Posts

Showing posts from April 24, 2018

MSIBA WA MASOGANGE WAZIMA NDOA YA ABDU KIBA

Image
MSIBA wa aliyekuwa video queen mkali Bongo, Agness Gerald ‘Masogange’ aliyefariki Ijumaa iliyopita, umezima tukio kubwa la kufunga ndoa la msanii wa Bongo Fleva, Abdul Kiba ambaye alioa jana alfajiri. Abdul Kiba ambaye amefunga ndoa siku tatu tu baada ya kaka yake, Ali Saleh Kiba ‘King Kiba’ aliyemuoa Amina Khaleef huko Mombasa nchini Kenya. Msanii huyo ambaye kwa sasa anafanya vyema na wimbo wake ya Jeraha alifunga ndoa hiyo jijini Dar, jana kwenye Msikiti wa Kichangani, Magomeni ambapo alimuoa mchumba wake wa muda mrefu, Luwada Hassan. Habari zilizolifikia Ijumaa Wikienda jana zilieleza kuwa, huenda Ali Kiba na Abdul Kiba wakafanya sherehe ya pamoja ya harusi Aprili 29, mwaka huu kwenye Hoteli ya Serena jijini Dar ili kufurahi na watu wao wa karibu kufuatia zoezi la wao kufunga ndoa. Taarifa zilieleza kuwa, baada ya Ali Kiba na Abdul Kiba kuoa, dada yao, Zabibu Kiba, naye anatarajia kufunga ndoa hivi karibuni na beki za zamani wa Timu ya Simba ambaye kwa sasa an

RC GAMBO AONGOZA MAZISHI YA LEYLA ARUSHA

Image
MKUU wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo , leo ameongoza mamia ya waombolezaji katika mazishi ya Leyla aliyeuawa na mumewe kwa kuchomwa visu na mumewe huko Uingereza wiki kadhaa zilizopita. Mazishi hayo yamefanyika katika makaburi ya Sinoni jijini Arusha. Kaburi la marehemu Leyla likiwekwa sawa baada ya mazishi yaliyofanyika katika makaburi ya Sinoni jijini Arusha leo. Mwili wa marehemu Leyla aliyeuawa na mumewe kwa kuchomwa visu na mumewe huko Uingereza wiki kadhaa zilizopita ukipelekwa makaburini. Mazishi yakiendelea. (Habari na Korumba Moshi, Arusha)

Mke mtarajiwa wa Jacob Zuma ajiuzulu kazi Afrika Kusini

Image
Mwanamke ambaye anatarajiwa kuwa mke wa saba wa aliyekuwa rais wa Afrika kusini,Jacob Zuma, Nonkanyiso Conco amejiuzulu kazi nchini Afrika Kusini. Jumamosi iliyopita Nonkanyiso (24) ambaye hivi karibuni alizaa mtoto wa kwanza na Zuma, alitangaza kujiuzulu mpaka ifikapo Jumatatu ya April 23. Conco analazimika kujiuzulu cheo chake akiwa ni afisa mawasiliano wa kampeni ya kukabaliana na maambukizi ya Virusi vya Ukimwi kwa wanawake wadogo, unyanyasaji wa kijinsia na ujauzito kwa watoto wadogo. Leonora Mathe ambaye ni naibu mwenyekiti wa shirika hilo, amethibitisha kuwa Conco ameandika barua hiyo. Hata hivyo mpaka sasa hajazungumza chochote juu ya uhuma hizo za kuhusishwa kuwa na mahusiano ya kimapenzi na Zuma. Wakati huo huo mrembo huyo anafanya kazi nyingine kwenye asasi inayohamasisha kampeni ya kuwawezesha mabinti wadogo katika maisha yao ya kila siku na kuacha kuwategemea wanaume wenye umri mkubwa. Taarifa za Jacob Zuma na Nonkanyiso Conco kuwa na mahusian

MZEE GELARD: AGNESS ALINIAGA KABLA HAJAFA, NIKALIA!

Image
MZEE Gerald Waya, ambaye ni baba mzazi wa aliyekuwa Msanii wa Bongo Movies na Model, Agness Gerald ‘Masogange’, amesema mwanaye alikuwa nguzo kubwa katika maisha yake, hivyo kifo chake ni pigo kubwa kwake na familia nzima. Akizungumza nyumbani kwake, Mbalizi wilayani Mbeya, Mzee Waya alisema Masogange ni mtoto wake wa nne katika familia ya watoto sita, wa kike wakiwa ni watano ambapo ameeleza kwamba Masogange alisoma Shule ya Msingi Utengule iliyopo Mbalizi na Sekondari ya Sangu ambapo alikomea kidato cha pili baada ya kupata matatizo. Aliishia kidato cha pili akapata matatizo, hivyo ilibidi aache shule. Tulikosana kidogo lakini tukayamaliza yeye akaenda Dar es Salaam. Agness amekuwa nguzo kwangu, alikarabati nyumba hii ninayoishi kwa sasa na nilikuwa nafarijika sana nikimuona, lakini leo kusikia msiba huu kwa kweli inaniuma sana,” alisema Mzee Waya. Alinipigia simu tukaongea naye akaniambia ‘mimi baba ninaumwa’, nikamuuliza nini tatizo akasema, ‘baba nio

Nafasi za Kazi TANROADS Tanzania

Image
Regional Manager, TANROADS – MOROGORO is looking for suitable qualified Tanzanian candidates for available Posts at Morogoro Weigh Bridge stations. Applications are invited from suitable qualified and competent Tanzanians to apply for the following position: POSITION TITLE: DRIVER (1 POST) A: KEY QUALIFICATION: 1. Holders of Form IV Certificate; 2. Holder of valid Class E driving license 3. Having driving experience of at least five (3) years 4. Must be fluent in both written and spoken English and Swahili languages 5. Age. Not above 35 years of age 6. Must be Tanzanian citizen. B: DUTIES AND RESPONSIBILITIES: 1. Driving Agency’s vehicle in urban and remote areas. 2. Maintaining the vehicle logbook and all accidents records pertaining to the assigned vehicle 3. Keeping the vehicle in good working order and clean condition 4. Reporting repairs or maintenance needs of the vehicle to the Shift In-charge timely 5. Observe good customer care, dignity and integ

Nafasi za Kazi NMB

Image
Senior Manager; Digital Lab Job Purpose The incumbent will be responsible to foster research, testing, and incubating of concepts, products and processes by leveraging on technology to deliver digital products which capture value, enhanced experience and capabilities to our customers. Main Responsibilities: Create, evolve, and scale a new method of delivering digital solutions, adopting a lean, fail fast delivery methodology based on Agile principles. Play a key role of a change agent responsible to influence peers, leaders within the bank to align, adapt to and use these new methodologies/technologies. Innovate from prototyping to testing with an eye towards encouraging speed to market in a dynamic and ever changing environment. Create a digital lab which will facilitate nurturing of new ideas into finalized solutions by establishing and drive the technical execution of the digital products. Create processes in the lab that are rooted in best practices for con

Mazoezi ya Polisi Moshi Mjini Yazua Taharuki

Image
Leo shughuli zimesimama kwa muda katika Mji wa Moshi wakati Vikosi vya Jeshi la Polisi vikipita katika maeneo mbalimbali ya mji huo wakiwa na silaha za moto na kuzua hali ya taharuki kwa baadhi ya wakazi wa Moshi.