Posts

Showing posts from April 9, 2015

8 Certain Signs You’re With the Man You Should Marrys

Image
Hello my Dear Friends You’ve survived a long-distance relationship This is great challenge for any couple. You love each other very much and believe everything is possible. You both are ready for necessary sacrifices, knowing everything will be ok when you get back together.Are you dating the right guy? It’s hard to tell, especially when you’re stuck in relationships and don’t know what you want from your man. What are you looking for in your partner? Does he want to be with you forever and ever? Most women can’t find the right answers. But there are some tricks to tell if you’re ready to marry a certain guy. Here is a list of qualities that you should pay attention on. These signs will help you to find out if you two are bound for life.   1. He’s a good teammate Fighting for something together is always good than fighting with each other. You both can improve and inspire each other achieving your dreams. If you are a good team – be sure, he will be there for you when

ANASWA AKIIBA MAHINDI;APEWA ADHABU YA KULA YOTE MABICHI!

Image
Akilazimishwa kula mahindi hayo. Jamaa ambaye jina halikuweza kupatikana mara moja, amejikuta akionja joto ya jiwe baada ya kudaiwa kukutwa akiiba kwenye shamba la mahindi hivyo kulazimishwa kula mahindi mabichi.Tukio hilo la aina yake lilijiri hivi karibuni kwenye Kata ya Miembeni, Bukoba mkoani Kagera na kuibua gumzo kubwa. Kwa mujibu wa shuhuda wetu, baada ya kumnasa kijana huyo akiiba mahindi aliyoyajaza kwenye gunia, wamiliki wa shamba hilo walimuamuru kukaa chini na kuyala yakiwa mabichi hadi yaishe, kitendo ambacho jamaa huyo alikubaliana nacho. Akila maindi hayo ili kuepuka kichapo. Ilielezwa kwamba, katika hali ya kushangaza, kijana huyo hakukataa wala kuonesha kutetereka kwani alianza kuyala hadi alipoamriwa kuacha na kuambiwa aondoke.Katika habari hiyo iliyoripotiwa na Mtandao wa Harakati, kijana huyo alionekana kuwa na matatizo ya kutosikia vizuri wala kuongea kwa maana ya kuwa ni ‘bubu’. Hata hivyo, kijana huyo hakujulikana alitokea wapi k

WAZIRI STEVEN WASIRA AWAFUKUZA WAKURUGENZI WATATU KWA KUISABABISHIA SERIKALI HASARA YA BILLION 2.5

Image
WAZIRI wa kilimo, Chakula na Ushirika Steven Wasira amewafukuza kazi wakurugenzi watendaji watatu wa Mamlaka ya Kuendeleza Bonde la Mto Rufiji (Yaani Rufiji River Basin Development Authority – RUBADA) kutokana na matumizi mabaya ya ofisi ya Umma ambayo yameitia hasara ya Bilioni 2.5 Serikali . Akitoa agizo hilo leo mbele ya Waandishi wa Habari, Waziri Wasira amewataja Watendaji hao kuwa ni Bwana Aloyce L. Masanja – Kaimu Mkurugenzi Mkuu; Bibi Tabu Ndatulu – Mkurugenzi wa Mipango na Uwekezaji; na Bwana Filozi John Mayayi – Mkurugenzi wa Fedha na Utawala. Wassira amesema baada ya Ofisi yake kupata malalamiko kutoka kwa wananchi wa vijiji vya Rufiji pamoja na wawekezaji juu ya Urasimu wa shirika hilo, aliunda timu ya Uchunguzi kutoka wizara ya Kilimo na Hazina kwenda kuchunguza malalamiko hayo. “Baada ya kuunda tume kutoka hapa Wizarani ikishirkiana na Hazina, walienda kwenye shirika hilo kufanya ukaguzi.Tume ilibaini kwamba mfumo wa pale ulikuwa ni

MTABIRI ABAINI MAMBO MAZITO KWENYE MAISHA YA JAY DEE

Image
  Kwa Lady Jaydee, mwaka 2015 utakuwa wenye mafanikio makubwa, ndoa mpya, stress kiasi na magonjwa lukuki, kwa mujibu wa mtabiri! Mtabiri huyo alialikwa na Lady Jaydee kwenye kipindi chake, Diary ya Lady Jaydee ambapo alidai kuwa mwaka huu muimbaji huyo atapata pesa nyingi kupitia muziki wake lakini kiafya akitabiriwa homa nyingi na kukifiria kifo mara kwa mara. “Kuna vitu vitaisha mwaka huu ambavyo itabidi uache,” mtabiri huyo alimweleza Jide. “KAwanza hii ni possibility you need to avoid, kuna wakati hali ya kifo itakupa stress sana, unaweza ukasema maisha yangu yatakuaje? “Usifikirie hivyo, utakuwa unafikiria kifo, utafikiria baada ya kifo nini kinaendelea, utakuwa unafikiria siku nikifa nitaenda peponi au nitaenda motoni, kwahiyo kifo kitakuja kwako lakini usifikirie, kwamba ukiumwa tu kidogo haa nitakufa, no hufi, because ningeona kifo kwenye utabiri wako wa mwaka 2015! Mwaka huu utaumwa kidogo, utaumwa magonjwa, afya yako itakuwa weak sana, kama ungeolewa ingek

BAADA YA UNYAMA ALIOFANYIWA AFRIKA KUSINI:TAVES MASHAUZI AAMUA KUFANYA DUA NYUMBANI KWAKE

Image
Jumanne Hassan ‘Tevez’ akiweka ubani wakati wa dua hiyo. MUME wa ‘long time’ wa mwimbaji nyota wa kike wa muziki wa Taarab nchini, lsha Ramadhan ‘Mashauzi’, Jumanne Hassan ‘Tevez’ ambaye hivi karibuni alitekwa na kuteswa na watu wasiofahamika nchini Afrika Kusini, amerejea nchini na kufanya dua ya kumshukuru Mungu kwa kumnusuru kifo katika tukio hilo. Tevez aliwakusanya ndugu, jamaa na marafiki na kufanya dua hiyo, Ijumaa iliyopita nyumbani kwao Msamvu, Madawa jirani na Shule ya Msingi Msamvu ‘A’ ambapo alifanya kisomo hicho kilichoambatana na dua na chakula. “Mungu amemnusuru na balaa lile, amemkingia hivyo ameona ni vyema aandae dua ya kumshukuru,” alisikika mmoja wa waalikwa.Baadhi ya mashehe na waumini wengine wa Kiislamu waliohudhuria dua hiyo walimpongeza Tevez kwa kitendo hicho cha kumkumbuka Mungu na kumshukuru kwa kumlinda na majanga yaliyomkuta. Watu waliohudhulia dua hiyo. “Hili ni jambo jema sana alilofanya Tevez ambapo tunaelekezwa na mitume wetu kwamba

ROSE NA SHETTA WADAIWA KULALA CHUMBA KIMOJA MORO!

Image
MUSA MATEJA KIMESANUKA! Mkali wa muziki wa kizazi kipya nchini, Nurdin Bilal maarufu kama Shetta anadaiwa kulala chumba kimoja na staa wa filamu Bongo, Rose Ndauka katika hoteli iitwayo Kingway iliyoko mkoani Morogoro mwishoni mwa wiki iliyopita. Staa wa filamu Bongo, Rose. Chanzo makini kinachofahamu kwa undani kinachoendelea baina ya mastaa hao wawili, kimelidokeza gazeti hili kuwa tukio hilo lilijiri wakati wakielekea katika shughuli za mazishi ya muasisi wa Kundi la Tip Top Connection, Abdul Bonge aliyezikwa kijijini kwao Mkuyuni mkoani humo, ambako watu wengi maarufu walihudhuria. “Si unajua mastaa kibao walikuwepo kwenye ule msiba, basi Rose na Shetta nao walikuwepo na wakati wa kwenda Mkuyuni, walipanda gari la Shetta hadi Morogoro mjini ambako walichukua chumba na kulala wote hadi kesho yake walipohudhuria mazishi na kurejea Dar es Salaam,” kilisema chanzo hicho. Ili kushibisha maelezo yake, mtoa habari huyo alilitumia gazeti hili video ya wawili hao wakiwa n

WEMA SEPETU BADO DIAMOND KAMKALIA MOYONI!

Image
Staa mrembo kutoka Bongo Movies, Wema Sepetu pamoja na kutengena na mpenzi wake Nassib Abdul ‘Diamond’ lakini alipoamua kutaja wasanii wanaofanya vizuri katika muziki wa Bongo Fleva mtaliki wake huyo kampa namba moja katika wasanii watano ambao yeye anaona wanafanya vizuri katika muziki.“Muziki umeshika kasi na kuna wasanii ambao wanafanya vinzuri kuliko wengine, kwangu Top 5 yangu 1 Nassib, wa pili ni Ashley, Ali kiba, Barnaba na wa tano ni mirrow hawa ni wasanii wanzuri wapo level za kimataifa,”anasema Wema. Aidha Wema amesema kwa upande wa wasanii wa kike anampenda sana mwimbaji Vanessa Mdee kwani anaimba na kucheza katika kiwango cha juu na kumfanya awe ni mpenzi wa kazi za msanii huyo, pia anataka watu wasimuelewe vibaya ni kwa mujibu wa mapenzi yake na maono yake