Posts

Showing posts from June 16, 2016

Amfumania mume, achoma nyumba!

Image
  Monika akiwa amezimia. Waandishi wetu, Amani Dar es Salaam: Mapenzi uchizi! Hii ndiyo kauli pekee unayoweza kuitumia baada ya mwanamke aliyetajwa kwa jina moja la Monika, mkazi wa Tabata-Senene jijini Dar, kudaiwa kumfumania mumewe na mchepuko ndani kwake kisha kuchoma moto nyumba kabla ya kuzimia. Nyumba ilivyochomwa moto. Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo lililojaza umati, sekeseke hilo lilijiri wiki iliyopita, mishale ya saa 5:00 asubuhi nyumbani kwa wanandoa hao maeneo hayo ambapo mwanamke huyo hakuwepo nyumbani hivyo aliporudi ndipo akaanzisha timbwili, akidai kumkuta mumewe ndani na mchepuko. “Unaambiwa baada ya Monika kurudi nyumbani na kumfuma mumewe ‘akimalizana’ na mchepuko, palikuwa hapatoshi. “Monika aliangusha timbwili la aina yake lakini yule mchepuko alifanikiwa kutoka nduki. “Kutokana na hasira, Monika alijifungia ndani, akamwagia nyumba mafuta ya taa, akawasha moto akitaka kujitoa uhai. “Tunashukuru Mungu, askari wa zima moto walifika na kufan

Huzuni…Familia ya Hoyce yanusa kifo ajalini

Image
Mama mzazi wa Hoyce Temu IMELDA MTEMA, Amani Dar es Salaam: Familia ya Miss Tanzania 1999, Hoyce Temu akiwemo mama yake mzazi, dada zake watatu na mdogo wake, wamenusurika kupoteza maisha baada ya gari walilokuwa wakisafiria, kupata ajali mbaya kwenye makutano ya Barabara za Ali Hassan Mwinyi na ile ielekeayo kwenye Ufukwe wa Coco, Amani linakujuza. Ajali ilivyotokea Akizungumza kwa masikitiko, Hoyce alisema ajali hiyo ilitokea mchana wa Jumapili iliyopita wakati wanafamilia hao wakielekea Ufukwe wa Coco kwa ajili ya kupata chakula cha mchana ambapo ghafla, gari jingine aina ya Range Rover Vogue, lililigonga gari walilokuwemo ndugu zake na kuwasababishia madhara makubwa. Hoyce aliongeza kuwa alipata taarifa za kupata ajali ndugu zake hao wakati akiwa Bagamoyo, Pwani kwenye kambi ya watoto wenye ulemavu wa ngozi. Miss Tanzania 1999, Hoyce Temu Mrembo huyo alisema kuwa alipigiwa simu na dada yake mkubwa aitwaye Edith aliyekuwa kwenye ajali hiyo na kumtaarifu kwamba wamep

Manji apiga hodi kwa JPM

Image
Dar es Salaam. Kama ulidhani lile sakata la ufukwe wa Coco Beach uliopo kandokando mwa Bahari ya Hindi jijini Dar es Salaam linalomhusisha Mwenyekiti wa Kampuni za Quality Group Limited (QGL), Yusuf Manji limemalizika, elewa kwamba bado. Manji amezungumza mambo mengi na gazeti la Mwananchi, lakini akasema bado anasubiria majibu yake kutoka kwa Rais John Magufuli baada ya kumwandikia barua Desemba, mwaka jana. Mfanyabiashara huyo ambaye anatarajiwa kustaafu uongozi katika kampuni hiyo mwezi ujao, amesema anatamani kuona suala hilo linamalizika haraka.

Kutoka Arusha: Mbaroni kwa kutupa mapacha

Image
Mtuhumiwa Happiness Joel JOSEPH NGILISHO, Amani ARUSHA: AMENASWA! Msako uliofanywa na wananchi wa Kitongoji cha Namayana, Kata ya Kiranyi wilayani Arumeru mkoani hapa, kufuatia tukio la mwanamke kudaiwa kutupa vichanga mapacha, umefanikiwa kumnasa mtuhumiwa Happiness Joel (29), tembea na Amani. Mwenyekiti wa kitongoji hicho, Elias Naigisa akizungumza na gazeti hili mwanzoni mwa wiki hii, alisema June 7, mwaka huu alipata taarifa ya kutupwa kwa vichanga viwili katika chemba ya choo kinachomilikiwa na mkazi wa kitongoji hicho, Elibariki Loti. Alisema baada ya taarifa hiyo, yeye na wananchi walikwenda kushuhudia na kukuta vichanga hao  wamefariki dunia na kutoa taarifa kwa jeshi la polisi huku yeye na wananchi wake wakianzisha msako mkali kumbaini mwanamke aliyekuwa na ujauzito. “Polisi walifika na kuchukua miili ya vichanga hao na kwenda kuihifadhi katika chumba cha maiti katika Hospitali ya Mkoa ya Mount Meru kusubiri uchunguzi,” alisema mwenyekiti huyo. Akipandishwa k