Posts

Showing posts from April 13, 2016

Maswali 6 utajiri wa Sh.bilioni 8 wa Diamond

Image
Staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz. Hashim Aziz na Musa Mateja, RISASI mchanganyiko Dar es Salaam: Hivi karibuni, Mtandao wa The Net Worth (www.the-net-worth.com) umetangaza utajiri wa staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ (26) ambapo kwa mujibu wa jarida hilo, nyota huyo ana utajiri wa dola milioni 4 za Kimarekani (sawa na zaidi ya shilingi bilioni 8.75), jambo lililozua maswali yapatayo 6 miongoni mwa Wabongo. Mtandao huo umekuwa ukijipambanua kwa kuanika utajiri wa watu maarufu barani Afrika wakiwemo David Adedeji Adeleke ‘Davido’ (shilingi bilioni 32), Ayodeji Balogun ‘Wizkid’ (bilioni 24) na wengineo kibao. Baadhi ya wasomaji wa gazeti hili wameuliza maswali hayo wakisema mwenye uwezo wa kuyajibu ni Diamond mwenyewe na si jarida hilo huku wakitia shaka kwamba, huenda waandaaji wa jarida hilio wamepewa taarifa za uongo na Diamond mwenyewe. AMEPATA WAPI UTAJIRI HUO WA HARAKA? Swali la kwanza ambalo wengi waliosikia taarif

TCRA yawapa kibano akina lulu!

Image
Staa wa filamu Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ Gladness Mallya na Ojuku Abraham, DAR ES SALAAM: Kufuatia tabia ya akina dada wengi kuweka picha za nusu utupu katika akaunti zao kwenye mitandao ya kijamii, wakiwemo mastaa kama Lulu, Masogange na wengineo, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imewapa kibano kikali, Risasi Mchanganyiko lina stori kamili. Akizungumza na gazeti hili mwishoni mwa wiki iliyopita, Meneja Mawasiliano wa Mamlaka hiyo, Innocent Mungi alisema ingawa jukumu la kuwakamata wote wanaoweka picha zinazokiuka maadili ni la jeshi la polisi kupitia kitengo cha makosa ya mtandao (Cyber Crime), taasisi hiyo inawasiliana na wamiliki wa mitandao ya kijamii ili kutafuta namna nzuri ya kuwadhibiti. Kidoa. “Tunachofanya ni kuzungumza na hawa watu ili kuwafungia wote wanaokiuka maadili, tunajua baadhi yao wanajiunga katika mitandao kwa kutumia majina ya uongo, lakini sisi tutazifungia ‘line’ maana kila moja ina namba zake za siri na hazifanani na zingin