Posts

Showing posts from November 8, 2016

Wezi Watokomea na Mashine ya ATM Ikiwa na Pesa

Image
NAIROBI: Polisi jijini Nairobi nchini Kenya wamemkamata mlinzi wa Benki ya Equity kuhusiana na tukio la wizi lililotokea Jumamosi iliyopita ambapo watu wanaoaminika kuwa ni wezi waliiba mashine ya kielektroniki ya kutolea pesa, Automatic Teller Machine (ATM) pamoja na pesa taslim ambazo hazijafahamika kiasi chake. Wezi hao walichimba ukuta wa nyuma wa Benki hiyo na kutoweka na sanduku la uhifadhi wa pesa pamoja na mtambo wa ATM, pesa zikiwa ndani. Wakati wakitekeleza tukio hilo, washukiwa waliweza kuzima kamera za CCTV na pia kengele ya usalama kabla ya kutekeleza adhma yao ya kuiba mashine na pesa hizo. Akizungumza na wanahabari, Kamanda wa Polisi wa Jimbo la Nairobi, Japheth Koome amesema kwamba polisi waliweza kupata mitungi ya gesi na vifaa vingine ambavyo hutumuka kukata chuma. Alipoulizwa kama wezi siku hizi wamepata maarifa na mbinu nyingi kama wacheza filamu, alisema kwamba kwa siku za hivi karibuni matukio ya wizi kwenye mabenki yanazidi kuongezeka na

SAKATA LA DIVA NA JOKATE KIDOTI KWA ALI KIBA,MAPYA YAIBUKA,GIGY MONEY AFUNGUKA

Image
Mwanadada Diva aliweza ku tweet kuhusiana na uwezo wa alikiba katika kuimba na kumalizia kuwa “Girlfriend anakutia gundu” kitu ambacho wengi walijiuliza inamaana Jokate (Kama inavyo julikana kuwa ndiye wa Kiba) kuwa anamtia gundu? Leo Mrembo Gigy_Money amejitokeaza na kupost picha hii hapa chini na kuandika maneno ya kumtetea Jokate: "Honestly jojo wangu mtoto classic uyu 😍wache waseme unagundu ila mwisho wa siku watakuelewa tu kwa mafanikio yako hadi unafikia umri wao yani we utakua Michael Jackson wa kike unajituma mwaya #USIFORCETUFANANE #HATUFANANI" Gigy Mone y