KWANINI WATU HUPOTEZA HAMU YA KUJAMIIANA?


Katika utafiti uliofanyika miaka ya karibuni nchini Marekani, imebainika kwamba kati ya ndoa
6,000 zilizovunjika, asilimia 57 zimesababishwa na mwenza mmoja au wote kupenda kuchati au kutumia intaneti kupita kiasi na hivyo kusababisha msisimko
kupotea kati ya wenza wawili na hatimaye mwisho ni kupungua uwezo au hamu ya kujamiana.


Ni kundi gani la wanawake lililo

katika hatari ya kukumbwa na

tatizo hili?

1. Wanawake ambao wana historiaya kupungua hamu ya kujamiana

2.  Wale ambao wamefanyiwaupasuaji wa kuondoa mayai yao ya uzazi kutokana na sababu
mbalimbali

3. Wanawake waliofika umri wa kuacha kupata hedhi (miaka
42-58)) na kupata dalilimbalimbali kama kutokwa na jasho usiku, kukosa usingizi mzuri
na msongo wa mawazo.

Kwa wanaume, visababishi vyatatizo la kupungua hamu au
uwezo wa kujamiana ni kama
ifuatavyo;

 
1. Msongo wa mawazo kama nilivyoeleza hapo juu. Kupungua au kukosekana upendo/mapenzi
katika uhusiano/ndoa.

2.  Unywaji pombe kupindukia kama nilivyoeleza awali.

3. Utumiaji wa dawa za kulevya
 

4.  Uvutaji sigara - Hupunguzakiwango na uzito wa mbegu za
kiume.

5 Uzito wa mbegu za kiume
hupungua kwa asilimia 22-57 kwawale wanaovuta sigara. Uwezo wa
mbegu za kiume kuogelea kwenye mirija ya uzazi ya
mwanamke pia nao hupungua kwa asilimia 20 kwa wale
wanaovuta sigara ikilinganishwa na wale wanaume wasiovuta
sigara.

Utafiti mwingine umethibitisha kuwa wanaume wanaovuta sigara
wana asilimia kubwa ya kutoa mbegu ambazo hazina maumbile
mazuri au ya kawaida na hivyo
kuongeza uwezekano wa mimba kutoka au kuzaa mtoto mwenye
maumbile ambayo siyo ya kawaida.
Tafiti mbalimbali pia
zimethibitisha kuwa uvutaji sigara
huharibu mirija ya seminiferous
tubules ambayo hupatikana
kwenye korodani na ni sehemu
ambapo mbegu za kiume
hutengenezwa, hivyo uharibifu
wake hupunguza wingi na uzito
wa mbegu
Pia uvutaji sigara hupunguza vichocheo aina ya testerone,
growth hormone, na vinginevyo.Wanaume wenye kiwango kidogo
cha testerone huwa na tatizo la kupungukiwa uwezo wa
kujamiana na kiwango kidogo cha mbegu.

Uvutaji sigara hupunguza mzunguko wa damu unaopita/
kwenda kwenye moyo na kwenye uume na hivyo basi kumfanya
mwanamume kushindwa kusimika na kupata tatizo la
kupungua uwezo wa kujamiana.

Katika tafiti zilizofanyika, asilimia
97 ya wale waliogunduliwa na
tatizo hili walikuwa wavutaji
sigara na katika tafiti nyingine
asilimia 87 ya wale wenye tatizo
hili walikuwa pia wavutaji sigara.
Katika utafiti uliowahusisha
wapenzi 290 mwaka 1999,
ilionyesha kwamba wanaume
ambao walikuwa wavutaji sigara
walifanya tendo la ndoa na wake
zao mara 6 tu kwa mwezi mzima
na wale ambao hawakuwa
wavutaji sigara walifanya tendo la
ndoa mara mbili zaidi ya wale
wavutaji sigara.

Uvutaji sigara, huhusishwa pia na kuongezeka kwa chembechembe
nyeupe za damu kwenye mbegu za kiume ambazo kwa kawaida
hutolewa kukiwa na ugonjwa ndani ya mwili.

Chembechembe hizi ambazozinakuwapo kwa wingi kwenye
mbegu za kiume pasipo na
kuwapo kwa ugonjwa, hupunguzauwezo wa mbegu kuingia na
kuungana na yai kutoka kwa
mwanamke na hivyo kusababishakutotunga kwa mimba.


1.    Ugonjwa wa kisukari

2. Uzito uliopitiliza unaotokana na
kuongezeka kwa mafuta ambayo
husababisha mishipa ya damu
inayopeleka damu kwenye moyo
na uume kuwa midogo na
kupungua uwezo wa kujamiana.
Kupungua uwezo wa kujamiana au kufanya mapenzi kwa
wanaume ni ishara mojawapo ya
ugonjwa wa moyo na kiharusi. 


Matatizo ya vichocheo katika tezi la koo
 
* Kuwa na wasiwasi.

 
* Kupenda mitandao ya kijami kupita kiasi .

 
* Umri - Kuanzia miaka ya 40, kiwango cha kichocheo aina ya
prolactin huongezeka na kusababisha kuongezeka kwa
kichocheo kingine aina ya dihydro-testerone ambacho
husababisha tezi dume kuongezeka na hatimaye
kupunguza uwezo wa kusisimka kwa mwanamume.

 
* Madhara katika neva inayohusika na kusimika kwa
uume
* Kuendesha baiskeli muda mrefu(kwa kipindi kimoja)

Hii hugandamiza neva na mishipa ya
damu inayopeleka damu kwenye uume na kusababisha tatizo la
kupungua kwa nguvu za uume.

Comments

Popular posts from this blog