Posts

Showing posts from February 25, 2014

KUHUSU MSANII KAJALA KUNYWA SUMU NA MPAKA KUKIMBIZWA HOSPITAL USIKU WA MANANE...!!

Image
Kajala ni miongoni mwa waigizaji wa Tanzania ambao wamekua wakimiliki headlines mara kwa mara nchini Tanzania.

KUANGALIA MECHI YA TWIGA STARS, ZAMBIA BURE

Image
Washabiki wa mpira wa miguu nchini watashuhudia bure mechi ya timu ya Taifa ya mpira wa miguu ya wanawake (Twiga Stars) dhidi ya Zambia (Shepolopolo). Mechi hiyo ya marudiano ya raundi ya kwanza ya michuano ya Afrika kwa Wanawake (AWC) itachezwa Ijumaa (Februari 28 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi, Dar es Salaam kuanzia saa 10 kamili alasiri. Twiga Stars ambayo ilipoteza mechi ya kwanza iliyochezwa Lusaka, Februari 14 mwaka huu kwa mabao 2-1 iko kambini chini ya Kocha Rogasian Kaijage na msaidizi wake Nasra Juma ikijiwinda kuwakabili Wazambia wanaotarajiwa kutua nchini Alhamisi (Februari 26 mwaka huu). Waamuzi wa mechi hiyo Ines Niyonsaba, Jacqueline Ndimurukundo, Axelle Shikana na Suavis Iratunga kutoka Burundi kutoka Burundi wanatarajiwa kuwasili nchini keshokutwa (Februari 26 mwaka huu). Kamishna Fran Hilton Smith kutoka Afrika Kusini yeye atatua nchini Februari 27 mwaka huu kwa ndege y

Milipuko ya mabomu yarindima Z’bar

Image
Na Mwinyi Sadallah, Mwananchi Zanzibar. Watu wanne wamejeruhiwa baada ya milipuko minne inayoaminika kuwa ni mabomu kutokea katika maeneo matatu tofauti Zanzibar. Katika moja ya matukio hayo, watu wanne walijeruhiwa, mmoja akikatika mguu, katika eneo la Unguja Ukuu, Mkoa wa Kaskazini Unguja. Majeruhi wawili wamelazwa katika Hospitali ya Mnazi Mmoja, Unguja. Mkuu wa Operesheni wa Polisi, Mkoa wa Kusini Unguja, Hamad Said Masoud alisema mlipuko wa kwanza ulitokea juzi katika eneo la Fuaoni Maili Nne wakati watu wasiojulikana waliporusha kitu kinachoaminika kuwa ni bomu wakati waumini wa Kanisa la Evangelist wakiendelea na ibada ya Jumapili. Kamishna wa Polisi Zanzibar, Hamdan Omar Makame alisema tukio la juzi, kitu kinachosadikiwa kuwa ni bomu kilirushwa wakati waumini wa kanisa hilo wakiendelea na ibada na kutoa mlipuko na kishindo kikubwa. Alisema wakati wakiendelea na uchunguzi wa tukio hilo, milipuko mingine mitatu ilitokea jana. Katika mlipuko wa kwanza kwa jana ul

Dalili za mume anayetembea kimapenzi na msichana wa kazi za ndani ‘hausigeli’.

Image
DALILI YA KWANZA Ishara ya kwanza ya mwanaume ambaye tayari yupo ndani ya uhusiano wa kimapenzi na msichana wa kazi ni kupenda sababu za kumwamsha mfanyakazi huyo  hata pale anaporudi na kumkuta amelala. Utakuta baba amerudi nyumbani usiku wa saa sita, mkewe anamfungulia mlango, akishaingia na kukaa, anaanza: “Dada amelala?” Mke: “Ndiyo.” Baba: “Mwamshe nimpe kazi f’lani.” Mke unaweza ukamtetea sana msichana, lakini mumeo akasimamia msimamo ule ule. Sasa utakapomwamsha, akifika, mumeo utamuona anavyojipinduapindua. “Hii mboga umepika wewe dada?” “Hapana, mama.” “Ooo. Ulifua zile soksi zangu?” “Ndiyo baba.” “Sawa kalale.” Mke unajiuliza, sasa kumwamsha kote kule ndiyo maswali yenyewe hayo tu. Sasa tuendelee… Katika hali kama hii, wewe mke jaribu kuwa makini sana. Hakikisha hutoi nafasi kwa mumeo kumfikia au kuwasiliana na hausigeli kwa kitu chochote. Kama ni maji ya kuoga tenga wewe, vitu ambavyo vinawezekana kufanywa na wewe vitimize ili kuukata uhusiano hata kama utaku

ANGALIA VYUO VILIVYOFUTWA NA SERIKALI...MUWE MAKINI KABLA YA KUOMBA

Image
SERIKALI kupitia Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi imekunjua makucha yake kwa kutangaza kuvifuta vyuo 10 ambavyo havikusajiliwa na Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) . Naibu Waziri wa wizara hiyo, Philip Mulugo, alitoa kauli hiyo jijini Dar es Salaama mbele ya Kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii na kuongeza kuwa kufutwa kwa vyuo hivyo ni kutokana na kutokufuata utaratibu wa kusajiliwa. Alivitaja vyuo hivyo ni Media and Research Center, Vision Hotel and Tourism College, East Africa College of Hospitality and Tourism, The Africa Institute of Business Management na Aspiration Training Center, vyote vya Dar es Salaam. Vingine ni Dar es Salaam School of Hair Design, Media and Values Training Institute na Information Technology Training Center vya Dar es Salaam. Pia alikitaja Chuo cha Morogoro School of Medical Sciences cha Morogoro. Katika hatua nyingine, Mulugo alikiri kuwa kuna upungufu katika kutoa mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vik

MWAKIFWAMBA, BATULI WAKWAA SKENDO MPYAA

Image
WAKATI mchakato wa Bunge la Katiba ukianza leo mjini Dodoma, ishu hiyo imemtia kwenye tope Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF), Simon Mwakifwamba baada ya kukwaa skendo ya ‘kutoka’ na mwigizaji Yobnesh Yusuph ‘Batuli’ walipotimba mkoani humo. Yobnesh Yusuph ‘Batuli’. Kwa mujibu wa staa wa filamu ambaye aliachwa katika safari hiyo ya kwenda kuhamasisha sanaa itambuliwe kwenye mchakato wa katiba mpya, Mwakifwamba alimteua Batuli ili akajiachie naye Dodoma kwa sababu hakuwa na vigezo. “Akina Monalisa (Yvone-Cherry Ngatikwa) walistahili kwa ukongwe wao kwenye fani, sasa Batuli aliingiaje? Akili za kuambiwa changanya na zako,” alisema msanii huyo. Akizungumzia skendo hiyo, Mwakifwamba alidai kuwa ameshasingiziwa vitu vingi hivyo anajua nyuma yake kuna kundi linalomchafua kila kukicha lakini ukweli ni kwamba hakumteua Batuli kwa lengo hilo. “Sasa kama nimemteua kwa sababu hiyo, je, akina Monalisa nao niliwateua kwa kigezo hicho?” alihoji Mwakifwamba huku akiki

MZUNGU AKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA UWANJA WA NDEGE

Image
Raia wa Henellic, Alexamdrios Atanasios, amekamatwa  maafisa wa usalama wa Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam Jumapili usiku Februari 24, 2014, akiwa na kilo tano za madawa ya kulevya. Kwa mujibu wa duru za kiusalama uwanjani hapo, raia huyo alikamatwa wakati wa upekuzi, akijiandaa kupanda ndege ya Swiss air akielekea mjini Zurich. Kwa mujibu w aduru hizo za usalama, madawa hayo yalikutwa yakiwa yamefichwa kwenye “sakafu” ya begi lake baada ya mitambo ya kisasasa ya upekuzi, kugundua kuwa kulikuwa na ‘mzigo’. Habari zinasema, kwa sasa mtuhumiwa anashikiliwa kwenye kituo cha polisi cha uwanja wa ndege akisubiri taratibu za kisheria ili afungukliwe mashtak

MBONGO ABAKWA MPAKA KUFARIKI NCHINI CHINA ... MAITI YAKE YAKUTWA NA MAAJABU

Image
AMA kweli dunia hadaa, ulimwengu shujaa! Kumeibuka mchezo mchafu, kuna Watanzania wanawachukua warembo nchini na kuwapeleka China kwa ahadi kwamba wanakwenda kufanya kazi saluni, wakifika kule wanawanyang’anya paspoti na kuwauza kwa wanaume (ukahaba), sasa yamemkuta Mbongo aitwaye Sabrina au Habiba, Ijumaa Wikienda lina mkasa wa kusikitisha. Sabrina au Habiba enzi za uhai wake. Habari za uhakika kutoka kwa chanzo chetu nchini humo zilisema kuwa, Sabrina (24), alifariki dunia Alhamisi iliyopita kufuatia kubakwa na wanaume watano, raia wa Nigeria ambao wamo nchini humo kibiashara. Tukio hilo lilijiri kwenye hoteli moja iliyopo kwenye Mji wa Guangzhou ambao umejaa wageni wengi, wakiwemo Watanzania. SIKU YA TUKIO Rafiki wa karibu wa Sabrina, Saada alisema siku ya tukio, marehemu akiwa katika harakati zake za kutafuta wateja alikutana na Mnigeria mmoja ambaye walipatana kulala wote kwa usiku mzima. “Kumbe yule Mnaigeria alikuwa na wenzake wanne. Usiku walimwingilia

MAGAZETI YA LEO JUMANNE TAREHE 25.02.2014

Image
MAGAZETI YA MICHEZO NA BURUDANI MAGAZETI YA UDAKU LEO