Posts

Showing posts from August 27, 2015

LIGI YA MABINGWA ULAYA MANCHESTER UNITED YAUWA

Image
Klabu ya Manchester United August 26 imeshuka dimbani kucheza mechi yake ya marudiano na Club Brugge ya Ubelgiji, mchezo huo ambao Club Brugge imecheza nyumbani lakini imepokea kichapo cha goli 4-0. Magoli ya Man United yamefungwa na nahodha wa timu hiyo Wayne Rooney dakika ya 20, 49 na 57 huku goli la nne lilifungwa na Ander Herrera dakika ya 63. Picha za mechi Nakusogezea video ya magoli mtu wangu

Siri 4 MATUSI ya DIAMOND Kwa DIVA wa CLOUDS FM Hizi Hapa...

Image
  Loveness Malinzi ‘Diva’ NI mtifuano! Agosti 24, mwaka huu ilikuwa siku mbaya kwa nyota wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ au baba Tiffah na mtangazaji anayekimbiza kwa sauti tamu hewani, Loveness Malinzi ‘Diva’ kufuatia kupishana lugha ndani ya studio za redio na hivyo, Diamond kumvurumishia matusi mwenzake. Kupishana kauli huko kuliashiria kuwepo kwa uhasama wa siku nyingi kwa wawili hao huku kila mmoja akiwa anaamini mwenzake ana makosa na ndipo siri tano za Diamond kumtusi Diva zikajulikana. MCHEZO ULIVYOANZA Siku hiyo majira ya saa 9:00 alasiri, Diamond alitia timu kwenye studio za redio hiyo zilizopo Mikocheni, Dar kwa lengo la kumtambulisha msanii wake mpya kutoka studio yake ya Wasafi Records iliyopo Sinza-Mapambano, Dar.Mwanyeji wa Diamond alikuwa mtangazaji Hamis Mandi ‘B12’. Lakini ndani ya studio hiyo alikuwepo Diva. Nyota wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ au baba Tiffah. ALIANZA DIAMOND Kabla Diamond hajaanza kumtambulisha msanii wake, alianza

LULU Amhenyesha Vibaya MBOTO Ukumbini!

Image
Haji Salum ‘Mboto akisaidia kulibeba gauni la Lulu. DIVA wa filamu Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ hivi karibuni amemhenyesha staa mwenzake wa filamu, Haji Salum ‘Mboto’ baada ya kumpa kibarua cha kulishika gauni lake lisiguse chini. Tukio hilo lilitokea kwenye fainali ya shindano la kusaka vipaji vya kuigiza lijulikanalo kama Tanzania Movie Talents (TMT 2015) iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa, Posta jijini Dar ambapo Lulu na Mboto walikuwa washehereshaji. Katika hali iliyoonesha Lulu alikuwa ‘siriaz’ stejini alimsisitizia Mboto kila mara ahakikishe amelishika gauni lake vizuri na asiliachie. “Mboto hapa kazi yako ni kulishika gauni langu kwa nyuma kila nitakapokuwa nawe na ole wako uliachie,” alisikika Lulu ambapo Mboto alitekeleza ombi la Lulu.

WEMA SEPETU Amtafuta Shetani Tena!

Image
Beautiful Onyinye, Wema Isaac Sepetu. Anadaiwa kutafuta shetani mwingine wa ugomvi baada ya ‘kumalizana’ na Aunt Ezekiel Grayson na kuanzisha ushosti na mwigizaji, Yobnesh Yusuph ‘Batuli’, jambo ambalo linawapa wasiwasi mashabiki wao kutokana na dhana iliyojengeka kuwa mrembo huyo (Wema), hawezi kudumu na rafiki kwa kipindi kirefu. URAFIKI WAANZIA KWENYE KAMPENI ZA CCM Mastaa hao walianza kuwa na ukaribu mkubwa kwenye mambo ya Kampeni za Chama Cha Mapinduzi (CCM) zilizozinduliwa Jumapili iliyopita katika Viwanja vya Jangwani, Dar. Habari zilieleza kwamba, kabla ya hapo, wawili hao hawakuwahi kuwa na urafiki hata zaidi ya salamu. WEMA AMPOZA BATULI Chanzo ambacho ni mtu wa karibu na wawili hao kilieleza kwamba, baada ya Batuli kupata mkasa wa kuunguliwa nyumba aliyokuwa akiishi maeneo ya …Mbezi Beach, Dar, mwishoni mwa wiki iliyopita, mastaa hao walikuwa wote saluni na walipopata taarifa ya mkasa huo, Wema ndiye aliyempooza machungu Batuli kwa kumsaidia katika kipindi

Mbowe Akata Rufaa Mahakama kuu Dhidi ya Hukumu yake

Image
Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema, Freeman Mbowe amekata rufaa Mahakama Kuu kupinga hukumu iliyotolewa dhidi yake Julai, mwaka huu, na kumtoza faini ya Sh1 milioni baada ya kupatikana na hatia katika kosa la jinai. Mbowe alitozwa faini ya Sh1 milioni au kutumikia kifungo cha mwaka mmoja jela kwa kosa la kumshambulia mwangalizi wa ndani wa Uchaguzi Mkuu wa 2010 katika Wilaya ya Hai, Nassir Yamin. Hata hivyo, Mbowe ambaye pia ni mwenyekiti mwenza wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) na Mbunge wa Hai, alilipa faini hiyo na kuachiwa huru na Mahakama ya Wilaya ya Hai. Katika rufaa hiyo namba 33/2015, iliyofunguliwa na wakili Peter Kibatala, Mbowe anailalamikia mahakama iliyomtia hatiani kuwa ilishindwa kushughulikia hoja muhimu katika kufikia uamuzi huo. Pia, Mbowe analalamika kuwa mahakama ilishindwa kupima ushahidi kwa usahihi na pia, ilishindwa kutilia maanani ushahidi wa mashahidi wa upande wa utetezi akiwamo yeye. Mbowe analalamika kuwa mahakama ilishindwa kutumia msi

Sheddy Clever: Nimelipwa pesa nyingi sana kutayarisha wimbo wa Diamond na Ne-Yo

Image
Producer Sheddy Clever wa Burn Records amesema kuwa amepata pesa nyingi alizolipwa na Diamond kutengeneza collabo yake na Ne-Yo, kiasi ambacho ingemchukua miezi mitatu kuipata kwa kazi zake za kawaida za production. Sheddy ambaye ndiye producer anayepika collabo ya Diamond na Ne-Yo inayosubiriwa kwa hamu na mashabiki wa muziki wa Afrika, ameiambia phars kuwa hajawahi kulipwa kiasi hicho cha pesa toka ameanza kufanya production. “Hii kazi tuliyoenda kufanya juzi nimelipwa, na nimelipwa vizuri tu...sijawahi kulipwa hivyo kwakweli yaani nafurahi sana,” alisema kwa furaha. “Diamond ni msanii tofauti sana na haogopi kuwekeza katika kazi zake kwasababu anajua nini anachokifanya...Nimelipwa vizuri japokuwa kazi bado sijamaliza lakini nimelipwa pesa nyingi tu nzuri nimefikia hoteli nzuri.” alisema Sheddy. Sasabu wengi huwa hawapendi kusema kiwango wanacholipwa, nilipomuuliza kama amelipwa zaidi ya shilingi milioni 1 alijibu; Sheddy:[kicheko] Inazidi milioni 1 hata mi

LIGI YA MABINGWA ULAYA MANCHESTER UNITED YAUWA

Image
Klabu ya Manchester United August 26 imeshuka dimbani kucheza mechi yake ya marudiano na Club Brugge ya Ubelgiji, mchezo huo ambao Club Brugge imecheza nyumbani lakini imepokea kichapo cha goli 4-0. Magoli ya Man United yamefungwa na nahodha wa timu hiyo Wayne Rooney dakika ya 20, 49 na 57 huku goli la nne lilifungwa na Ander Herrera dakika ya 63. Picha za mechi Nakusogezea video ya magoli mtu wangu