ya mwisho marehemu alionekana nje siku ya jumamosi hadi leo walipohisi harufu nzito chumbani kwake ndipo walitoa tarifa kwa jeshi la polisi na kumkuta ndani amefariki na kichwa kikiwa kimebanwa kwenye stuli. Wakizungumzia tukio hilo ndugu wa marehemu wamesema hawanawasiwasi na kifo cha ndugu yao kwani alikuwa mlevi wa pombe kwa muda mrefu ambapo wamesema siku ya jumamosi walikuwa na sherehe ya ukoo lakini marehemu hakuweza kufika ingawa hawakujua kama amefariki. Jeshi la polisi mkoa wa Morogoro limedhibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo mwili wa marehemu umehifadhiwa kwenye chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya mkoa wa morogoro.

MVUA KUBWA ILIYONYESHA LEO MAENEO KADHAA YA JIJI LA DAR ES SALAAM IMESABABISHA USUMBUFU KWA WAKAZI WA JIJI LA DAR9

Image
MVUA INAYONYESHA LEO JIJINI DAR ES SALAAM IMEZUA BALAA CHENI ZINAONDOKA NA MAJI

BREAK NEWZ:MAFURIKO DAR SASA HIVI BAADA YA MVUA YA AJABU

Image

NYALANDU ATANGAZA RASMI KUWANIA URAIS 2015

Image
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazalo Nyalandu alisalimia wananachi baada ya kuwasili na mkewe Faraja Kota kwenye Mkutano wa jimbo uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Michezo wa Ilongelo, jimboni humo (Picha na Bashir Nkoromo)   Waziri wa Maliasili na Utalii, Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazalo Nyalandu alisalimia wananachi baada ya kuwasili na mkewe Faraja Kota kwenye Mkutano wa jimbo uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Michezo wa Ilongelo, jimboni humo   Waziri wa Maliasili na Utalii, Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazalo Nyalandu alisalimia wananachi baada ya kuwasili na mkewe Faraja Kota kwenye Mkutano wa jimbo uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Michezo wa Ilongelo, jimboni humo  Mwimbaji wa muziki wa Injili, Frola Nkone akiimba kutumbuiza wakati wa mkutano huo   Mwanamuziki wa muizki wa Injili, Rose Mhando akiimba kutumbuiza wananchi katika mkutano huo wa Nyalandu   Wasanii wa kikundi cha Makomandoo cha mjini Singida wakitu