Posts

Showing posts from May 20, 2014

MBINU TANO(5) ZA KUISHI NA WAFANYAKAZI WENZAKO AMBAO NI WAKOROFI

Image
Huyu mtu siku zote ni mkorofi na mwenye kukusababishia hasira. Hata ukiongea naye kwa utaratibu lazima alete maudhi, anakusababishia kazi uione mbaya kila unapomwona. Unahitaji mbinu za kuishi naye.   1. Utambue ya kuwa sio wewe peke yako Unaweza kusema kwamba huyu mtu ana visa na wewe tu, mara nyingi watu wa namna hii ni kwa jinsi tu ya tabia zao na namna walivyokuzwa. Jitahidi kwa kadri uwezavyo kutotilia maanani wanachokiongea ili usiingie kwenye ugomvi bila sababu. Wengine huwa hawajui kwamba wanakera wenzao kwa namna ambavyo wanafanya au kuongea, wao hupenda namna wanavyojisikia kila wanachofanya au kusema ndio furaha yao. 2. Jiepushe nao Punguza au ujiepushe kukutana nao mara kwa mara ili kupunguza kero. Hata kama watafika ofisini kwako, onyesha uko kikazi zaidi kuliko utani na mambo yasiyo ya msingi. Kama kuna jambo wanauliza waombe kukutumia barua pepe au kuacha ujumbe kwenye dawati lako la kazi. Unapopunguza kukutana nao mara kwa mara unaboresha nam

ANGALIA PICHA UKATILI MTOTO ALIYELIPULIWA NA MAMA YAKE

Image
Mtoto Samwel Paulo akiwa hospital baada ya kufanyiwa kitendo cha kinyama na mama yake mzazi. Dunia haina huruma! Mtoto Samwel Paulo (13), anayesoma darasa la nne Shule ya Msingi Amani wilayani Ilala, Dar, amelazwa wodi ya watoto katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, akiendelea kuuguza majeraha yaliyotokana na kile kinachodaiwa ni kulipuliwa kwa moto na mama yake mzazi aliyetajwa kwa jina la Doricus Iganga.  Tukio hilo la kusikitisha lilitokea nyumbani kwao maeneo ya Mombasa Gongo la Mboto, Dar mwishoni mwa wiki iliyopita, saa 8:00 usiku ambapo mwandishi wa habari hii alimtembelea wodini hapo. Alipoulizwa kisa na mkasa hadi kuwa katika hali mbaya kiasi hicho, mtoto huyo alikuwa na haya ya kusema: “Najisikia vibaya sana kutokana na maumivu makali ya moto. Sikutegemea kama mama yangu mzazi angenifanyia hivi kwa kunituhumu kuwa nimemuibia fedha zake shilingi elfu kumi. “Amekatisha ndoto yangu ya masomo, kwa sasa wenzangu wanajiandaa na mtihani wa muhula

HATARI SANA: DIVA WA CLOUDS FM AWAPA MAKAVU LIVE WANAOCHONGA KUHUSU ISHU YAKE NA WEMA SEPETU...

Image
Diva ameandika katika page yake instagram kama ifuatavyo: Kuna Mtu Amenitusi na team zao sijui nini na nini... So umeniita Kibaraka wa @wemasepetu ryt?! very good .. ndio mie kibaraka wake kwani do you have Problem with that ?! come on now ....  i love her and yes she is my girl and ndio mie kibaraka wake.. mitusi na kumtusi my baby unapoteza muda coz yes i love my baby hata kama unahisi sio type yangu but humjui .. ushaenda bank kuangalia salio lake? uyo mbunge si umfuate wewe kama unamtaka? my life my rulz nachagua nani niwe nae nani simtaki.. uyo unamuona hanifai mwenzio ndio sili silali sababu yake.... yaan dats my future husband... afu wema ndio my girl sasa na nitamtetea daily nikiona mnamkosea....afu ka hujui ushajijua wewe ulienitukana kurasa na kuingilia hadi familia yangu uso na adabu unaetafuta followers kinguvu... i am team @wemasepetu for life and speaking of my baby well .....   nitakua nae ndio wangu tena Mpaka kifo kitakapotutenganisha... asa ki

REKODI NA SIFA ZA KOCHA MPYA WA MANCHESTER UNITED

Image

ANGALIA PICHA NJIWA MWENYE HIRIZI ATIKISA MUHIMBILI

Image
Njiwa aliyetua kwenye kitanda cha mgonjwa na baada ya muda mgonjwa akafariki. Hofu kubwa ilitanda katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jumatatu ya wiki iliyopita, baada ya Njiwa mweusi, mwenye miguu myekundu akiwa na hirizi iliyofungwa katika mojawapo ya mabawa yake, kutua katika miguu ya mgonjwa aliyekuwa amelazwa wodi namba tatu, jengo la Mwaisela.Taarifa zilizopatikana kutoka kwa baadhi ya wauguzi wa wodi hiyo ambao hawakutaka majina yao yaandikwe gazetini, walisema tukio hilo lilitokea saa 3.55 asubuhi ambapo njiwa huyo aliingia kupitia dirishani na kwenda kutua mguuni mwa Mwanahawa Ngunda (61) aliyekuwa amelala kitanda namba 7, ambaye anadaiwa kuwa mkazi wa Kimara. Njiwa huyo aliingia dirishani muda mfupi baada ya mgonjwa aliyekuwa jirani na Mwanahawa, aitwaye Fatuma Musa (45) kurejea wodini hapo akitokea kupata vipimo ambapo alisaidiwa na ndugu zake kupanda kitandani kutokana na kuishiwa nguvu. Inadaiwa kuwa baada ya kuingia wodini, njiwa huyo alianza

HOMA YA DENGUE YABISHA HODI MBEYA, MGONJWA ALAZWA HOSPITALI YA MKOA

Image
HATIMAYE ugonjwa wa homa ya  Dengue umeripotiwa kuingia Mkoani Mbeya baada ya kupatikana kwa kesi ya mgonjwa mmoja mwanamke ambaye amelazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Mbeya. Mwanamke huyo ambaye ni mkazi wa Sae,  Jijini hapa, ambaye hata hivyo hakuwa tayari jina lake liandikwe gazetini  inasemekana alipata ugonjwa huo baada ya kung’atwa na  mbu aina ya Aides alipokuwa akiishi ,  Jijini Dar es salaam. Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo, Dk. Gloria Mbwile, alithibitisha kupokelewa kwa  mgonjwa huyo na kwamba tayari hali yake imeimarika baada ya madaktari kumpatia matibabu baada ya kufikishwa hospitalini hapo. Amesema mgonjwa huyo alifikishwa hospitalini hapo Mei 17  majira ya mchana,  huku akionesha kuwa dalili zote za ugonjwa huo Amesema kutokana na hali hiyo madaktari walianza kuchukua hatua za haraka kwa kuchukua sampuli za vipimo kwa ajili ya kuvipeleka Dar es salaam kwa uchunguzi zaidi, wakati huo huo wakimtoa katika wodi ya wagonjwa m

HOMA YA DENGUE YABISHA HODI MBEYA, MGONJWA ALAZWA HOSPITALI YA MKOA

Image
HATIMAYE ugonjwa wa homa ya  Dengue umeripotiwa kuingia Mkoani Mbeya baada ya kupatikana kwa kesi ya mgonjwa mmoja mwanamke ambaye amelazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Mbeya. Mwanamke huyo ambaye ni mkazi wa Sae,  Jijini hapa, ambaye hata hivyo hakuwa tayari jina lake liandikwe gazetini  inasemekana alipata ugonjwa huo baada ya kung’atwa na  mbu aina ya Aides alipokuwa akiishi ,  Jijini Dar es salaam. Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo, Dk. Gloria Mbwile, alithibitisha kupokelewa kwa  mgonjwa huyo na kwamba tayari hali yake imeimarika baada ya madaktari kumpatia matibabu baada ya kufikishwa hospitalini hapo. Amesema mgonjwa huyo alifikishwa hospitalini hapo Mei 17  majira ya mchana,  huku akionesha kuwa dalili zote za ugonjwa huo Amesema kutokana na hali hiyo madaktari walianza kuchukua hatua za haraka kwa kuchukua sampuli za vipimo kwa ajili ya kuvipeleka Dar es salaam kwa uchunguzi zaidi, wakati huo huo wakimtoa katika wodi ya wagonjwa m

MUUGUZI MWENYE HIV AFUNGWA JELA UGANDA

Image
Muuguzi Namubiru aliambia mahakama hakuwa na nia ya kumuambukiza mtoto huyo HIV Nchini Uganda mahakama imempata na hatia muuguzi mwenye HIV, aliyeshitakiwa kwa kumdunga mtoto mchanga sindano, ambayo awali ilimchoma yeye mwenyewe. Muunguzi huyo, Rosemary Namubiru, mwenye umri wa miaka 64, mwathiriwa wa virusi vya HIV, amefungwa miaka mitatu jela, kwa kile hakimu amekiita, 'uzembe wa weledi'. Hukumu hio imetolewa wiki moja baada ya bunge la Uganda kupitisha muswada, unaomtia hatiani mtu yeyote ambaye kusudi anamuambukiza mtu mwengine virusi vya ukimwi. Mtoto huyo hata hivyo hakuambukizwa virusi vya HIV na wanaharakati wamekosoa mahakama kwa kumfunga jela mwanamke huyo. Bbake mtoto huyo hata hivyo alielezea kufurahishwa na uamuzi wa mahakama. Baba huyo, Daniel Mushabe, amesema kuwa anatumai kesi hiyo itampa motisha Rais Museveni kuidhinisha mswada uliopitishwa na wabunge wa kuwachukulia hatua za kisheria watu wa

YALIYOJIRI KWENYE MSIBA WA DIRECTOR WA FILAMU ADAM KUAMBIANA!

Image
Mwili wa Adam Kuambiana ukiandaliwa tayari kwa kuagwa nyumbani kwake Bunju B jioni hii. Waombolezaji wakiwa msibani tayari kuaga mwili. Wa tatu kutoka kulia waliokaa mbele ni mke wa marehemu Janeth Rithe ambaye ni Diwani Kata ya Kunduchi, Dar. Watangazaji Sauda Mwilima (kulia) na Zamaradi Mketema (kati) wakiwa msibani hapo. Kushoto ni msanii Shamsa Ford. William Mtitu (katikati) akiwa na waombolezaji. Ibada ya kumuombea marehemu ikiendelea. Mwili wa marehemu Adam Kuambiana ukitolewa kwa ajili ya kuagwa. Baadhi ya wasanii baada ya kuwasili Bunju B. Mwili wa marehemu ukiwasili nyumbani Bunju B. Mwili wa marehemu ukishushwa kutoka kwenye gari Bunju B. MWILI wa mwongozaji na mwigizaji wa filamu Bongo, Adam Kuambiana umeagwa nyumbani kwake Bunju B, Dar ambapo ndugu, jamaa, wanasiasa, marafiki wameshiriki tukio hilo. Kesho asubuhi mwili utapelekwa Viwanja vya Leaders kuagwa na baadaye kuzikwa katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar

KINANA AWASILI SINGIDA

Image
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini Ndugu Lazaro Nyalandu katika kijiji cha Kaskazi mkoani Singida,Katibu Mkuu atakuwa kwenye ziara ya siku nane mkoani Singida.  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisaidiana na mafundi kupandish bati wakati wa ujenzi wa maabara ya shule ya sekondari Mgando,Singida  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiongozana na viongozi wa CCM mkoa wa Singida na Kundi la akina mama wajasiriamali wa Itagata kuelekea kwenye mkutano wa hadhara  baada ya kufungua shina la akina mama hao wa Itagata,Singida.  Katibu Mkuu Ndugu Abdulrahman Kinana akikagua mradi wa bwawa la maji la Itagata,Singida.  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa Itigi mkoani Singida .  Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Itigi na kuwaambia  CCM ipo imara na kuwaambia wananchi hao muungano  wa vyama vya siasa unaofahamika  k