Posts

Showing posts from June 14, 2014

ANGALIA PICHA ZA DIAMOND,SHILOLE,SAID FELLA,BABU TALE,MARTIN KADINDA NA WASANII WENGINE

Image
 Martin Kadinda akiwa na Shilole Ndani ya Uwanja wa Jamhuri Dodoma  Martin Kadinda na Diamond wakijadiliana  Shilole,Martin Kadinda na Diamond Mzee Chilo na Diamond wakishow love katika Uwanja Jamhuri Dodoma Leo hii Ambapo wasanii wote watahusika katika Jukwaa Moja

PICHA ZA TAMASHA LA UZINDUZI WA VIDEO YA MIAKA 50 YA MUUNGANO WA TANZANIA

Image
Diamond Platnumz akiwa katika pozi pamoja na baunsa wake Habari picha toka  tamasha la uzalendo na uzinduzi wa video ya miaka 50 ya Muungano wa Tanzania iliyoimbwa na wasanii wakubwa 50 kutoka pande zote za Tanzania.  Mgeni rasmi ni Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania. Wasanii Diamond Platnumz, Ommy Dimpoz, Mwana FA, Weusi, Hadija Kopa, TMK Wanaume na Yamoto Band na wengine wengi watatumbuiza Mzee Chilo akiwa na Diamond Msanii wa mziki alietokea EBSS, Menina na Rachael Kizunguzungu wakifatilia uzinduzi wa Mwanamziki wa Twanga Pepeta, Kalala Junior (katikati). Umati wa watu waliojitokeza katika uzinduzi wa Video ya Wimbo wa Muungano katika uwanja wa Jamhuri, Dodoma.

PICHA DIAMOND AKIWA NA MZEE CHILO LEO HII MJINI DODOMA

Image
Mzee Chilo na Diamond wakishow love katika Uwanja Jamhuri Dodoma Leo hii Masaa  machache kabla ya Show leo Ambapo wasanii wote watahusika katika Jukwaa Moja.

FLORA MBASHA AVAMIWA NYUMBANI KWAKE NA WATU WASIOFAHAMIKA

Image
SIKU chache baada ya tuhuma za ubakaji na mzozo wa familia ya mwimba Injili mahiri nchini, Flora Mbasha na mumewe, Emanuel Mbasha, mambo mengine yameibuka.    Yaliyoibuka safari hii ni taarifa kwamba, juzikati, Flora alivamiwa na watu wasiojulikana nyumbani kwake, Tabata Kimanga jijiini Dar dakika chache baada ya yeye kuingia na gari akitokea mafichoni anakoishi kwa sasa.   Kwa mujibu wa chanzo, siku ya tukio ilikuwa  saa 9.15 alasiri ambapo Flora aliingia nyumbani kwake na kufunguliwa geti kubwa kisha kuingiza gari ndani na geti kufungwa tena.   “Flora aliingia na gari akitokea hotelini anakoishi kwa sasa. Alikuwa ameshaingia na geti likafungwa. Ghafla, watu wakafika na kugonga geti hilo kwa nguvu huku wakisema watalibomoa geti kama wenyeji hao hawatafungua,” kilisema chanzo. Chanzo kikazidi kudai kwamba, ilibidi Flora apige simu polisi ili wafike kumuokoa yeye na familia yake.   “Polisi wawili walifika haraka sana wakiwa na bunduki na kukuta wale wat

ANGALIA PICHA INASIKITISHA; BOMU LALIPUKA DARAJANI ZANZIBAR, MMOJA AFARIKI

Image
  Mlipuko unaosadikiwa kuwa ni bomu jana Juni 13, 2014  ulilipuka eneo la Darajani Zanzibar na kusababisha kifo cha mtu mmoja na kujeruhi watatu. Tarifa zinasema mlipuko Huo umetokea baada ya waumini wa dini ya kiislamu kumaliza muhadhara uliokuwa ukitolewa Miskiti wa darajani baada ya salsa ya Isha. Aliyekufa ni mmoja kati ya wahadhiri waliokuja kutoka Tanga na Sheikh Hamad ndiyo aliyekuwepo theater. Na Sheikh Kassim Mafuta kaumia kidogo. Majeruhi 3 wamelazwa hospitali ya Mnazi Mmoja, Zanzibar wakiwa na majeraha madogo 'madogo. Majeruhi wa nne yupo theatre sasa hivi na nali yake sio mbaya. Picha/Habari na Salim Sujae

JAQUELINE WOLPER ANASWA LIVE NA MUME WA MTU

Image
KABANG!  Baada ya kutoonekana katika pozi za kimahaba kwa muda mrefu, kwa mara ya kwanza, staa wa sinema za Kibongo, Jacqueline Wolper Massawe ‘Gambe’ amenaswa ‘live’ na mwanaume anayedaiwa kuwa ni mume wa mtu, Risasi Jumamosi limesheheni. Jacqueline Wolper Massawe ‘Gambe’ amenaswa ‘live’ na mwanaume anayedaiwa kuwa ni mume wa mtu.   Kwa muda mrefu Wolper amekuwa makini na picha zake za kimahaba tangu alipokuwa akitoka kimapenzi na mfanyabiashara maarufu jijini Dar, Abdallah Mtoro ‘Dallas’.   CHANZO CHAMWAGA MTONYO Awali, chanzo makini kilipenyeza habari kuwa kuna mawasiliano yamenaswa ‘kimafia’ ambayo yalitoka kwa Wolper kwenda kwa rafiki yake yakionesha anabanjuka na mwanaume huyo wa mtu aliyejulikana kwa jina moja la Gee.   YADAIWA NI MUME WA SHOSTI YAKE Chanzo hicho kilikwenda mbali zaidi kwa kudai kwamba licha ya kuwa ni mume wa mtu, mwanaume huyo ni bwana wa rafiki yake kutokana na mawasiliano hayo yalivyosomeka.   “Mashabiki kila siku huwa wanamtetea Wolpe

ZIJUE DAWA ZA NYWELE ZINAZOSABABISHA UVIMBE WA KIZAZI.

Image
Dawa za kulainisha nywele (relaxer) zimekuwa zinapendwa na wanawake wengi wa Afrika kwa kuwa zina uwezo wa kulainisha nywele na kumfanya apendeze na awe wa kuvutia. Hata hivyo, wataalamu wa afya wanadai kuwa dawa hizo zinasababisha uvimbe kwenye kizazi kutokana na kemikali za dawa hizo ambazo huingia mwilini kupitia majeraha au ngozi wakati wa kupaka . Daktari wa Manispaa ya Ilala, Laurent Chipata alifanya utafiti na kubaini kuwa dawa za nywele na vipodozi zina kemikali ambazo husababisha uzalishwaji wa vichocheo kwa kiasi kikubwa na kusababisha uvimbe kwenye kizazi uitwao fibroids au leimyoma. "Kemikali hizi hupenya kwenye ngozi na wakati mwingine hata kwa harufu tu, husababisha kuzalishwa kwa wingi wa vichocheo aina ya estrogen ambavyo huchangia kuota kwa uvimbe wa fibroids," anasema. Dk Chipata anasema kukua kwa uvimbe kwenye kizazi hutokea katika kipindi ambacho mama yupo kwenye uzazi yaani kabla hajakoma hedhi. Utafiti

LIVE KUTOKA KENYA MDA HUU:::TAZAMAPICHA 5 ZA MWILI WA MAREHEMU GEORGE TYSON NDIO UNATOLEWA MOCHWARI KUPELEKWA SIAYA KWA MAZISHI

Image
Ndugu jamaa na marafiki wakiwa wamebeba jeneza la Marehem George Tyson wakati wanautoa mwili wa marehemu kutoka chumba cha kuhifadhia maiti leo asubuhi tayari kwa safari ya kuelekea Siaya kwaajili ya mazishi.  Mwiliwa Marehemu George Tyson ukipelekwa kwenye gari kwenda Siaya kwa mazishi  Waombolezaji wakati wakijianda kuelekea Siaya, eneo ambalo atazikwa marehemu George Tyson  Mmoja wa Ndugu wa marehemu

CAMEROON WACHAPWA GOLI MOJA BILA NA MEXICO

Image
LONG WAIT: ORIBE PERALTA (LEFT) GIVES MEXICO THE LEAD IN THE 61ST MINUTE Ahead: Peralta wheels away in celebration after given Mexico a deserved lead in the Group A clash Jubilant: The Mexico players celebrates the opening goal with the substitutes on the sidelines Bad  day: Giovani Dos Santos saw two seemingly fair goals disallowed during the  first half One to forget: Samuel Eto'o missed a glorious chance to give his side the lead in the first half Friday’s decisions were worse. Dos Santos was denied his first goal even though he was level with the last Cameroon defender and he was later ruled offside when the ball had gone to him via the head of opponent Eric Choupo-Moting. Before kick off, nearly 20,000 Mexican fans provided a party atmosphere in Natal despite pouring rain.