Posts

Showing posts from October 7, 2016

Aveva Amuandikia Barua Rais Magufuli Ya Kuomba Radhi

Image
Rais wa timu ya Simba, Evans Aveva. UONGOZI wa Klabu ya Simba umemuandikia barua Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Pombe Magufuli, ukiomba radhi kwa kitendo cha mashabiki wao kufanya uharibifu kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar. Wakati barua hiyo ikiwasilishwa serikalini, upande wa pili Simba chini ya rais wake, Evans Aveva, imeteua kamati maalum ya wajumbe wenye uwezo mzuri wa kifedha kwa ajili ya kuiwezesha kufanya vizuri msimu huu, kamati ambayo ilianza kazi kuanzia katika mechi dhidi ya Yanga. Sehemu ya viti vilivyog’olewa na mashabiki wa Simba siku ya mechi ya Ligi Kuu Bara dhidi ya Yanga. Kabla hujaijua kamati hiyo, upande wa kuomba radhi ni kuwa hatua hiyo imefikiwa siku chache tangu serikali kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ikiwakilishwa na waziri wake, Nape Nnauye kuzisimamisha Simba na Yanga kuutumia uwanja huo baada ya uharibifu kutokea wakati wa mechi baina ya timu hizo, Jumamosi iliyopita. Rais wa Jamhuri ya Muung

ZIARA YA JAJI MKUU WA AUSTRALIA YA KUSINI NCHINI TANZANIA

Image
Jaji Mkuu wa Australia ya Kusini, Mhe.Christopher Kourakis (kushoto) akisoma kitabu kinachohusu Chama cha Majaji Wanawake Tanzania wakati alipotembelea ofisini kwa Mwenyeji wake Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Mohamed Chande Othman. Jaji Mkuu wa Australia ya Kusini, Mhe. Christopher Kourakis (kushoto), akizungumza jambo na Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Mohamed Chande Othman (kulia) katika ofisi ya Jaji Mkuu wa Tanzania, iliyopo kwenye jengo la Mahakama ya Rufani Tanzania, jijini Dar es Salaam. Mhe. Jaji Kourakis yupo nchini kwa ziara ya siku tatu yenye lengo la kujenga ushirikiano katika utendaji kazi wa Mahakama baina ya nchi hizo mbili. Kushoto ni Bi. Emma Gorman, Katibu wa Jaji Mkuu wa Australia Kusini.

Madaktari Wasema Said Ally Hatoona Tena

Image
Said Ally akiwa katika hali ya huzuni baada ya kuambiwa haotoona tena. …akifarijiwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Saalam, Paul Makonda. …Akizungumza na Mhe. Makonda. Mapema leo Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ametoa majibu kuhusu na hatma ya kijana Said Ally aliyetobolewa macho na Scorpion maeneo ya Buguruni Sheli na kusema hatoweza kuona tena. Akizungumza na waandishi wa habari mkuu huyo wa mkoa amesema: “Majibu yametoka na Said ameturuhusu tuyaweke wazi majibu ni mabaya ila tumeyapokea itabidi tukubaliane na matokeo kwamba ndugu yetu hataweza kuona tena kwa maisha yake yote. “Serikali ya mkoa imejitolea kumpatia matibabu ya macho ya bandia kwa ajili ya kutengeneza shape ya uso wake tena, kumpatia elimu ya kusoma tena kujifunza kwa alama ili aweze kuendana na mazingira. Serikali ya mkoa imetoa gari kwa ajili ya kumsaidia kipindi chote atakachokuwa kwenye matibabu yake. “Kabla ya kupatwa na ulemavu huo, Said alikuwa kinyozi hivyo kuna mdogo wake yupo atamsaidia

TANESCO YATILIANA SAINI MIKATABA YA KUJENGA NJIA YA UMEME WA KILOVOTI 400 UTAKAOUNGAMISHA MIJI YA SINGIDA, ARUSHA NA NAMANGA NCHINI KENYA

Image
 Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Tanzania, (TANESCO), Felchesmi Mramba, (kushoto), akibadilishana hati za mkabata na Mkurugenzi wa Maendeleo ya Biashara ya Kimataifa wa kampuni ya Bouygues Energies&Service, Patrick Canton baada ya kusini, mradi wa ujenzi wa njia ya umeme (transmission line) itakayounganisha Tanzania na Kenya, makao makuu ya TANESCO jijini Dar es Salaam, Oktoba 7, 2016. Shirika hilo limeingia mkataba na makampuni matatu kutekeleza mradi huo (KTPIP), wa Msongo wa KV400 unaofadhiliwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika, (AfDB) na Shirika la Misaada ya Maendeleo la Japan, (JICA), kwa gharama ya dola za Kimarekani 309.26  Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Mhandisi Felchesmi Mramba, (kushoto), na Mkurugenzi wa Maendeleo ya Biashara ya Kimataifa wa kampuni ya Bouygues Energies&Service, Patrick Canton wakisaini mkataba huo  Mhandisi Mramba, (kushoto), na  S.K. Sarotra, Makamu wa Rais msaidizi wa Kampuni ya KALPA-TARU, wakisaini mkataba