Posts

Showing posts from June 11, 2015

SOMA BAJETI YA MWAKA 2015/16 ILIYOWASILISHWA NA WAZIRI WA FEDHA BUNGENI LEO

Image
Waziri wa Fedha, Mhe. Saada Salum Mkuya (MB) akiwasilisha bungeni Bajeti Kuu ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2015/16, Mjini Dodoma leo. Waziri wa Fedha, Mhe. Saada Salum Mkuya (Mb) akionyesha Begi la Bajeti Kuu ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2015/16 wakati anawasili katika Viwanja vya Bunge, Mjini Dodoma leo. SOMA BAJETI YA MWAKA 2015/16 HAPA===>>> BAJETI

MAKAMBA AVUNJA REKODI YA MAPOKEZI NA UDHAMINI IRINGA

Image
Wanafunzi wa Iringa University wakimpokea Mhe. Makamba kwa shangwe na furaha huku wakiwa wameshika mabango Mbunge wa Bumbuli na Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia anayeendelea kusaka udhamini wa wananchama wenzake  ili kuingia katika kinyang’anyiro cha Urais mapema Oktoba mwaka huu, Mheshimiwa January Makamba, leo amepokelewa kwa kishindo na wanachama wa CCM Mjini Iringa na kuvunja rekodi ya udhamini ukilinganisha na wagombea waliopita. Akiongea kabla ya kumkaribisha mtangaza nia huyo anayeonekana kuwa na mvuto wa aina yake kwa vijana, Katibu wa CCM wilaya ya Iringa Zongo Lobe Zongo amemtaja Mheshimiwa Makamba kuwa ni mgombea aliyevunja rekodi mkoani hapo baada ya kupata wadhamini 680 ukiachilia mbali mapokezi yenye msisimko mkubwa tofauti na wagombea waliotangulia. Akiwashukuru Mheshimiwa January Makamba, ambaye anaomba kupendekezwa na chama chake kugombea nafasi ya urais, alisema kwamba ameamua kugombea si kwa kubip bali anagombea kushinda, pia kwamba

TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI YATOA RATIBA KAMILI YA UANDIKISHAJI KWA MIKOA 15

Image

MTITU, STEVE NYERERE BIFU KALI WAAPA KUTOZIKANA!

Image
Msanii wa filamu Steven Mengere ‘Steve Nyerere’. Wakizungumza na Amani kwa nyakati tofauti juzi, wawili hao wameapa wasijuane kwa hali yoyote iwe kwa matatizo kama mmoja wao kufiwa au yeye kufariki dunia, basi mwingine asihudhurie msiba na mazishi. WASANII William Mtitu na Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ wamejiapiza kuwa wasizikane ikitokea mmoja kati yao akafariki dunia huku chanzo ni kila mmoja kumtuhumu mwenzake kwa unafiki. Steve Nyerere, ndiye alikuwa wa kwanza ‘kuachama’ mbele ya gazeti hili ndani ya Viwanja vya Leaders, Dar kulikokuwa na kikao cha maandalizi ya sherehe ya harusi ya msanii mwenzao, Hadji Adam ‘Baba Haji’. “Hakuna mtu mnafiki kama Mtitu, sitaki kabisa hata kumsikia na kila nikimtazama najisikia vibaya mno, mkiwa pamoja anaonekana mwema lakini baada ya hapo anakuwa msaliti, kwanza hata nikifiwa sitaki kumuona msibani, nikifa mimi hakika asihudhurie mazishi yangu, naapa,” alisema Nyerere huku akimtazama mwandishi kwa jicho la ‘sitanii kaka’. Naye kwa u

TWO INMATES MADE A DARING AND CINEMATIC ESCAPE OVER THE WEEKEND FROM CLINTON CORRECTIONAL FACILITY

Image
Two inmates made a daring and cinematic escape over the weekend from Clinton Correctional Facility, the upstate prison known as “Little Siberia,” somehow obtaining the power tools necessary to carve their way out of their steel cells and into a large pipe leading to a street outside. The account below is based on statements from the New York State governor’s office and police officials. First, the inmates cut neat rectangular holes in the steel at the backs of their cells. They fashioned dummies from sweatshirts and stuffed their beds to thwart discovery during regular cell checks by guards. The inmates, both serving long terms for vicious murders, had adjoining cells. The rectangular holes can be seen in both walls from the catwalk behind the cells. Once inside the mechanical corridors of the prison, the men broke through a brick wall, made their way to a 24-inch drain pipe and cut a hole in it. They left a taunting note for the authorities that included a racist ca

MANGULA ATAJA VIGEZO 13 VYA MGOMBEA URAIS WA CCM..NI HIVI HAPA

Image
MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Philip Mangula amesema vigezo 13, vitatumika kuwachuja wanachama wa chama hicho ambao wameomba kugombea urais CCM. Alisema hayo jana mjini hapa wakati wa mkutano wake na waandishi wa habari kwenye makao makuu ya CCM mjini Dodoma. Aliwakumbusha watangaza nia kuwa hawaruhusiwi kutoa rushwa, kushawishi au kushawishika kuwapa rushwa wale wanaowadhamini. Vigezo vyenyewe Alitaja vigezo 13 vitakavyotumika kuwachuja wagombea kuwa ni uwezo mkubwa na uzoefu katika uongozi, uadilifu, unyenyekevu na busara. Pia, kuwa na elimu ya chuo kikuu au inayolingana na hiyo, mtu mwenye upeo mkubwa wa kuimarisha na kuendeleza Muungano, umoja na amani. “Anatakiwa kuwa na upeo mkubwa usiotiliwa mashaka kuhusu masuala ya kimataifa, asiye na hulka ya kidikteta au mfashisti, awe tayari kulinda kanuni, sheria na utawala bora,” alisema Mangula. Alitaja vigezo vingine ni kuwa mtetezi wa wanyonge na haki za bin

TAZAMA HAMISA MOBETO AKIWA KWENYE UBORA WAKE BAADA YA KUJIFUNGUA HIVI KARIBUNI.. HUWEZI KUAMINI ALIVYOKUWA MCHARO

Image
WEKA MAONI YAKO HAPA

JOHARI: RAY NI KILA KITU KWANGU!

Image
Diva wa filamu Bongo, Blandina Chagula ‘Johari’. PATAMU hapo! Diva wa filamu Bongo, Blandina Chagula ‘Johari’ amesema msanii mwenzake, Vincent Kigosi ‘Ray’ ndiye kila kitu maishani mwake kutokana na msaada aliompa wa kumtoa kisanii na kumsapoti kwa mambo mengi kikazi. ‘Akianika mwanya’ katika mazungumzo na Amani juzikati, Johari alisema haoni sababu ya kuficha ukweli kuwa bila Ray isingekuwa rahisi yeye kufika alipo kisanii hivyo lazima akumbuke kurudisha shukrani. Vincent Kigosi ‘Ray’. “Lazima niwe mkweli kuwa, Ray ni kila kitu kwangu, nipo hapa nilipo leo kwa sababu ya jitihada zake. Alikuwa mwalimu wangu wa sanaa tangu Kaole (kundi la sanaa), siyo mimi tu hata marehemu Kanumba (Steven) na wengine, hivyo siwezi kuacha kumrudishia shukrani zangu,” aliweka nukta Johari.

MR NICE AMWANDIKIA BARUA YA WAZI RAIS WA BURUNDI, PIERRE NKURUNZIZA..ISOME TU UMPE NA WEWE USHAURI

Image
Mr Nice amechukizwa na hatua za rais wa Burundi, Pierre Nkurunziza ya kutangaza nia ya kuombea urais kwa awamu ya tatu kinyume na katiba hali ambayo imesababisha machafuko. Kupitia ukurasa wa Facebook, Mr Nice ameandika: NI MAONI BINAFSI TU WALA SIJASHAURIWA NA YOYOTE…Pierre wewe ni kaka yangu ki -umri,,,,,ki -elimu huenda na kii -,,,,tejilinsia pia …. ukiwa kama mzaliwa na damu ya mburundi toka ktk kabila lolote lile ama dini ama jinsia yoyote pale burundi nakuomba sana hebu jaribu kuona uchungu na masononeko ya watu wako walioamini kuwa wewe ndiye mkombozi wao toka ktk lindi la machafuko na umwagaji damu uliotukuka duniani…usiwakumbushie tena kule ulikowatoa na sasa unataka kuwarejesha tena huko ..kama nchi yako umeiweka vizuri hadi hapo ilipo kaka kwanini usipewe sifa za uliyoyafanya baada ya machafuko ya damu za watu muda mrefu na nchi yako kuwa na amani..ningeoenda nikuone ukiishi kwa amani na heshma iliyotukuka kama waliotangulia……nchi c y