Posts

Showing posts from March 14, 2016

Maskini Millen Magese..Ugonjwa Wake Waendelea Kumsumbua Afanyiwa Operation Mara 13...Ashindwa Kufanya Show Afrika Kusini

Image
Akiwa kitandani, Millen Magese anaongea kwa tabu baada ya kuzidiwa katikati ya onesho la Mercedes Benz Fashion Week, jijini Johannesburg, Afrika Kusini. Anawatoa hofu mashabiki wake kwasababu kilichotokea kiliwashtua. Akiwa kwenye kitanda cha hospitali, mwanamitindo huyo aliyewahi kuwa Miss Tanzania, anasema kiwango cha sukari kilikuwa kimeshuka kwa kiasi kikubwa kutokana na kupata maumivu makali na kutokwa damu nyingi kwa siku nane mfululizo. Millen akipewa huduma ya kwanza baada ya kuzidiwa Kutokana na tukio hilo, Millen ameshindwa kuendelea kushiriki kwenye show hiyo kubwa ya fashion. Maumivu anayoyazungumzia Millen si maumivu ya kawaida, ni maumivu makali. Mrembo huyo yupo kwenye vita vigumu na virefu dhidi ya ugonjwa uitwao Endometriosis. Ni ugonjwa ambao huhusisha seli zinazofaa kuwa ndani ya mji wa uzazi kuwa nje ya mji huo. Millen na wanawake wengine wanaosumbuliwa na ugonjwa huo hukabiliana na maumivu makali kila nyakati za siku zao za hedhi. N

Mike Tyson auza mjengo wake wa Las Vegas

Image
Mike Tyson. -UNGEPENDA kuishi kistaa na una kiasi cha Dola za Marekani Usd milioni 1.5 sawa na shilingi bilioni 3.3? Kama hivyo ndivyo, basi unaweza kununua mjengo wa kifahari wa mwanamasumbwi wa zamani wa Marekani, Mike Tyson. Staa huyo ameishi katika mjengo huo wenye futi za mraba 5,800 tangu mwaka 2008 ila sasa ameamua kuhamia kwenye mjengo mpya wenye vyumba vitano vya kulala na mabafu sita. Mbali na kuhama, mjengo huo bado hauko vibaya maana una sehemu tatu za kupashia moto nyumba (fireplaces), chumba cha kukutana na wahabari, sehemu ya kunywea mvinyo, eneo la kuchezea pool na maporomoko yaliyo sehemu ya kuingilia jumba hilo. Wakala wa Tyson, Ken Lowman, ameeleza kuwa eneo hilo lote limefanyiwa maboresho mapema mwaka huu na lipo katika muonekano mzuri japo linakosa kitu kimoja ambacho ni sehemu ya kufugia chui.

Mke, mume wazua timbwili studio za radio

Image
Wakiwa studio. Stori:  Dustan Shekidele, Wikienda Morogoro: Kioja! Mwanamke Betina Kimbe (25) na mumewe, Emmanuel Peter (30), wamezua timbwili ‘hevi’ ndani ya Studio za Radio Planet FM ya mjini hapa baada ya mke kukimbilia redioni akiomba achangiwe nauli ya kurudi kwao mkoani lringa akitaka kumtoroka muwewe kwa sababu alimweka ‘bondi’ wakati wa Mechi ya Simba na Mbeya City iliyochezwa jijini Dar wiki iliyopita. Betina alitinga na mwanaye wa mwaka mmoja ndani ya studio hizo akitokea nyumbani kwa baba mtoto wake huko Dumila kwa madai ya kuchoshwa na mumewe huyo huku akimshushia tuhuma lukuki. MKE ‘AMTUMBUA JIPU’ MUMEWE Akihojiwa na Mtangazaji Warda Makongwa wa Kipindi cha Mcharuko wa Pwani cha Radio Planet FM, Betina alisema aliamua ‘kumtumbua jipu’ mumewe huyo kufuatia mateso aliyokuwa akiyapata kila kukicha. “Nilipojifungua mtoto huyu, mume wangu alishinda klabuni, aliporudi nyumbani alikuja na mwanamke na kulala naye chumbani kwetu huku mimi akinilaza chini. “Nilip

BREAKING NEWS : ZITTO KABWE AFUNGUKA KUHUSU UTEUZI WA MAKONDA MTAKA NA SHIGELA

Image

MAGAZETI YA LEO JUMATATU TAREHE 14.03.2016

Image

BASI LA LEINA TOURS LA KAHAMA- DAR LAPATA AJALI,LATUMBUKIA MTARONI

Image
Basi la Leina Tours lililokuwa likitokea Kahama kwenda Dar es Salaam, limeacha njia na kutumbukia katika mtaro eneo la Kimara Bucha usiku wa kuamkia leo Idadi ya waliofariki haijafahamika ila waliojeruhiwa ni zaidi ya 30 na walikimbizwa Haospitali ya Mwananyamala na Muhimbili.

SAFARI ZA TRENI RELI YA KATI ZAANZA RASMI

Image
Huduma  ya usafiri  wa reli ya Kati iliyokuwa imesimama kwa takribani miezi miwili sasa imerejea kufuatia  kukamilika kwa ukarabati wa reli  hiyo katika eneo la kidete wilayani kilosa, mkoani Morogoro. Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa  amesema  hayo baada ya kukagua na kuridhika na ukarabati uliofanywa katika maeneo ya Magulu, Munisagara, Mzaganza na kidete Wilayani Kilosa. “Hakikisheni mnailinda reli hii kwa manufaa yenu na ya Taifa, leo hii reli iko vizuri na treni ya kwanza kutoka Dar Es Salam  kwenda bara itapita na kumaliza changamoto ya usafiri iliyokuwa inawakabili wananchi wanaotumiia reli hii”.Amesema Profesa Mbarawa. Profesa Mbarawa amewataka wananchi wa maeneo ya Kilosa, Magulu, Munisagara, Mzaganza, Kidete, Godegodena Gulwe ambao maeneo yao yanakabiliwa na mafuriko ya mto Mkondoa kuacha Kilimo cha kuelekeza Maji kwenye reli bali washirikiane na Serikali kudhibiti maji hayo kwenda kwenye  hifadhi ya reli. Ames

WAZIRI MKUU MAJALIWA AZUNGUMZA NA WATUMISHI WA SERIKALI,VIONGOZI WA DINI NA WADAU WA MAENDELEO WA MKOA WA KAGERA

Image
 Baadhi ya watumishi wa serikali, viongozi wa dini na wadau wa maendeleo wa mkoa wa Kagera wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  wakati alipozungumza nao kwenye ukumbi wa ELCT mjini Bukoba akiwa katika ziara ya mkoa wa Kagera Machi 13, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Watumishi wa serikali, Viongoze wa dini na wadau wa maendeleo wa mkoa wa Kagera kwenye  ukumbi wa ELCT mjini Bukoba Machi 13, 2016. Alikuwa katika siku ya kwanza ya ziara ya mkoa wa Kagera.

MBARAWA AFUNGUA RASMI SAFARI ZA TRENI RELI YA KATI

Image
Muonekano wa Sehemu ya Reli katika eneo la Kidete, Wilayani Kilosa, mara baada ya ukarabati kufuatia mvua kubwa zilizonyesha katika mikoa ya Iringa na Dodoma na kukata Mawasiliano kati ya Mkoa wa Morogoro na Dodoma. Kazi za ukarabati wa mwisho zikiendelea katika eneo la Kidete, Wilayani Kilosa, mara baada ya ukarabati kufuatia mvua kubwa zilizonyesha katika mikoa ya Iringa na Dodoma na kukata Mawasiliano kati ya Mkoa wa Morogoro na Dodoma. Treni ya Mizigo ikiwa tayari kuanza safari katika eneo la Kidete Wilayani Kilosa, kufuatia kukamilika kwa ukarabati wa eneo hilo, uliodumu kwa takriban miezi miwili na hivyo kurudisha mawasiliano ya reli kati ya Mkoa wa Morogoro na Dodoma. Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa akitoa maelekezo kwa Mhandisi wa Kampuni Hodhi ya Rasilimali za Reli (RAHCO), Mhandisi Felix Nlalio, kuhusu namna ya kudhibiti mkondo wa maji katika mto mkondoa yasiathiri hifadhi ya reli. Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na