Posts

Showing posts from October 21, 2013

Makamu wa Rais Dkt. Mohammed Gharib Bilal afungua mkutano wa Mabunge ya SADC mjini Arusha

Image
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiangalia vikundi vya sanaa vya ngoma za aina mbalimbali alipowasili katika Jengo la Ukumbi wa mikutano A I C C mjini Arusha kwa ajili ya kufungua mkutano wa siku 11 wa 34 kwa Mabunge ya Nchi wanachama wa Jumuiya ya SADC leo Octoba 20, 2013. (Picha na OMR) Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Mbunge wa Arusha mjini Mhe. Godbles Lema nje ya ukumbi wa mikutano wa A I C C Arusha, Baada ya kufungua mkutano wa siku 11 wa 34 kwa Mabunge ya Nchi wanachama wa Jumuiya ya SADC katika ukumbi wa A I C C mjini Arusha leo 20 Octoba 2013. Kushoto Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nasari. Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Mbunge wa wawi kisiwani Pemba Mhe Hamad Rashid nje ya ukumbi wa mikutano wa A I C C Arusha, Baada ya kufungua mkutano wa siku 11 wa 34 kwa Mabunge ya Nchi wanac

KATI YA HAWA MASTAA WA KIKE WANAOTINGISHA BONGO NI NANI MKALI?

Image
Wema Sepetu...I just love her voice,lips, skin tone and that caring heart Lulu Michael she knows sifa zake zote ambazo nilikuwa nampa kila siku tukiwa wote... her smile huwa linaninyong'onyeza kabisa. Ana heshima, ni mwelewa na ni Jambazi wa hisia za watu.. akiamua kuiteaka tanzania kwa hisia tu anaweza  Jackie cliff.... am sure hapa sipo peke yangu bana kwa kutokwa na udenda... look at her sexy body.... kimwili kisichokomaa!! ana akili na ni mtafutaji katika maisha.. in her Young age she is married and managed to kip her life more personal Tune to 88.4Fm utajua nini kimeniteka kwa huyu mtoto....mke wangu akikosa sauti ya Wema apewe Ya Diva Lovess love... anateka vijana wengi muda wa show yake ukifika... mahusiano yamevunjika sababu ya watu kusikiliza show yake badala ya kula chakula cha usiku na wapenzi zao TUPE MAONI YAKO, NA USISAHAU KULIKE KURASA WETU WA FACEBOOK

WASTARA AUUMIZA TENA MGUU WAKE

Image
MWANADADA anayeendesha maisha yake kwa kupitia filamu za Bongo, Wastara Juma ameumia mguu baada ya kuwekewa mwingine mpya wa bandia huko Nairobi nchini Kenya. Akizungumza na paparazi wetu siku chache baada ya kurudi Bongo, Wastara alisema aliumia wakati akifanya mazoezi ya mguu mpya aliowekewa ambapo kwa sasa anaendelea kuuguza jeraha hilo na amerudi mara moja kwa ajili ya Sikukuu ya Idd, ikimalizika atarejea tena nchini humo kwa ajili ya matibabu zaidi. “Nimeshindwa kula sikukuu mbali na watoto wangu ndiyo maana nikaja mara moja japokuwa siko vizuri kwa sababu niliumia kwenye mazoezi ya kutumia mguu mpya huko Nairobi na sasa nauguza kidonda lakini baada ya hapo nitarudi tena Nairobi kwa ajili ya matibabu,” alisema Wastara.

MTOTO WA MIAKA 14 AJIFUNGUA MAPACHA HUKO MOSHI

Image
UKISTAAJABU ya musa utayaona ya firauni ndivyo ilivyotokea kwa mtoto wa miaka miwili ambaye amejifungua mtoto. Mtoto huyo aliyefahamika kama Xiao Feng alijifungua kwa njia ya upasuaji katika hospit ali moja mjini Xuaxi nchini China. Kwa mujibu wa taarifa, madaktari waligundua kuwa mtoto Xiao alikuwa na mimba baada ya kupelekwa na mama yake. Binti wa miaka 14 akiwa na mtoto wake katika Manispaa ya Moshi.Picha ya Maktba. Awali mzazi wake huyo aligundua kuwa tumbo la binti yake lilikuwa kubwa isivyo kawaida hivyo alimpekeka hospitali kujua kulikoni. Nao matabibu hao wakafanya kazi yao ya kumpiga picha za mionzi ya jua ‘x-rays’ na kubaini mtoto huyo alikuwa amebeba mwenzake tumboni. Walimfanyia upasuaji ambao ulimalizika kwa mtoto huyo kuzaa watoto pacha

Mama mwenye UKIMWI amchukua mtoto wa jirani na kumnyonyesha maziwa yake....Serikali yamkamata na kumfunga miaka miwili jela

Image
MWANAMKE mmoja raia wa Zimbabwe aliyenyonyesha mtoto wa jirani bila ruhusa anakabiliwa na kifungo cha karibu miaka miwili kwa kumwambukiza mtu HIV kwa kukusudia kwa kuwa yeye ni mwathirika. Annie Mpariwa, 39, alifikishwa mbele ya mahakama ya Gaborone wiki iliyopita na kesi hiyo iliahirishwa hadi Oktoba 24 kuruhusu kipimo cha pili cha HIV kufanyiwa mtoto huyo. Matokeo ya kwanza ya mtoto huyo yalionyesha hana virusi ilhali ya mama huyo yalikuwa na virusi. Mpariwa alikamatwa wiki jana kwa mashtaka ya usumbufu na iwapo mtoto huyo atapatikana na virusi, mashtaka hayo yatazidishwa hadi 'kumwambukiza mtu mwingine HIV kimakusudi.’ Mama wa mtoto huyo wa miezi 14, Nyasha Mironga, alisema kumwona mwanawe akinyonyeshwa na jirani wake lilikuwa ni jambo lililomshtua sana. Kisa hicho kimetokea baada ya kupitishwa kwa sheria mpya ya HIV/Aids inayotoa adhabu kali zaidi kwa wale wanaowaambukiza wengine HIV kimakusudi

WABAMBWA WAKIFANYA MAPENZI KWENYE NDEGE

Image
skip to main | skip to sidebar Wapenzi wawili wamekamatwa kutokana na kitendo cha kufanya ngono ndani ya ndege. Kwenye shitaka lao, wawili hao walipatikana na hatia hivyo kila mmoja alitozwa faini ya $250 kutokana na kitendo hicho kilichotokea wakati ndege hiyo ilipokuwa inatoka Medford, Ore., kwenda Las Vegas. Wapenzi hao walitozwa faini hiyo mnamo June 21, huku ikielezwa, abiria walishuhudia mwanaume aitwaye Christopher Martin, akijiachia kwa raha zake kwa kufanya mapenzi na mwenza wake aitwaye Jessica Stroble, licha ya onyo lililotolewa na wafanyakazi wa ndege hiyo wenza hao waliendelea kufanya yao. Baadaye Martin aliomba msamaha kwa wale walioumizwa au kukwazwa kutokana na kitendo hicho.  

Julius Nyaisanga (Mtangazaji wa zamani Radio One na Mkurugenzi wa Abood Media) afariki dunia

Image
Aliyekua mkurugenzi wa Abood media bwana Julius nyaisanga,amefariki dunia huko Morogoro katika hospitali ya Mazimbu... Marehemu aliwahi pia kufanya kazi katika kituo cha Redio Tanzania Dar es Salaam (RTD) na katika Kituo cha Redio One ambapo alikuwa Mkurugenzi. Mpaka sasa chanzo cha kifo chake bado hakijafahamika japo marehemu alikuwa akiugua kwa muda mrefu. Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi. AMEN! BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA JINA LA BWANA LIHIMIDIWE.