Posts

Showing posts from May 25, 2015

NEC YATOA RATIBA YA UCHAGUZI MKUU

Image
Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi (Nec), Jaji mstaafu Damian Lubuva. TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetoa ratiba ya Uchaguzi Mkuu kwa mwaka huu 2015. Katika taarifa iliyotolewa na Mwenyekiti wa tume hiyo, Jaji Damian Lubuva ni kwamba; Agosti 21, 2015: Uteuzi wa wagombea Urais, Ubunge na Udiwani. Agosti 22 - Oktoba 24, 2015: Kampeni za uchaguzi. Oktoba 25, 2015: Siku ya kupiga kura.   NINI MAONI YAKO MDAU WETU

BOSS LADY ZARI ATUA MWANZA KWA SIRI SIKU YA JEMBEKA FESTIVAL.

Image
Mama kijacho wa msanii nyota Diamond Platinum atua jijini Mwanza kumsindikiza kipenzi chake kazini.Wengi hawakuweza kufahamu uwepo wake kutokana na usiri uliowekwa na star huyo wa bongo fleva kwa sasa. Tukio hilo linafananishwa na lile la ujio wa mwanamuziki wa hiphop Jay Z miaka ya nyuma na mkewe Beyonce bila mashabiki kutambua.Ingawa washabiki wa Diamond Platinum wana hamu ya kumuona boss lady huyo.

EDWARD LOWASSA AFUNGUKA MAZITO DODOMA LEO

Image
Waziri Mkuu aliejiuzulu Edward Lowassa amesafirisha wahariri wakuu wa vyombo vyote vya habari toka Dar es salaam na kufanya nao mkutano maalum leo nyumbani kwake mjini Dodoma. Katika mkutano huo kwa ufupi Lowassa amesema yafuatayo; 1. Amesema Hahusiki lolote na sakata la Richmond na ndio sababu hata kamati ya Mwakyembe haikuona sababu ya kumhoji. Amesisitiza kuwa cheo cha uwaziri mkuu ndio ilikuwa lengo la kamati ya mwakyembe na spika wa bunge kipindi hicho Samwel Sitta. Amesisitiza hicho sio kikwazo kwake katika kuingia Ikulu kwani sakata la Richmond lilipikwa kumchafua. Amechukua muda mrefu kuzungumzia hili la Richmond na amesema atalisema zaidi Arusha wikendi hii. 2. Anaamini kila mtangaza nia ana makundi ya kumuunga mkono. Yeye katika mkutano huu na wahariri leo ameambatana na Nazir Karamagi, Peter serukamba, Diana chilolo, Hussein Bashe na wengineo huku wengi wakiwa ni waliojeruhiwa katika serikali ya awamu ya nne akiwemo Aliekuwa DC Igunga Elibariki K

HISTORIA MPYA ALIYOANDIKA DIAMOND PLUTNUMZ MWANZA

Image
Diamond Plutnumz alikwenda mwanza kufanya show ya jembeka festival ila mapokezi yake yali dhihirisha kuwa msanii huyu ni mtu wawatu kama unamchukulia poa tazama picha zote hapa!! MAPOKEZI YA DIAMOND YALIKUWA HIVI UNAAMBIWA AKIENDA KUFANYA SOUND CHEK TAYARI WALIKU WAWANAMNGOJEA  BODA BODA WALIAMUA KUMSINDIKIZA MTU WA WATU  SOUND CHECK SHOW BADO DONE AKISEMA NA WATU WAKE  Posted by Boss Ngasa

RAIS JAKAYA KIKWETE APANGUA TENA WAKUU WA WILAYA

Image
THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS Telephone: 255-22-2114512, 2116898 E-mail: ikulucommpress@googlemail.com Website : www.ikulu.go.tz  Fax: 255-22-2113425 PRESIDENT’S OFFICE, STATE HOUSE, 1 BARACK OBAMA ROAD,  11400 DAR ES SALAAM. Tanzania. TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Bwana Anthony Peter Mavunde kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa, Mkoa wa Dodoma, kuanzia leo, Jumatatu, Mei 25, 2015. Aidha, Rais Kikwete amefanya uhamisho wa wakuu 10 wa Wilaya kwa nia ya kuongeza ufanisi katika uongozi wa Wilaya mbali mbali nchini. Katika mabadiliko hayo, Rais Kikwete amemhamisha Luteni Edward Ole Lenga kutoka Wilaya ya Mkalama, Mkoa wa Singida kwenda kuwa mkuu wa wilaya mpya ya Kyerwa, Mkoa wa Kagera. Luteni Lenga anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Luteni Kanali Benedict Kulikela Kitenga ambaye alifariki dunia Aprili 20, mwaka