Posts

Showing posts from January 7, 2018

Pretty Kind afungiwa miezi sita kwakutoa Wimbo usio na maadili

Image
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza amemfungia msanii Suzan Michael maarufu kama Pretty Kind kujihusisha na sanaa kwa muda wa miezi sita. Akizungumza leo Jumapili Januari 7 jijini Dar es Salaam, Shonza amesema amechukua hatua hiyo kutokana na msanii huyo kutoa wimbo uitwao ‘viduduwasha’ usio na maadili. Msanii huyo pia amekutwa na kosa la kufanya  kazi ya sanaa bila kusajiliwa na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata), kuweka mtandaoni picha ya nusu utupu kinyume na maadili. ‘’Kumekuwa na wimbi kubwa la wasanii kutoa nyimbo zenye maneno ya matusi na zisizo na maadili, pamoja wanawake kupiga picha wakiwa wamevaa nusu utupu na kuweka picha hizo katika mitandao,” amesema Shonza na kuongeza, “Nataka kuwapa angalizo wasanii wenye tabia hizi kuwa Serikali inawafuatilia kwa karibu na mwaka huu tumeanza na huyu na wengine wanafuata kama msanii Gift Stanford maarufu kama Gigy Money na  Jane Rimoy maarufu kama Sanchi.” Shonza amemtaka msanii

Madereva boda boda wenye hasira wateketeza Basi kwa moto

Image
Madereva wa Boda boda wenye hasira wameliteketeza Basi la abiria la Kampuni ya Simba  Coach lililokuwa linatokea jijini Nairobi kwenda Malindi nchini Kenya jana mchana. Basi hilo ambalo kabla ya tukio hilo mashuhuda wamesema kuwa lilimgonga muendesha bodaboda mmoja na kufa hapo hapo lakini halikusimama kitu ambacho kilipelekea waendesha boda boda kuanza kulikimbiza. Wakielezea tukio abiria wamesema dereva wa Basi alitaka ku-overtake gari ndogo katika eneo la Kijiwetanga na ndipo alipomgonga dereva huyo wa Boda boda. Abiria wamesema baada ya Basi hilo kusimamishwa na madereva boda boda waliamuriwa kutoka kwenye Basi hilo kabla ya kulichoma moto. Tayari Kamanda wa Polisi mjini Malindi,  Matawa Muchangi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na dereva wa gari hilo bado anatafutwa huku Dereva wa boda boda aliyegongwa mwili wake umepelekwa katika Hospitali ya Malindi. Chanzo:The Star Kenya

Tundu Lissu Awasili Ubelgiji Kwa Ajili Ya Matibabu Ya Mazoezi Ya Viungo

Image
Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Antipas Lissu akiwa na madaktari baada ya kufika Ubelgiji. Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Antipas Lissu amewasili katika uwanja wa ndege jijini Brussels, nchini Ubelgiji ambapo amepelekwa kwa ajili ya awamu ya tatu ya matibabu yake yatakayohusisha mazoezi ya viungo. Tundu Lissu amewasili jijini hapo akitokea katika Hospitali ya Nairobi, nchini Kenya alikokuwa anapatiwa matibabu kwa muda wa takribani miezi minne sasa kutokana na kushambuliwa kwa risasi mnamo septemba mwaka jana mkoani Dodoma Mbunge Tundu Lissu, ambaye pia ni Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzani Bungeni, alishambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana alipokuwa akitoka Bungeni, majira ya saa 7 mchana, karibu na nyumbani kwake Area D, mjini Dodoma. Kwa mujibu wa taarifa ya madaktari waliokuwa wanamtibu, walieleza kuwa jumla ya risasi 16 zilimpata Tundu Lissu mwilini mwake na wamefanikiwa kuzitoa 15, isipokuwa moja ambayo ipo nyuma ya uti wa mgongo. Tundu Li