Posts

Showing posts from April 26, 2016

BREAKING NEWZ:JPM Avunja Bodi ya TCRA, Amsimamisha Kazi Mkurugenzi Mkuu

Image
Rais Magufuli alipofanya Mkutano na Bodi ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA). Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ameivunja Bodi ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) na kumsimamisha kazi Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo Dkt. Ally Yahaya Simba kutokana na kutosimamia ipasavyo Mkataba wa utekelezaji wa mfumo wa usimamizi wa mawasiliano ya simu (TTMS), na kusababisha nchi kupoteza mapato ya takriban shilingi bilioni 400 kwa mwaka. Rais Magufuli amechukua hatua hiyo leo tarehe 26 Aprili, 2016 Ikulu Jijini Dar es salaam baada ya kufanya kikao cha kazi kati yake na viongozi na wataalamu kutoka Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi, Wizara ya fedha na Mipango na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU). Tarehe 22 Machi, 2013 Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA) iliingia mkataba na kampuni ya SGS juu ya uwekaji, uendeshaji na uhamishaji wa mapato ya simu ambapo kampuni hiyo ilipaswa kutekeleza vipengele vitano l

Mbunge Nusura… Akamatwe na ‘unga’ Dar

Image
Kamanda wa Kitengo cha Kupambana na Kudhibiti Madawa ya Kulevya, ACP Mihayo Msikhela Na Makongoro Oging’, UWAZI Dar es Salaam: Jeshi la Polisi Kitengo cha Kupambana na Kudhibiti Madawa ya Kulevya, wiki iliyopita nusura limnase mbunge mmoja kutoka jimbo moja lililopo katika moja ya mikoa ya pwani (jina linahifadhiwa) baada ya kumuwekea mtego kutokana na madai kwamba alikuwa akisafirisha madawa ya kulevya ‘unga’ kutoka kwenye ufukwe mmoja wilayani Bagamoyo kuelekea jijini Dar. Taarifa zilizopatikana kutoka kwa vyanzo vyetu ndani ya jeshi hilo zinadai kuwa, msamaria mwema mmoja alivujisha siri kwa jeshi hilo kwamba, mbunge huyo amebeba unga kwenye gari lake dogo akielekea Dar ambapo bila kupoteza muda, polisi walimuwekea mtego kabambe kwenye njia ambazo alitarajiwa kupita ambapo hata hivyo, aliukwepa baada ya kubadilisha njia. Taarifa zaidi zinaeleza kuwa, mbunge huyo alikuwa akipita usiku wa saa mbili na mzigo huo lakini inadaiwa kuwa alishtukia kwamba amewekew

BREAKING NEWZ:Mke wa Mwai Kibaki Afariki Dunia.

Image
NAIROBI, KENYA Mke wa rais wa zamani nchini Kenya, Mwai Kibaki, Mama Lucy Kibaki amefariki dunia leo asubuhi, Jumanne, Aprili 26, 2016 akiwa kwenye matibabu mjini London Uingereza. Taarifa iliyotolewa na rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta imesema, Mama Lucy Kibaki amefariki akiwa katika hospitali ya Bupa Cromwell mjini London Uingereza alikokuwa akitibiwa. Mwezi mmoja uliopita, Mama Lucy alipewa rufaa ya kwenda Nairobi Hospital akitokea hospitali ya Gertrudeiliyopo Muthaiga, baada ya hali yake kutokuimarika wiki iliyopita alisafrishwa hadi mjini Landon kwa matibabu ambako ndiko mauti yamemkuta. Akithibitisha kifo hicho, rais wa Kenya Uhuru Kenyatta amesema kuwa kenya imesikitishwa na kifo cha mama Lucy mke wa aliyekuwa rais wa Kenya Mwai Kibaki. Katika taarifa iliotumwa katika vyombo vya habari Uhuru amesema Mama Lucy amekuwa mgonjwa kwa kipindi cha mwezi mmoja. Amesema kuwa Kenya imempoteza mwanamke aliyechangia mengi katika maendeleo ya taifa la Kenya hus

PICHA ZA MAJIVU YA MWILI WA PRINCE YAKIINGIZWA KWENYE GARI ZAONEKANA

Image
Majivu ya mwili wa mwanamuziki nyota Prince ulichukuliwa ukiwa umebebwa kwenye chombo kilichofunikwa na koti jeusi na kuingizwa kweye gari punde tu baada ya kuchomwa moto. Prince ambaye ni muumini wa dhehebu la dini ya Mashahidi wa Yehova aliacha wosia mwili wake kuchomwa na kufanyiwa maziko ya siri na ya kawaida yaliyogharimu dola 1,600.   Majivu ya Mwili wa Prince yakiingizwa kwenye gari huku dada wa marehemu  Tyka Nelson akishuhudia          Dada wa marehemu  Prince, Tyka Nelson, akiwa na majonzi mazito Posted by JAFE MALIBENEKE at Tuesday, April 26, 2016 Email This BlogThis! Share to Twitter Share to Facebook Share to Pinterest