MUUGUZI MWENYE HIV AFUNGWA JELA UGANDA

Muuguzi Namubiru aliambia mahakama hakuwa na nia ya kumuambukiza mtoto huyo HIV
Nchini Uganda mahakama imempata na hatia muuguzi mwenye HIV, aliyeshitakiwa kwa kumdunga mtoto mchanga sindano, ambayo awali ilimchoma yeye mwenyewe.
Muunguzi huyo, Rosemary Namubiru, mwenye umri wa miaka 64, mwathiriwa wa virusi vya HIV, amefungwa miaka mitatu jela, kwa kile hakimu amekiita, 'uzembe wa weledi'.
Hukumu hio imetolewa wiki moja baada ya bunge la Uganda kupitisha muswada, unaomtia hatiani mtu yeyote ambaye kusudi anamuambukiza mtu mwengine virusi vya ukimwi.
Mtoto huyo hata hivyo hakuambukizwa virusi vya HIV na wanaharakati wamekosoa mahakama kwa kumfunga jela mwanamke huyo.

Bbake mtoto huyo hata hivyo alielezea kufurahishwa na uamuzi wa mahakama.


Baba huyo, Daniel Mushabe, amesema kuwa anatumai kesi hiyo itampa motisha Rais Museveni kuidhinisha mswada uliopitishwa na wabunge wa kuwachukulia hatua za kisheria watu wanaowaambukiza wengine HIV kusudi.

Adhabu ya kosa hilo ni faini ya dola 1,900 au miaka kumi jela.

Sheria hiyo ikiwa itapitishwa itawaadhibu wanaotenda uhalifu huo kwa maksudi.

Wananchi bila shaka walionyesha kuudhiwa na kitendo cha muuguzi huyo ingawa wanaharakati wamemtetea mama muuguzi.

Hakimu aliyetoa hukumu alisema kuwa Namubiru alikosa kuonekana kama aiyesikitishwa na kosa lake.

Namubiru, muuguzi mwenye uzoefu wa kazi wa miaka 30, alisisitiza kwamba hana hatia na kuwa mtoto huyo hakuambukizwa HIV.

Namubiru aliamua kumdunga sindano mtoto huyo kutafuta mshipa lakini kapata ugumu na hivyo kujidunga mwenye kwa bahati mbaya lakini amesisitiza kuwa hakuwa na nia yoyote ya kumuambukiza mtoto huyo virusi vya HIV.

Rais anasubiriwa kuidhinisha au kutupilia mbali mswada wa adhabu kwa wanaombukiza wengine HIV kusudi

source:bbc

Comments

Popular posts from this blog