Posts

HAWA NDIO BAADHI YA MASTAR WA BONGO WALIOJITOKEZA KWENYE MSIBA WA BABA WA SUPER STAR WEMA SEPETU!!

Image
Mastaa na marafiki wa karibu na Muigizaji Wema Sepetu wamejitokeza kwa wingi katika hali ya Kumfariji kutokana na kufiwa na baba yake mzazi Balozi ISAAC ABRAHAM SEPETU aliyefariki jana kwa maradhi ya Kupooza aliyougua kwa Muda Mrefu. Msiba upo sinza Mori Nyumbani Kwa Familia Ya Marehemu na marehemu anatarajia kusafirishwa kesho kwa mazishi huko Zanzibar Mjane wa marehemu Mama yake Wema Sepetu wa katikati kabisa Wema Sepetu wa kushoto akiwa na waombolezaji wengine Tunu Sepetu Mtoto wa marehemu wakati kati kabisa Kutoka Kushoto ni Msanii ElizaBeth Michael (Lulu) akifuatiwa na mama wa Msanii Marehemu Kanumba Msanii wa Maigizo Kajala pia yupo msibani Junaithar Pemba na Director Johanna marafiki wa karibu na Wema Sepetu

DINI MPYAAAA YAIBUKA ... IFAHAMU KWA KINA HABARI ZAKE ...

Image
Dini inayoamini katika MUNGU lakini ikiruhusu yale ambayo dini zingine zinapinga imeanzishwa eneo la mji mdogo wa Makongolosi wilayani Chunya mkoani Mbeya, Dini hiyo haiamini katika kutoa sadaka bali inasema tunamtolea nani sadaka wakati Vitu vyote tulivyonavyo ni mali ya MUNGU,kwa nini tunampa MUNGU mali zake Mwnyewe.! Dini hiyo inaruhusu ulevi,uchawi na uzinzi kwa sababu vimeumbwa na MUNGU,Vile vile inaamini hakuna dhambi duniani,Dini hiyo inaitwa DIMAYO, sasa imeanza kuenezwa Mbeya ========================= Ufafanuzi ========================= By GAMBISHI DWESE Yawezekana kweli Bwana Domy umekutana nami. Mimi Ndiyo PAPA-DIMAYO 1: GAMBISHI DWESE,( nabii wa kwanza wa DIMAYO) hata hivyo pengine umeninukuu kimakosa.Kwanza kabisa Dimayo haiamini katika uwepo wa mungu muumbaji aliye hai wala aliyekufa anayedaiwa kuhusika na kila kinachoendelea ulimwenguni. Na nimeshatoa kitabu kinachoitwa HAKIKA HAKUNA MUNGU MUUMBAJI ALIYE HAI WALA ALIYEKUFA anayehusika na kila kinachoende

CHANZO CHA NDOA YA BOB JUNIOR KUVUNJIKA KISA NI HUYU MREMBO....

Image
Ashely Toto in German Hapa Bob Junior Akiwa Mombasa na Ashley Toto hivi Karibuni Hapa Bob Junior Akiwa Ujerumani na Dada Ashley Toto Wakila Raha Ujerumani Frankfurt Wakiwa Ujerumani Mall Wakifanya Shopping Ashley Toto Ni Msanii wa movies kutoka Kenya ambae makazi yake ni Ujerumani ila kwa sasa yupo Mombasi kwa mapumziko ..Mnyetishaji wa habari ametuhabarisha kuwa wawili hawa wapo mapenzini kwa muda mrefu sana hata alipokuwa Ujerumani Bob Junior huwa anaenda huko kama baadhi ya picha zinavyoosha ..Pia inasemekana kuwa baada ya Mwana Dada huyu kuja Mombasa kwa mapumziko Bob Junior alienda Matembezi huko na Kukaa kwa muda wa week moja akiwa nae na baadae Mwana dada huyo Mrembo alimtafutia Show mbili Huko Mombasa ...Inasemekana ndio Sababu mojawapo ya mke wake kuona wivu wa mapenzi na kuamua kuachana na Bob junior.. -Mdau

Mchina aukata uume wake baada ya kutoswa na demu wake ampendaye

Image
Mwanaume mmoja wa Jiaxing, China amejikuta akichukua uamuzi mgumu wa kujikata uume wake baada ya nyota yake ya bahati katika mapenzi kushindwa kung’aa katika anga la maisha yake, kiasi cha kumfanya akate tamaa na kuamua kuchukua uamuzi huo. Baada ya kujikata kiungo hicho muhimu katika mwili wa mwanaume, mchina huyo Yang Hu mwenye miaka 26 aligundua kwamba haikuwa ndoto ni kweli ameukataa uume wake, ndipo alipochukua baiskeli yake na kukimbia hospitali kwa matarajio ya kwenda kuunganishiwa kiungo chake alichokikata mwenyewe. Sipati picha aliwezaje kunyonga ‘pedal’ za baiskeli yake mpaka hospitali ilihali maumivu makali aliyokuwa nayo, lakini mbaya zaidi kutokana na kuchanganyikiwa kwa alichokifanya, baada ya kufika hospitali ndipo ndoto zake zikazidi kufifia baada ya madakrati kumueleza kuwa amesahau kuja na kiungo hicho ili kirudishiwe sehemu yake. Hu alinyonga baiskeli yake tena kwa haraka kurudi nyumbani kuuchukua uume wake aliousahau na

BREAKINGS NEWZ"Mwanga adondoka huko Msata-Chalinze Asbh hii".

Image
mtu mmoja ambaye hajafamika kwa jina lake haraka leo asubuhi ameanguka kwenye bati uko maeneo ya msata -chalinze, ambaye alionekana na vitu kama pembe yenye hirizi na kujulikana ni mwanga, tutakuletea habari zaidi juu ya hili baadae, KWA HABARI ZAIDI USISAHAU KULIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK/TWITTER

Saini zaanza kukusanywa ili kumng'oa Spika Anne Makinda kwa madai kwamba amekuwa akikiuka kanuni za bunge

Image
Mbunge wa Nzega, Dk Khamis Kigwangalla, (CCM), leo anatarajiwa kuanza kukusanya saini za wabunge akitafuta kuungwa mkono katika hoja ya kutokuwa na imani na Spika wa Bunge, Anne Makinda kwa madai kwamba amekuwa akikiuka kanuni za Bunge. Dk Kigwangalla aliibua hoja ya kutokuwa na imani na Spika katika kikao cha wabunge wote cha kuelezea shughuli zitakazofanywa na Bunge katika mkutano wa 13, kilichofanyika juzi jioni kwenye ukumbi wa Pius Msekwa. Mbunge huyo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, jana alithibitisha kuwapo kwa mjadala huo katika kikao cha wabunge, lakini hakuwa tayari kueleza kwa undani na badala yake alisema kwamba leo ataanza kukusanya saini za wabunge kwa ajili ya kukamilisha hoja ya kutokuwa na imani na Spika Makinda. Chanzo chetu kutoka katika kikao hicho cha wabunge kilibainisha kuwa Kigwangalla alihoji kuhusiana na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Bajeti, Andrew Chenge (CCM-Bar

Mama Yangu!! Uvumilivu wamshinda Irene Uwoya! Alichokiandika hapa watoto chini ya miaka 18 msisome!

Image
“...Wale ma- (Tusi linalohusisha kiungo cha mwili) wanao post (Tusi kama la hapo mwanzo) humu...waaandike watakavyo...sio (Tusi- vitendo vibaya kwenye jamii) tuuu yan na vza yakuzunguka dunia nzima....siitaj watu ma- (Tusi kali sana) ...kama na kuboa kafe mbele....eti range nimehongwa mtasubiri sanaaaa....sina mdaa huo sinaaa...wakukaa pemben na kumsmanga mtuuuu...wote mnao ni disss ma- (Tusi la kumalizia sentensi)... ” Hayo ni maneno ya mwadada Irene Uwoya aliyoaandika usiku wa leo hii kupitia ukurasa wake wa mtandao mmoja wa kijamii. Tulipoyasoma tuu, tulishtushwa sana kwani si kawaida kwa mwanadada huyu kuandika maneno mzito kama haya na ndipo tulipoamua kufanya utafiti yakinifu ili tujue why??? Na haya ndo majibu ya uchunguzi wetu huu… Tujikumbushe Historia fupi Hivi majuzi mwadada Irene Uwoya alipost kwenye mtandao picha za gari yake mpya aina ya Range Rover na ndipo watu wengi walianza ku-comment na “kumponda” mwanadada huyu kuwa sio yake bali kahongwa na wanaume “

Rushwa ya ngono kwa boss wake yamponza Baby Madaha baada ya wanakundi kuanza kumtenga

Image
Mwanamuziki na mwigizaji Bongo, Baby Joseph Madaha ‘Baby Madaha’, amemshukia mwanamuziki memba mwenzake wa Candy n’ Candy, Top C na kumtaka asimuingilie katika maisha yake. Kupitia kipindi cha redio hivi karibuni, Top C alisema tangu Baby Madaha asajiliwe katika kampuni hiyo ya muziki iliyopo nchini Kenya, memba wengine wamekuwa wakipuuzwa na bosi wao, Joe Kairuki kiasi kwamba hawasikiki kabisa na kuainisha kuwa Baby anatamba kwa sababu amekuwa ‘kiburudisho’ cha bosi huyo. Alipoulizwa kuhusiana na tuhuma hizo, Baby alikanusha: “Top C na wenzake ni wazushi, sina uhusiano na Joe. Mimi nina kipaji kikubwa na nina nidhamu ya kazi kuliko wao ndiyo maana ninapewa nafasi. Wanaendekeza uzushi kwa nini wasipigwe chini?” JE, UNA MAONI GANI KATIKA HILI? KWA KUPATA HABARI ZAIDI LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK/TWITTER

Ray C na Nora watwangana ngumi studio wakimgombania producer

Image
KATIKA hali ya kushangaza, siku chache baada ya kuripotiwa kupona na kuacha matumizi ya madawa ya kulevya, mwanamuziki Rehema Chalamila ‘Ray C’ anadaiwa kugeuka mwanamasumbwi na kumpa kipigo mwigizaji Nuru Nassoro ‘Nora’.. Kwa mujibu wa shuhuda wetu, tukio hilo lilijiri wiki iliyopita ndani ya studio moja ya kurekodia muziki iliyopo Kinondoni, Dar ambapo wawili hao walikutana walipokwenda kurekodi ngoma zao. Ilidaiwa kuwa akiwa studio hapo, Nora alikutana na Ray C ambaye pia alizama mahali hapo bila mawasiliano na prodyuza anayemtengenezea ngoma mpya. Chanzo hicho kilipasha kuwa baada ya Ray C kuingia studio hapo alimkuta prodyuza huyo akiandaa ngoma ya Nora ambapo alihoji kilichompeleka mwigizaji huyo mahali hapo. Ilidaiwa kuwa prodyuza huyo ambaye jina halikupatikana alimwambia Ray C kuwa Nora alifika kurekodi wimbo wake. Ilisemekana kuwa Ray C hakuridhishwa na majibu hayo, akaomba asikilizishwe ngoma hiyo ya Nora lakini baada ya kusikiliza ilidaiwa k

DIAMOND PLATNUMZ NAYE AHUDHULIA MAZISHI YA BABA YAKE NA WEMA SEPETU HUKO ZANZIBAR

Image
Ujumbe huo hapo chini unajitosheleza pita ukisoma japo kimya kimya...... Babu Tale, Zamardi na Diamond ndani ya Zanzibar kwaajili ya mazishi ya Balozi Sepetu Habari ndo hiyo kwa wazushi. Well done Prezident wa Wasafi na leo naona ametokelezea ki Al Haj zaidi. TUPE MAONI YAKO, NA USISAHAU KULIKE WETU WA FACEBOOK

Kapten Komba ajitoa mhanga:...Adai kuwa Lowassa ndo Rais mteule wa watanzania- 2015 baada ya Kikwete

Image
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Kapteni Mstaafu, John Komba amevunja ukimya na kutamka wazi kuwa Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, ndiye chaguo lake na atakuwa Rais ajaye uchaguzi wa 2015. Komba anakuwa mtu wa pili kumtaja Lowassa hadharani kuwa anafaa kuwa rais 2015. Itakumbukwa Mbunge wa Viti Maalumu, Beatrice Shelukindo (CCM) naye alivunja ukimya baada ya kutangaza kumuunga mkono Lowassa kumrithi Rais Kikwete. Shelukindo alitoa kauli hiyo wakati akiwasalimia wakazi wa Monduli baada ya kukaribishwa kuchangia ujenzi wa Hosteli ya KKKT, kwenye sherehe za kukaribisha Mwaka Mpya zilizofanyika nyumbani kwa Lowassa na kuhudhuriwa na makada kadhaa wa CCM. Akizungumza na Mwananchi katika mahojiano maalumu jana, Komba ambaye ni Kiongozi wa Kundi la Uhamasishaji cha CCM Tanzania One Theatre (TOT Plus), alisema mtazamo wake kwa mtu anayefaa kumrithi Rais Jakaya Kikwete ni Lowassa. Komba aliyeingia kwenye siasa kutokana na msukumo

Baba adaiwa kuwabaka na kuwalawiti binti zake wawili wa miaka 10 na 13 huko Marangu Moshi

Image
Baba mzazi wa mabinti wawili mkazi wa Kijiji cha Kiria Kata ya Mamba Kusini, wilayani Moshi, mkoani Kilimanjaro, amewabaka na kuwalawiti binti zake hao wenye umri wa miaka 10 na 13 na kuwajeruhi vibaya. Kitendo cha baba huyo kufanya unyama huo kimedaiwa kuwapandisha hasira kinamama wa kijiji hicho walioamua kumkamata na kumpeleka Kituo cha Polisi Himo huku wakitishia kumuua iwapo polisi watamwachia huru, kwa madai imekuwa ni kawaida yao kila akifikishwa kituoni hapo kuhusiana na unyama anaowafanyia watoto hao huachiwa. Mwanamume huyo anadaiwa kuwa na tabia ya kuwatendea vitendo hivyo wanaye hao kwa muda mrefu, kutokana na ugomvi baina yake na mkewe uliosababisha mkewe akimbie na kuwaacha watoto hao na baba huyo. Akizungumza Mwenyekiti wa Kijiji cha Kiria, Doroth Mtui, alisema taarifa hizo alizipata kutoka kwa majirani wa watoto hao, ambapo mtoto mmojawapo alimweleza kwa undani juu ya ukatili huo na baadaye walimkamata mwanamume huyo na kumpeleka Kituo cha

RAIS WA ZANZIBAR AHUDHURIA SHUGHULI ZA MAZIKO YA BABA YAKE WEMA SEPETU

Image
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, alipokuwa akiuwaga Mwili wa Marehemu Balozi Isaac Sepetu,katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi la zamani,Mnazi mmoja Mjini Unguja leo asubuhi,Marehemu alifariki juzi Jijini Dae es Salaam,na atazikwa Kijiji kwao Mbuzini Wilaya Magharibi. Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akimpa pole Mjane wa Marehemu Balozi Isaac Sepetu,Mama Miriam Sepetu,alipofika katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi la zamani,Mnazi mmoja Mjini Unguja,kuuaga mwili wa Marehemu leo Asubuhi.{Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.} Baadhi ya Wananchi mbali mbali wakiwa katika sehemu maalum nje ya ukumbi wa Baraza la Wawakilishi la zamani,Mnazi mmoja Mjini Unguja,wakisubiri kuuaga mwili wa Marehemu Balozi Isaac Sepetu,leo asubuhi ambapo utazikwa Kijiji kwao Mbuzini Wilaya Magharibi.{Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.}

RUFAA YA BABU SEYA, PAPII KOCHA KILICHOBAKI NI HUKUMU TU BAADA YA KESI KUPITIWA UPYA

Image
Leo, Jumatano, jopo la majaji watatu wa Mahakama ya Rufani nchini Tanzania limeipitia upya hukumu yao. Katika rufaa hiyo leo wakili wa Babu Seya na Papii Kocha ameiomba mahakama hiyo ifute ushahidi na waachiwe huru lakini serikali imepinga. Kutokana na hatua hiyo, leo mahakama ya rufaa haijafanya uamuzi wowote imewapiga kalenda na kesi inasubiri hukumu mpya. Nguza Viking na Papii Kocha wanatumikia kifungo cha maisha jela kwa makosa ya kubaka na kulawiti watoto wadogo wa shule ya msingi. Nyuso za matumaini....... Johnson Nguza 'Papii' akibusu mkono wake baada ya kuibusu ardhi mara baada ya kutoka mahakamani. Papii akinyoosha mkono juu kama ishara ya kumshukuru mungu. Waandishi wa habari wakiwa chini wakati wa harakani za kuchukua matukio mahakamani hapo. Nguza Vicking 'Babu Seya' akiwa na Mwanawe Johnson Nguza wakati wakitoka mahakamani. Nguza Vicking 'Babu Seya' akiwa na Mwanawe Johnso

Kiongozi wa waasi wa M23 ajisalimisha

Image
Kiongozi wa waasi wa M23 Bertrand Bisiimwa ameripotiwa kusalimu amri kwa jeshi la Uganda. Kiongozi huyo wa waasi alivuka na kuingia nchini Uganda kwenye masururu wa magari mawili huku wanajeshi wa Umoja wa Mataifa na wale wa DRC walipofika kilomita tano kuelekea katika kambi yake ya kijeshi Mwandishi wa BBC Ignatius Bahizi amesema baada ya kuongea na afisaa mmoja wa usalama eneo la Bunagana alimthibitisha kujisalimisha kwa Bisiimwa akisema kuwa anahojiwa na maafisa wa usalama katika eneo la Bunagana katika mpaka wa Uganda na Congo DRC. Waasi wa M23 mnamo siku ya Jumatatu walitoroka maeneo yao ya vita ikiwemo eneo la Rumangabo baada ya kukabiliwa na mashambulizi kutoka kwa jeshi la UN na sasa inaarifiwa wametorokea msituni. Majeshi yanayopambana na waasi hao yamefanikiwa kuwashinda waasi hao katika miji waliyokuwa wameiteka na sasa kuna matumaini kuwa jeshi la DRC linaweza sasa kusitisha harakati za kundi hilo ambazo zilianza miezi 20

Mtuhumiwa sugu akamata mkoani Simiyu...Silaha 45 za kivita , 17 za kienyeji na risasi 892 zanaswa

Image
OPERESHENI Maalumu ya Jeshi la Polisi Mkoa wa Simiyu kukabiliana na vitendo vya Ujambazi, Ujangiri wa uwindaji haramu pamoja na wahamiaji haramu umefanikisha kukamatwa kwa silaha 45, zikiwemo za Kivita na 17 za kienyeji na risasi 892 na magazine 24 huku watuhumiwa sugu wa ujambazi na ujangiri wakitiwa mbaroni. Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Simiyu Salum Msangi. Akizungumza jana na mbele ya waandishi wa Habari ofisini kwake, Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Simiyu Salum Msangi alisema kuwa opresheni hiyo ilitokana na kuwepo vitendo vya uhalifu katika Wilaya tano za Mkoa huo na kwenye maeneo ya mbalimbai ya Mapori Tengefu ya Uwindaji kwa kipindi cha mwaka moja tangu kuanzishwa kwake Desemba 2012. Silaha zilizokamatwa za kisasa na za kienyeji. Kamanda Msangi alieleza kuwa miongoni mwa silaha hizo 45 na magazine 28 zilikamatwa ni pamoja na SMG 7 risasi 763 na G3 moja ikiwa na risasi zake 35 iliyokuwa ikitumiwa na mwanamke mmoja aliyekamatwa Hollo Mabuga

NAFASI MPYA ZA KAZI BENKI KUU ( B.O.T) ZAIDI YA 50

Accountants, Database Administrator, Business Analyst, Web Developer, Computer System Analyst/Programmer, IT Technician, Senior Enterprise Architect (Information Systems Services), Senior Legal Officer, Economist, Financial Analyst, Bank Examiner, Receptionist, Office Attendant (Kitchen), Artisan (Plumber), Personal Secretary, Security Officer, Risk Analyst, Senior Legal Officer, Drivers, Messenger, Bank Officer, Senior Supplies Officer, Human Resource Officer Applications deadline: 11th November, 2013 EMPLOYMENT OPPORTUNITIES The Bank of Tanzania, an equal opportunity employer and Tanzania’s central bank, is looking for suitably qualified young Tanzanian citizens of high personal integrity to fill the following vacant positions at the Head Office and at its Branches in Mwanza, Mbeya, Arusha, Zanzibar and Training Institute, Mwanza. 1 Position: Accountant III (Domestic Payments and Settlement) - 2 Posts Reports to: Head of Division Contract type: Contract for