Posts

Showing posts from January 26, 2016

Mbunge aangua kilio msibani

Image
Mbunge huyo akilia. Stori: Imelda Mtema, UWAZI D AR ES SALAAM: Ukimwona mtu mzima analia, ujue kuna jambo! Mbunge wa Jimbo la Tarime (CCM) kwa miaka mitano (2010-2015), Nyambari Chacha Mariba Nyangwine (40), amejikuta akimwaga machozi kwenye misa ya kuuombea mwili wa aliyekuwa mkurugenzi wa kampuni yake ya kuchapa vitabu ya Nyambari Nyangwine Publishers, marehemu Edwin Semzaba (pichani). Tukio hilo lilijiri hivi karibuni kwenye Kanisa Katoliki  Mlimani jijini Dar ambako mwili huo ulikuwa ukifanyiwa ibada na kuagwa. Wakati Semzaba akikutwa na mauti, Nyambari alikuwa kwenye safari ya kibiashara nchini Brazil ambapo baada ya kupokea taarifa hizo alikatisha shughuli zake nchini humo na kurejea Tanzania kwa mazishi.   Akizungumza na Uwazi jijini Dar juzi, Nyambari alisema alilia kwa sababu marehemu alikuwa msaada mkubwa kwake katika biashara ya vitabu. “Mimi nje ya ubunge ni mchapishaji mkubwa wa vitabu. Marehemu alikuwa mkurugenzi kwenye kampuni yangu. Sasa

TWIGA ALIBINO APATIKANA TANZANIA,AWA GUMZO ,ASHANGAZA WENGI

Image
Wataalamu wasema kuna hatari ya kuwindwa na majangilihivyo wanatakiwa kupewa ulinzi wa kutosha      Mwanasayansi Dk Derek Lee amegundua twiga albino kwenye hifadhi ya mbuga ya Tarangire iliyopo katika Mkoa wa Arusha nchini Tanzania. Mtafiti huyo Dk Derek Lee, alipiga picha mbalimbali zikiwa zinamwonyesha mnyama huyo akiwa katika kundi kubwa la twiga, huku akiwa na rangi ya kipekee ikilinganishwa na twiga wengine duniani. Dk Lee, alimgundua twiga huyo wakati akifanya utafiti kwenye mbuga hiyo na nyingine za wanyama za barani Afrika, Taarifa iliyoripotiwa na shirika la habari nchini Uingereza kupitia gazeti la Dailymail zimeeleza kuwa, twiga huyo adimu kupatikana duniani iwapo atahifadhiwa atakuwa kivutio cha pekee katika mbuga hiyo. Twiga huyo anayejulikana kitaalamu kwa jina la ‘Omo’ likimaanishwa twiga mweupe/mwenye ulemavu wa ngozi ‘albino’, alionekana akizunguka katika mbuga hiyo katik

Mume amuua mke mjamzito!

Image
Marehemu Clara Justin Munishi enzi za uhai wake. Stori: Makongoro Oging’, UWAZI D AR ES SALAAM: Dunia katili! Clara Justin Munishi (30), mkazi wa Keko Mwanga, Temeke jijini Dar amefariki dunia baada ya kudaiwa kupigwa na kujeruhiwa vibaya na mumewe, Novatus Peter Kabero. Tukio hilo la kikatili, lilitokea usiku wa saa tano, Januari 13, 2016 nyumbani kwa wanandoa hao ambapo kwa mujibu wa majirani, mwanamke huyo alisikika akilia na kuomba msaada kwa muda mrefu kutokana na kushushiwa kipigo kikali na mumewe. Mume wa marehemu   Novatus Peter Kabero. “Unajua hawa ilikuwa kama kawaida yao kugombana, mara kwa mara mwanaume alikuwa akimpiga sana mkewe hasa nyakati za usiku. Sasa siku hiyo hata tuliposikia Analia na kuomba msaada, tulijua ni kama kawaida yao, kumbe mwenzetu alikuwa anauawa,” alisema mwanamke mmoja anayeishi jirani na eneo la tukio, aliyekataa kujitambulisha jina lake. Habari zaidi kutoka kwa vyanzo vyetu, zinaeleza kuwa baada ya kuzidiwa na kipigo, mwa

Simbachawene Amsimamisha Kazi Mkurugenzi Manispaa ya Dodoma

Image
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mh. George Simbachawene. Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mh. George Simbachawene amemvua madaraka Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa ya Dodoma, Bw. Augustino Kalinga kufuatia kuruhusu ofisi yake kuwachangisha wazazi michango ambayo serikali imezuia katika kutoa elimu ya msingi bila malipo. Mh. Simbachawene alifikia uamuzi huo jana mjini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu hatua zilizochukuliwa na serikali baada ya kugundua kuwa manispaa ya Dodoma imesambaza barua kwa walimu wakuu wa shule za msingi ambazo zimeagiza kuwatoza wazazi michango ya maji, umeme na mlinzi ambayo imekatazwa na serikali. Amesema kuwa Bw. Kalinga amevuliwa madaraka yake baada ya kubainika kuwa ameshindwa kuwasimamia watumishi walio chini yake hadi kusababisha kuandika barua na kusambaza kwa walimu wakuu wa shule za msingi katika manispaa ya Dodoma amb

NYUMBA YA MCHUNGAJI RWAKATARE YASABABISHA WAZIRI JANUARY KUCHUKUA HATUA HIZI KALI KWA MAOFISA HAWA

Image
SAKATA la maofisa watatu wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), waliosimamishwa kazi kwa tuhuma ya kukiuka miiko yao ya kazi, limechukua sura mpya, baada ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, January Makamba, kuagiza wafikishwe mbele ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru). Pamoja na hayo, Waziri huyo amemsimamisha kazi aliyekuwa mwanasheria wa baraza hilo, John Mnyele kwa matumizi mabaya ya ofisi. Akizungumza  jana, alisema tayari amemwagiza Katibu Mkuu wa wizara hiyo, kuwasilisha mashtaka yanayowakabili maofisa hao watatu Takukuru kwa ajili ya uchunguzi na hatua zaidi, ikiwemo kufikishwa mahakamani. Maofisa waliosimamishwa kazi kutokana na udhaifu huo ni pamoja na Ofisa Mazingira Mwandamizi Dk Eladius Makene, Mwanasheria Daraja la II Wakili Heche Suguta Manchare ; na Ofisa Mazingira Boniface Benedict Kyaruzi. Wanatuhumiwa kukiuka miiko ya kazi yao katika kusimamia kiwand

Wema Sepetu na Idriss Sultan Wavujisha Picha Wakiwa Kitandani Kama zile za Watuache Tulale..Mashabiki Walalamika

Image
Picha za Wema Sepetu na Idriss Wakiwa kitandani asubuhi ya leo zimesambaa katika mitandao ikiwa ni siku moja tu baada ya Idriss kuweka wazi uhusiano wao wa kimapenzi na kuwa wanakaribia kupata mtoto... Mashabiki wa couple hiyo inayoongelewa zaidi kwa sasa wametoa maoni yako katika picha hizo, hapa nimekuwekea baadhi ya maoni;  tamia_ismail @zara_elia u u gat the point,l lov ths lady ila apo tu ndo anaponiudhi ...she like to expose evrythin i wsh she cn lern to keep othr things fr herself wala asingekua midomon mwa watu..anyway evry one has got a weaknes sy_salum_y_madai  Wewe idrus chaliloo ukija machimboni R chugga lazima tukuwekechini...maan kweli... Ustaa wa gafla unakuzingua maan wakati tumetoka mbali Manzi yako umemwacha bonge lakisu unaenda Pambana na makonkodi maan... Dah unazingua maan  team.watafutaji  Kila mwanaume anamtimia wema kwa manufaa yake na kujipatia umaarufu pcolour543  Tushazoea huyo dada na hzo picha.. Sio ajabu  zara_elia Ila

Mrembo wa UDSM aliyedaiwa kuwa Msukule uliokutwa shimoni anena kwa uchungu

Image
Picha zinazomuonesha mwanamke aliyekutwa kwenye shimo la mfanyabiashara mmoja jijini Dar es Salaam akiwa katika hali ya kutisha zimetumiwa kufanya upotoshaji kwa kumzushia msichana mmoja wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Picha iliyounganishwa ikionesha taswira ya msichana huyo wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wakidai kuwa hapo ni kabla zilisambazwa kwenye mitandao ya kijamii na watu wasio na nia njema na kusababisha usumbufu kwa mrembo huyo. Msichana huyo ambaye anatumia jina la Ms.Adelaide kwenye Instagram amekanusha vikali taarifa hizo huku akieleza kwa uchungu jinsi ambavyo ameathiriwa na uzushi huo. “ NAJUA WENGI MTAKUA MMEKUTANA NA HIZI HABARI..SIJAJUA NANI ALIEANZISHA HII MADA NA SIJUI IMEANZIA KWA NANI. MIMI NI MZIMA NA SIO MSUKULE JAMANI NINA WAZAZI WOTE WAWILI WAPO HAI NA WAMEUMIZWA SANA NA HIKI KITENDO, MY FAMILY MEMBERS WAMEUMIA MNOOO KUPITA KIASI, LICHA YA HIYO MIMI BADO NI MWANAFUNZI WA CHUO KIKUU, WANAFUNZI WENZANGU WENYE MAPENZI NA MIMI WANAUMIA