Posts

Showing posts from August 19, 2013

Ujumbe wa Ray C kwa wavuta bangi wote...

Image
Ray  C   ambaye aliathirika na matumizi ya dawa za kulevya na baadae kupona  ameendelea kuwa kioo cha jamii kwa ku-share experience yake baada ya kupona kwenye ishu ya dawa za kulevya. Msanii  huyo  ametoa ujumbe mpya ambao ni muhimu kila mtu kuujua kwasababu kwenye mazingira yetu kuna waathirika wengi wa dawa za kulevya. Haya ndiyo maneno ya Ray C mwenyewe ambayo yana ujumbe mzuri ndani yake: “Wote hawa tuliokaa hapa(picha hapo chini) tuliathirika na dawa za kulevya na tumepona kwa kunywa dawa moja tu inayoitwa Methadone. Inapatikana Muhimbili na Mwananyamala pekee na ni bure kabisa. "Tunamshukuru sana Mh Jakaya Mrisho Kikwete kwa kutuletea dawa hii.Ningependa kuwashauri walioathirika wa dawa za kulevya iwe wewe,ndugu  yako,rafiki,kaka,dada,mjomba,jirani au yoyote aliye karibu na wewe. "Usiogope amua tu kwamba unataka kupona na nenda kanywe hii dawa utapona kabisa.”

CHADEMA yafukuza wanachama wake 8 -Ukonga

Image
KAMATI ya Utendaji ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Jimbo la Ukonga imewafukuza uanachama wanachama wake wanane huku wawili wakipewa onyo kali kwa tuhuma za kukihujumu. Akizungumza na Tanzania Daima Jumapili ofisini kwake jijini Dar es Salaam jana, Katibu wa CHADEMA Jimbo la Ukonga, Jumaa Mwipopo, alisema kuwa kwa muda mrefu kulikuwa na tuhuma za wanachama hao kukihujumu chama hicho kwa kufanya vikao vya siri ili kuwarubuni wanachama na viongozi wa matawi kukihama. Mwipopo alisema kuwa mikakati hiyo ilikuwa ikiratibiwa na Mchungaji Zabron Shilinde na Habibu Rajabu. Alisema kuwa Mchungaji Shilinde awali alikuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Kata ya Kitunda, lakini alivuliwa uongozi Aprili 10, 2012 kutokana na tuhuma mbalimbali, ikiwamo kuchukua fedha za chama na kuzitumia bila  idhini na kuchukua kadi za chama kwenye kata na matawi bila kujulikana alikokuwa akizipeleka, tuhuma ambazo alikiri, hivyo kubaki kuwa mwanachama wa kawaida. Akimzung

Miss utalii aliyepiga picha za uchi na Manaiki apewa kichapo cha mbwa mwitu

Image
Zile picha za aibu zilizoongoza  kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii nchini pamoja na nje ya nchi hasa nchini Kenya zilizokuwa zikimuonesha mwanamuziki na msanii wa bongo muvi Manaiki Sanga akiwa na mabint mbalimbali wakiwa kwenye picha utupu sasa  zimechukuwa sura mpya baada mrembo aliyekuwa mshiriki Miss Utalii 2013 Fathiya Alfani kupigwa nusu ya kupoteza uhai wake na mchumbaake kwa madai ya kumdhalilisha.   Habari za uhakika toka kwa rafiki wa karibu na mrembo huyo ambae amevujisha picha hizi za kupigwa kwa Fathiya amedai kuwa  mrembo  wa  faceboook  yuko  taabani  baada  ya  kupewa  kichapo  cha  mbwa  mwitu... “ Jamani tumuone huruma Mrembo wa Facebook kwani hali yake   ni  mbaya  sana...Yaani  amepigwa sana nusura  atolewa nafsi na mchumbaake anaeishi nae huko Buza” Kilisema chanzo hicho... Katika tukio hilo ,  mtuhumiwa namba moja na Manaiki Sanga aliyeshiriki kwenye filamu za Tikisa  na  Love Position... Inadaiwa Manaiki kwa sasa anaishi kama di