JOHARI: RAY NI KILA KITU KWANGU!

Diva wa filamu Bongo, Blandina Chagula ‘Johari’.
PATAMU hapo! Diva wa filamu Bongo, Blandina Chagula ‘Johari’ amesema msanii mwenzake, Vincent Kigosi ‘Ray’ ndiye kila kitu maishani mwake kutokana na msaada aliompa wa kumtoa kisanii na kumsapoti kwa mambo mengi kikazi.
‘Akianika mwanya’ katika mazungumzo na Amani juzikati, Johari alisema haoni sababu ya kuficha ukweli kuwa bila Ray isingekuwa rahisi yeye kufika alipo kisanii hivyo lazima akumbuke kurudisha shukrani.

Vincent Kigosi ‘Ray’. “Lazima niwe mkweli kuwa, Ray ni kila kitu kwangu, nipo hapa nilipo leo kwa sababu ya jitihada zake. Alikuwa mwalimu wangu wa sanaa tangu Kaole (kundi la sanaa), siyo mimi tu hata marehemu Kanumba (Steven) na wengine, hivyo siwezi kuacha kumrudishia shukrani zangu,” aliweka nukta Johari.

Comments

Popular posts from this blog