MR NICE AMWANDIKIA BARUA YA WAZI RAIS WA BURUNDI, PIERRE NKURUNZIZA..ISOME TU UMPE NA WEWE USHAURI



Mr Nice amechukizwa na hatua za rais wa Burundi, Pierre Nkurunziza ya kutangaza nia ya kuombea urais kwa awamu ya tatu kinyume na katiba hali ambayo imesababisha machafuko.

Kupitia ukurasa wa Facebook, Mr Nice ameandika:

NI MAONI BINAFSI TU WALA SIJASHAURIWA NA YOYOTE…Pierre wewe ni kaka yangu ki -umri,,,,,ki -elimu huenda na kii -,,,,tejilinsia pia …. ukiwa kama mzaliwa na damu ya mburundi toka ktk kabila lolote lile ama dini ama jinsia yoyote pale burundi nakuomba sana hebu jaribu kuona uchungu na masononeko ya watu wako walioamini kuwa wewe ndiye mkombozi wao toka ktk lindi la machafuko na umwagaji damu uliotukuka duniani…usiwakumbushie tena kule ulikowatoa na sasa unataka kuwarejesha tena huko ..kama nchi yako umeiweka vizuri hadi hapo ilipo kaka kwanini usipewe sifa za uliyoyafanya baada ya machafuko ya damu za watu muda mrefu na nchi yako kuwa na amani..ningeoenda nikuone ukiishi kwa amani na heshma iliyotukuka kama waliotangulia……nchi c yako ni ya watu wote na hakuna aliyemilikishwa ardhi ya dunia hii sii muhammad wala yesu …hii ni mali ya mwenyezi mungu tu sisi tunafanya peana na kuachiana madaraka ya ardhi hii ….mbona hakupewa yesu ama muhammad s.a iwe yakeee ? ..walichopewa ni kuisemea na kuiwakilisha kwa uaminifu waliopewa na alllah…cc wote tunamuomba mungu ….je unataka kuniambia kuwa wewe nkurunzinza haumuombi mungu ?????…uongozi ni vitu vya kupita tu na wala havina mamlaka kwa muumbaa….mimi ni mtanzania lakini sioni utanzania wenye amani bila east africa iliyo salama…(1) je unadhani kwa yanayoyokea east frican community unakuelewa na kukupa supporty au kuwa upande wako..???….(2)hivi unajua kama umeanzisha ukimbizi ambao tulikuwa tumeusahau na tukiwa ktk hatua za mwisho wa kutokomeza makovu yakeeee..?….(3) je umejaribu kujipima na kuona kama unafaa kuendelea kuwa kiongozi ktk kipindi hikiii…?(4) huoni kama unawatesa ndugu zako ambao ni damu yakooooooo…(5) je huguswi na misitisho ya misaada ambayo imekatwa mpaka sasa kutoka nchi wahisani ambao ndio lisho la taifa lako kwa ajili ya wewe mtu mmoja tuuuu kungangania madaraka ambayo wananchi hawataki tena….?????.(6) je unafurahia ICC kuanza kutoa matamko yake juu yako kama waliotanguliaaa?(7) je unataka kina MR NICE tuogope kuja bujaa(bujumbura na viunga vyake)) …. ………niitangazie duni kwa haya niliyosema kuwa nimeyatoa moyoni mwangu na nimeandika haya kwa mkono wangu.naumizwa na yanayotokea kwa wenzetu saaana maana ni ndugu zetu, NKURUNZINZA PIMA IMANI YAKO KWA WATU WAKO …mambo ya kijeshi yalishapitwa na wakati katika tawala zetu za kiafrica… kama mlielewana kugawana madaraka gawana sasaaaaaaaaa usinganganie ..iga mfano wa wenzio .kila chenye mwanzo hakikosi mwisho bro .. BURUNDI PEACE FOREVER …mungu tusaidie africa tunaisha kila dakika atabakia naniii…??????????

Bongo5

Comments

Popular posts from this blog