Posts

Showing posts from June 30, 2013

Hawa ndo WAPENZI WALIODONDOKA NA KUFA WAKATI WAKIFANYA MAPENZI DIRISHANI

Image
Wapelelezi wakifunika miili ya wapenzi hao eneo la tukio. Wapenzi wameanguka na kufa baada ya dirisha walipokuwa wakifanyia mapenzi kufunguka ghafla nchini China. Wawili hao wanasemekana kudondoka kutoka kwenye dirisha la jengo moja la makazi kwenye jiji la Wuhan nchini humo pale dirisha hilo walilokuwa wameegemea kufunguka. Mashuhuda walivieleza vyombo vya habari vya China kwamba wapenzi hao walikumbatiana wakati wakianguka kwenye njia ya waenda kwa miguu nje. Kwa mujibu wa The Sun, chanzo kimoja cha habari kilisema: "Huku wawili hao wakiwa wameshikamana vilivyo, walianguka nje ya jengo hilo." Picha za kuogofya zimefichuliwa kwenye tovuti za nchini humo zikionesha wapenzi hao wakiwa wamefunikwa kwa mashuka na polisi. Damu ilitapakaa kwenye njia ya waenda kwa miguu karibu na wapelelezi wanaonekana wakichunguza eneo la tukio. Miili ya wapenzi hao ilipigwa picha karibu na baiskeli ambayo ilikuwa imelazwa chini, lakini hakukuwa na ripoti zozote kwa

OBAMA na MKEWE WAKIWA WAMEVAA VAZI LA KIASILI LA KIZULU

Image

HATIMAYE LULU AFANYA INTERVIEW YA KWANZA TANGU ATOKE JELA, UTAIPATA HAPA

Image
Hatimaye mwanadada Elizabeth Michael a.k.a Lulu amefanya interview yake ya kwanza rasmi baada ya kipindi cha takribani mwaka mmoja na nusu toka atoke jela. Katika kipindi hicho kitakachorushwa hivi karibuni lulu ameongelea mambo mengi sana hasahasa experience yake ya maisha ya jela na mambo mengine mengi. Naye Lulu kupitia mtandao mmoja wa kijamii aliandika. “Kwa zaidi ya mwaka na nusu sasa!!!hii ni interview yangu ya kwanza baada ya kipindi chote hicho....thanks zamaradi….” Unahisi ameongelea mambo gani mengine? Tupe maoni yako

BINTI AOZA MKONO BAADA YA KUANGUKA KATIKA BAISKELI....MADAKTARI WAMESHINDWA KUUPONYA, MAOMBEZI YAHITAJIKA

Image
Janeth Nicholaus (25)mkazi wa Rwanzari Manispaa ya Tabora akionesha mkono wake wa kulia ukiwa tayari umeanza kuoza baada ya kupata ajali ya baiskeli maarufu daladala wakati akitokea nyumbani kwenda Soko kuu la Tabora mjini ajali ambayo ilitokea kwenye makutano ya barabara ya NBC.  Huu ndio mkono wenyewe unavyoendelea kuharibika baada ya kupita hospitali kadhaa hapa Tabora mjini na kushindikana kupona lakini sasa aliamua kufika kwenye huduma ya Maombezi  Kanisa la AGAPE MIRACLE CENTER Mwanza road Tabora manispaa kwa Mchungaji Mbagata.

LOWASSA AMTAKA OBAMA ASIZUNGUMIE MAMBO YA USHOGA NA NDOA ZA JINSIA MOJA AKIWA TANZANIA

Image
Mwenyekiti wa Kamati ya Mambo yaNje na Ushirikiano wa Kimataifa, Edward Lowassa, amemtahadhalisha kujiepusha na kauli za kuunga mkono ushoga.   Lowassa ambaye pia ni Mbunge wa Monduli, ameliambia NIPASHE Jumapili ofisini kwake jijini hapa jana kuwa ushoga na hai za ndoa kwa watu wa jinsia moja vinaweza `kuiharibu’ ziara yake hapa nchini. Mapema wiki hii, Rais Obama alikaririwa akizungumzia masuala hayo yanayotajwa kuwa ni moja ya haki za msingi za binadamu, alipokuwa Senegal, lakini akapingwa.   “Watanzania hawatalikubali na wataendelea kushikilia uhuru na heshima walizojengewa tangu awali, kwamba ushoga na ndoa za jinsia moja havikubaliki,” alisema. Akiwa Senegal, Rais Obama alitaka serikali za Afrika kutoa haki kwa mashoga kama inavyotoa kwa raia wengine.   "Ninachotegemea, I pray and hope (ninasali na kutegemea) kwamba kuhusu mashoga na ndoa za jinsia moja, Rais Obama hatarudia kauli aliyoitoa kule Senegal,” alisema. Aliongeza, "ninasema hivi k