Posts

Showing posts from August 3, 2015

Hapa na Pale: Hii ndiyo Mistari ya Nuh Mziwanda Alipokuwa Anamtongoza Wema Sepetu, Utavunja Mbavu

Image
Nuh Mziwanda amejikuta akiumbuka vibaya baada ya Wema Sepetu kuvujisha sauti anayosikika akimtongoza mrembo huyo. Mazungumzo hayo yanachekesha sana hasa kutokana na mistari anayompa Miss Tanzania huyo wa zamani. Haya ni maongezi yaliyofanyika mwezi June (siku moja kabla ya KTMA 2015). Tunafahamu wapo wasioweza kusikiliza clip yote hivyo tumekuandikia mazungumzo hayo. Nuh Mziwanda: Kuna ua moja lilikuwa limefuatwa sana na vipepeo pamoja na nyuki kwaajili ya kutengeneza asali, unanielewa? Wema Sepetu: Yeah Nuh: Kwahiyo lile ua yule mama alikuwa anapenda sana kulitunza na kulifanya special kuliko maua yote. Mama yupo radhi maua yote yakauke lakini lile ua alimwagilie maji ili likue. Wema: Hilo ua lilikuwa nyumbani kwenu? Nuh Mziwanda: Yeah nyumbani kwetu Ilala Posta, alipokulia Shetta kwa akina Shetta pale kwetu hapa. Ua hilo hadi leo hii lipo. Ua ambalo mama analipenda na kulithamini kwakuwa lililikuwa linavutia. Kwahiyo katika kuvutia kwake, vipepeo

WANAWAKE WENGI HULIA NA KUUMIA SANA PALE WANAPOSHINDWA KUSHIKA MIMBA, ZIFAHAMU SABABU ZA TATIZO HILI HAPA

Image
Miongoni mwa matatizo ambayo yanapatikana sana kwa sasa katika jamii zetu na kusababisha wanandoa wengi au wanawake wengi kukosa furaha, hili suala la kukosa uwezo wa kupata ujauzito kwa mwanamke. Lakini kimsingi tatizo hili si swala la mwanamke pekee yake kama jamii inavyolichukulia bali ni tatizo ambalo  linahusisha pande zote mbili, yaani upande wa mwanamke na pia upande wa mwanamme, wote wawili wanapokuwa katika afya nzuri ndipo ujauzito unaweza kupatikana kwa mwanamke. Miongoni mwa sababu zinazoweza kumfanya mwanamke ashindwe kupata ujauzito ni kama zifuatazo: Kuziba kwa mirija ( fallopian tubes ), mwanamke anapokuwa na hali hii huchangia mbegu za kiume (sperms) kushindwa kulifikia yai na kulirutubisha ili ujauzito utungwe. Kuziba kwa mirija huweza kusababishwa na magonjwa yanayoambukizwa kwa njia ya kujamiiana na mara nyingi wanawake ambao mirija yao imeziba, hawahisi dalili zozote. Uvimbe katika kizazi ( fibroids ),  hali hii nayo huchangia mwanamke

Obama makes first trip to Kenya as President (July 2015)

Image
Barack Obama lands in Nairobi for GES 2015 US President Barack Obama (right) talks with Kenyan President Uhuru Kenyatta as he signs a guestbook upon his arrival on Air Force One at Kenyatta International Airport in Nairobi on July 24, 2015. PHOTO | SAUL LOEB | AFP By AGGREY MUTAMBO & JOHN NGIRACHU In Summary The journey had taken him from Washington to south-western Germany at the Ramstein Air Force Base before he reconnected to Nairobi. Mr Obama was also accompanied by his National Security Advisor Susan Rice, Foreign Policy aide Ben Rhodes and White House Spokesman Josh Earnest US President Barack Obama on Friday landed in Nairobi on his first trip to Kenya as President, ending a long wait for his arrival in the land of his father. President Obama’s plane, Air Force One, touched down at 8:02pm. He emerged 18 minutes later and waved briefly at the door before meeting the small crowd that awaited him. BROAD SMILE I

BREAKING NEWSSSSS: MBOWE ATOA KAULI KUHUSU TETESI ZA DR SLAA KUJIUZULU

Image
Akizungumza na Radio one mda wa saa 4, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na maendeleo(CHADEMA) Freeman Mbowe, amesema Dr Slaa hawezi kuhama chama hicho na hafikirii kamwe, kwa sasa anapumzika kwa likizo ya wiki moja.  Alipoulizwa kuhusu Slaa kutokubaliana na ujio Wa Lowassa amejibu kila kitu tulikubaliana na Slaa mwenyewe aliunga mkono suala hilo. Mbowe amesema wananchi na wanachadema kwa ujumla wasiwe na wasiwasi kwani hiki chama ni makini na hakiwezi fanya maamuzi bila maridhiano na akasisitiza kuwapuuza wanaoeneza habari kuwa Slaa amejiuzulu siasa. Alipoulizwa mara ya mwisho kuwasiliana na Dr Slaa ni lini akajibu jana saa kumi na mbili jioni. Alipoulizwa walizungumza nini akajibu anajua yeye na Slaa. Walipomuuliza hasa mbona sisi tukimpigia hapatikani akajibu sijui lakini mimi nimewasiliana nae jana. Chanzo: Radio one

NEWS ALERT : BAADA YA KUKAA KIMYA KWA MUDA, DK SLAA AZINDUKA NA KUTOA MANENO HAYA MAZITO KWA WANA CHADEMA =

Image
Baada ya Uvumi wa Muda Mrefu Kuhusu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleoa CHADEMA Mh  Dr Slaa Kuhama chama hizo.Dr Slaa Ameamua Kukata shauri na Kutoa Tamko kwenda kwa wanachama wa CHADEMA Pamoja na watanzania na Kumaliza Kabisa Uvumi  Ulioenea sana kwenye Mitando ya Kijamii

BALOZI JUMA MWAPACHU AFUNGUKA MAZITO KUHUSU EDWAED LOWASSA

Image
Kauli ya  Juma Volter Mwapachu   Kuhusu Lowassa Nimekuwa kimya kwa muda mrefu katika mabadilishano ya fikra kwenye mtandao huu ambao kwa hakika, kwa maoni yangu, haubidi kuwa ni wa fikra pevu zisizo shawishika na misimamo ya ' kimalaya ya siasa'.  Kama tutaserereka katika msingi huu, basi ni bora Chambi ukafunga virago na kusitish huu mtandao. Nimesoma mabadilishano na mabishano ya fikra kuhusu hali ya siasa nchini mwetu na hususa ni baada ya Mhe Lowassa kuamua kujiunga na Chadema na kuwa mwakilishi wa UKAWA katika kinyang'anyiro cha nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano. Sijui nyie wenzangu  mmesimamia wapi katika suala hili. Naomba niseme mwanzoni kabisa kwamba nchi yetu hii leo imefikia mahali ambapo wasomi, wanazuoni kama sisi katika mtandao huu, Hatuna budi kujitokeza na kuhesabika tunamuunga nani mkono katika uchaguzi ujao wa Rais wa Tanzania. Tuwe wakweli na siyo kuendelea kuegemea katika kificho cha 'uhuru' wa wanazuoni katika kutoa maomi na

Pichaz Mastaa walivyoipendezesha Birthday party ya Mose Iyobo dancer wa Diamond Platnumz..

Image
Sherehe za Birthday nazo zina uzito wake siku hizi, unaambiwa dancer mkali   Mose Iyobo ambaye ni mmoja wa dancers wa   Diamond Platnumz   alifanya party yake August 02 2015, wakaalikwa mastaa wengi kutoka Bongo Movie na Bongo Fleva, kiukweli ilipendeza sana. Aunty Ezekiel   ni mzazi mwenzake na   Mose Iyobo , kwa pamoja walikutana na marafiki zao na kushereheka party hiyo… kwenye list ya mastaa waliotokea alikuwepo pia  Diamond Platnumz   na crew nzima ya WCB wakatoa na burudani ya nguvu kabisa. Hapa ni   Aunty Ezekiel ,   Mose Iyobo   na   Diamond Platnumz . Diamond Platnumz  na   Maimartha  Diamond   anapiga chabo hiyo keki inavyoliwa yani !! Martin Kadinda   na   Mose   kwenye keki. Shamsa Ford Mwigizaji   JB . Diamond Platnumz   nae akapita kwenye keki. TID   akimpongeza   Mose Iyobo . Hii ndio time ambayo kila mtu alisimama kucheza sankoro. Birthday Boy hakupishana na maji aisee !!

ZARI AWAPIGA ‘STOP’ NDUGU WA DIAMOND PLATINUMZ

Image
  Wakati akisubiriwa kujifungua muda wowote, mwandani wa staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ anadaiwa kuwazuia baadhi ya ndugu wa jamaa huyo kuingia kwenye chumba maalum kilichoandaliwa ili kuepuka kisiingie vumbi na kiwe safi wakati wote. Chanzo chetu ambacho ni mmoja wa ‘memba’ wa familia hiyo kilipenyeza kuwa, kwa sasa nyumbani kwa mwanamuziki huyo maeneo ya Madale-Tegeta, Dar, wana bashasha wakimsubiria mtoto huku chumba hicho kikiwekewa uangalizi mkubwa.  “Yaani Zari hataki mchezo kabisa na haruhusu mtu kuingia chumbani humo hovyo kwa sababu ya kuepuka vumbi kwa mtoto kwa maana chumba hicho hakihitaji msongamano wa watu wengi,” kilisema chanzo hicho.  Mpashaji huyo aliweka wazi kuwa, Zari alitia ngumu na kusema ni sheria aliyoiweka mwanamama huyo na haitakiwi kukiukwa na mtu yeyote kwa kuwa wanafahamu fika kuwa chumba cha mtoto hakihitaji msongamano wa watu hivyo ndugu hao imebidi wawe wapole. Kilidai kwam

KAULI YA MNYIKA BAADA YA LOWASSA KUPENDEKEZWA KUWANIA URAIS KUPITIA CHADEMA

Image
  Ikiwa ni siku Chache tangu lowassa ajiunge na chama cha chadema kumekuwepo uvumi kuwa MBUNGE wa Ubungo, John Mnyika, amekiama chama chake kutokana na chama hicho kumkalibisha Lowassa na kumpa nafasi ya juu kabisa Ukweli wa madai haya umethibitishwa leo hii baada ya Mnyika kuhudhulia katika mkutano wa kamati kuu (CC) ya chama cha demokrasia na maendeleo Licha ya Lissu kutoa taarifa kuwa hakuna hali ya sitofahamu ndani ya chama icho ila bado watu wamekuwa wakivumisha mambo kuwa chama icho kimevurugika baada ya wanachama kutounga ujio wa aliyekuwa waziri mkuu Edward Lowassa Taarifa kutoka ndani ya kikao cha CC kinachofanyika katika hoteli ya Bahari Beach zilizotufikia dawati la habari clansmedia zinasema, Mnyika amehudhuria mkutano huo na kueleza kuwa kutoonekana kwake, kumetokana na matatizo ya kifamilia. Mwanasheria mkuu wa Chadema, Tundu Lissu amethibitisha Mnyika kuhudhuria mkutano huo. “Mnyika yupo ndani ya ukumbi wa mkutano. Anashiriki kikao cha kamati

WASOMI:DR.SLAA HATORUDI CHADEMA!!,SOMA NDANI

Image
Wakati uvumi wa kujiuzulu cheo na kujivua uanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Wilbroad Slaa, ukiwa umetawala kupitia mitandao ya kijamii na magazeti, taarifa zinadai kuwa sababu ya kuchukua hatua hiyo ni shinikizo kutoka kwa mkewe. Taarifa zilizochapishwa na gazeti moja likimnukuu Dk. Slaa mwenyewe, zilisema ameachana na siasa na kujivua wadhifa wake na atabaki kufanya shughuli zingine. Dk. Slaa amedaiwa hakubaliani na namna chama chake kilivyompokea Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa. Lowassa aliyekuwa Mbunge wa Monduli alitangaza kuhamia Chadema, Julai 28, mwaka huu baada ya kutoridhishwa na mchakato wa CCM wa kumpata mgombea wa urais. Habari za uhakika kutoka vyanzo vyetu vya habari ndani ya Chadema zinadai, Dk. Slaa alishiriki katika mchakato mzima wa kumpokea na kuridhia Lowassa, kusimamishwa kuwa mgombea urais kupitia Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa). Hata hivyo, chanzo kingine cha habari kinadai kuwa mke wa Dk. Slaa, Jos

MGOMBEA MWENYE ELIMU YA MSINGI APITA KURA ZA MAONI!!..SOMA HAPA

Image
Jimbo la Makambako ALIYEKUWA mbunge wa Jimbo la Njombe Kaskazini, Deo Sanga Maarufu kwa jina la Jah People yupo katika nafasi ya kurudi bungeni baada ya kuibuka mshindi wa kura za maoni za jimbo jipya la Makambako. Alipokuwa akigombea mwaka 2010, Sanga atakumbukwa kwa namna alivyokuwa akiinadi elimu yake ya msingi kwa wapiga kura wake. "Mimi ni msomi wa elimu ya juu ya msingi ndio maana ni mfanyabishara mkubwa niliyeajiri wasomi wanaosikiliza maelekezo yangu," hiyo ni moja ya nukuu zake. Katika kinyang'anyiro hicho, Jah People amezoa kura 7,643 dhidi ya kura 499 alizopata mshindani wake Alimwike Sahwi. Jimbo la Njombe Kusini: Vitalis Konga 76, Hassan Mkwawa 152, Mariano Nyigu 86, Alfred Luvanda 978, Arnold Mtewele 1,136, Daniol Msemwa 1976, Romanus Mayemba 2,153 na Edward Mwalongo 3,870. Ludewa: Kapteni Jacob Mpangala 205, Zephania Chaula 770 na Deo Filikunjombe 18,290 kabla ya kata tatu za Lifumu, Kilondo na Makonde. Wanging’ombe Eston Ngilang

BASATA YAMFUNGIA SHILOLE MWAKA MMOJA KUTOJIHUSISHA NA MUZIKI

Image
Habari zilizotufikia jana usiku July 30 2015 kutoka Baraza la sanaa Tanzania (BASATA) zinasema kuwa baraza hili limemfungia Shilole kutojihusisha na kazi yoyote ya sanaa kwa muda wa mwaka mmoja.Kwa zaidi soma hii barua hapa chini

MAJINA YA WALIOSHINDA JANA KWENYE KURA ZA MAONI KWENYE MAJIMBO 28 HAYA HAPA

Image
KURA ZA MAONI CCM 1. Mwigulu - Iramba 2. Nape - Mtama 3. Mwakasaka - Tabora Mjini 4. Mama Sitta - Urambo 5. Kadutu - Ulyankulu 6. Bashe - Nzega 7. Ngeleja - Sengerema 8. Seif - Igunga ktk jimbo jipya. 9. Masaburi - Ubungo 10. Patel - Ukonga 11. Prof Kamala - Nkenge, Misenyi 12. Kagasheki -  13. Lukuvi - Isimani 14. January - Bumbuli 15. Muhongo - Musoma vijijini 16. Ndugai - Kongwa 17. Chumi - Mafinga 18. Kigola - Mufindi kusini 19. Mgimwa - Mufindi kaskazini 20. Filikunjombe - Ludewa 21. Mgimwa - Kalenga... 22. Lusinde - Mtera 23. Imani Moshi - Kaliua 24.Mwakasaka -Tabora mjini 25.Fenala Mkangara -Kibamba 26.Mapunda-Mbinga mjini 27.Masele -Kahama 28.Antony Mavunde-Dodoma hizi ndio data nilizopata TUTAENDELEA KUKUTUMIA KADILI TUWEZAVYO