Posts

Mrembo afanyiwa kitu mbaya

Image
Mrembo huyo akiongea na simu kuomba msaada. Na Chande Abdallah, AMANI Dar es Salaam: Hatari! Mrembo aliyetambulika kwa jina moja la Saida, amefanyiwa kitu mbaya kweupe baada ya kukombwa vitu vyote na mwanaume aliyedaiwa kutoka naye baa aliyemsukuma kutoka ndani ya Bajaj waliyopanda na kumsababishia majereha. Tukio hilo likiwa ni mfululizo wa mengi yanayotokea maeneo ya Sinza, Afrika Sana jijini Dar, hasa nyakati za alfajiri, hivi karibuni wapita njia wa eneo hilo walisema kuwa walimuona Saida akitokea kwenye baa moja maarufu eneo hilo akiwa na mwanaume huyo asiyejulikana. Ilidaiwa kwamba, wawili hao walionekana wakiyumba kutokana na kukesha wakipata kinywaji, walipanda Bajaj kisha ikaanza kuondoka lakini kabla hawajafika mbali ndipo wakamuona mrembo huyo akidondoka huku Bajaj ikitokomea kusikojulikana. “Alipoinuka, alikuwa amechafuka sana na ameumia begani, damu zilikuwa zikimtoka ndipo akarudi tena hapa baa lakini wahudumu waligoma kumpokea, wakamweka nje,” alisema

LIGI YA MABINGWA ULAYA BARCELONA WAITANDIKA ARSENAL GOLI 3 KWA 1

Image
   

Rais Magufuli na Mke Wake Wamekifagilia Kipindi cha 360 cha Clouds FM..Wapiga Simu Laivu Wakiwa Hewani Nakusema Haya

Image
Leo asubuhi Mkuu wa Nchi Rais John Pombe Magufuli amepiga simu kwa kusuprise kwenye kipindi cha Clouds 360 cha Clouds TV huku kikiwa hewani na Kuwaambia kuwa yeye na mkewe ni washabiki wakubwa sana wa kipindi hicho..amesema yeye na mkewe kila asubuhi huwa waangalia na kufurahishwa sana na watangazaji hao....Mkewe naye aliongea na kusema huwa anacheka sana kwa vituko vya watangazaji hao wakati wakichambua habari mbali mbali .... Hongera wana Clouds 360.....

MAGAZETI YA LEO LAHAMISI TAREHE 17.03.2016

Image

Mama Diamond Atoa Siri ya Zari

Image
Mama mzazi wa staa wa Afro-Pop, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Sanura Kassim ‘Sandra’ ametoboa siri ya mkaza mwanaye, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ kushindwa kuishi Bongo na badala yake kukimbilia nchini Afrika Kusini ‘Sauz’. Sandra au Mama D aliyasema hayo katika mahojiano maalum na Ijumaa Wikienda juu ya uhusiano wake na Zari kufuatia tetesi kuwa hawaivi ndipo akaweka mambo sawa. Mama D alisema kuwa yeye na Zari wapo vizuri lakini kinachomfanya mkwewe huyo kushindwa kuishi naye Bongo ni kutokana na biashara zake kudoda nchini Afrika Kusini. “Unajua anapokuwa huku (Bongo), biashara zake huwa zinayumba sana, wakati mwingine akipiga simu akiulizia biashara zinakwendaje anaambiwa hali ni mbaya au hazijaingiza chochote hapo ndipo huwa anachanganyikiwa. “Kwa mfano hivi karibuni alipiga simu akaambiwa hakuna fedha kabisa na biashara haziendi. Kilichofuata ni kujiandaa na kumchukua Tiffah (Latifah Nasibu) kisha akaondoka zake. “Hicho ndicho kinacho

Siri Imefichuka...CUF Watoa Sababu za Maalim Seif Sharif Hamad Kuishi Serena Hoteli Pamoja na Gharama Iliyotumika Hadi sasa

Image
SIRI imefichuka kuhusu hatua ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Zanzibar (SUK), Maalim Seif Sharif Hamad, kuishi hotelini jijini Dar es Salaam. Maalim Seif ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), amekuwa akiishi katika Hoteli ya Serena jijini Dar tangu aliporuhusiwa kutoka Hospitali ya Hindu Mandal Machi 8, mwaka huu alipokuwa amelazwa kwa matibabu. Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, mmoja wa ofisa wa ngazi za juu wa CUF, alishangazwa na hatua ya baadhi ya watu kuhoji kiongozi huyo kuendelea kuishi hotelini hapo. Alisema hatua ya kiongozi huyo kuishi hotelini ni matokeo ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), kushindwa kutekeleza ahadi ya kumpa nyumba pindi anapokuwa Dar es Salaam katika shughuli zake. Alisema kutokana na hali hiyo imekuwa ni utaratibu kwa kiongozi huyo kufikia katika hoteli hiyo na gharama za kuishi hotelini hapo hulipwa na SMZ kwa mujibu wa sheria. “Tangu mwaka 2010 Maalim aliah

Rais Magufuli Awaapisha Wakuu wa Mikoa

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimuapisha Meja Jenerali Mstaafu Salum Mustafa Kijuu kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Hafla hiyo fupi ya kuwaapisha Wakuu hao wa Mikoa imefanyika leo Ikulu,jijini Dar na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimuapisha Meja Jenerali Mstaafu Raphael Mugoya Muhuga  kuwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimuapisha Kamishna Mwandamizi Msaidizi wa Jeshi la Polisi, Zelote Steven Zelote kuwa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimuapisha Mh. Anne Kilango Malecela kuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga.   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimuapisha Paul Christian Makonda kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimuapisha Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel E

ZIARA YA WAZIRI MKUU WILAYANI ISSENYI 2

Image
Waziri Mkuu, Kassim Majajaliwa  akifurahia zawadi ya picha aliyozawadiwa na wananchi wa Kata ya Kakunyu wilayani Missenyi akiwa katika ziara ya mkoa wa Kagera  Machi 14, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) Afisa Mifugo  wa Kata ya Kakunyu wilayani Missenyi, Eric Kagoro  akitoa maelezo mbele ya Waziri Mkuu na wananchi kuhusu tuhuma kuwa analinda wafugaji toka nchi jirani wanaolisha mifugo yao kwenye ardhi ya Tanzania kinyemela. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Maskini Millen Magese..Ugonjwa Wake Waendelea Kumsumbua Afanyiwa Operation Mara 13...Ashindwa Kufanya Show Afrika Kusini

Image
Akiwa kitandani, Millen Magese anaongea kwa tabu baada ya kuzidiwa katikati ya onesho la Mercedes Benz Fashion Week, jijini Johannesburg, Afrika Kusini. Anawatoa hofu mashabiki wake kwasababu kilichotokea kiliwashtua. Akiwa kwenye kitanda cha hospitali, mwanamitindo huyo aliyewahi kuwa Miss Tanzania, anasema kiwango cha sukari kilikuwa kimeshuka kwa kiasi kikubwa kutokana na kupata maumivu makali na kutokwa damu nyingi kwa siku nane mfululizo. Millen akipewa huduma ya kwanza baada ya kuzidiwa Kutokana na tukio hilo, Millen ameshindwa kuendelea kushiriki kwenye show hiyo kubwa ya fashion. Maumivu anayoyazungumzia Millen si maumivu ya kawaida, ni maumivu makali. Mrembo huyo yupo kwenye vita vigumu na virefu dhidi ya ugonjwa uitwao Endometriosis. Ni ugonjwa ambao huhusisha seli zinazofaa kuwa ndani ya mji wa uzazi kuwa nje ya mji huo. Millen na wanawake wengine wanaosumbuliwa na ugonjwa huo hukabiliana na maumivu makali kila nyakati za siku zao za hedhi. N

Mike Tyson auza mjengo wake wa Las Vegas

Image
Mike Tyson. -UNGEPENDA kuishi kistaa na una kiasi cha Dola za Marekani Usd milioni 1.5 sawa na shilingi bilioni 3.3? Kama hivyo ndivyo, basi unaweza kununua mjengo wa kifahari wa mwanamasumbwi wa zamani wa Marekani, Mike Tyson. Staa huyo ameishi katika mjengo huo wenye futi za mraba 5,800 tangu mwaka 2008 ila sasa ameamua kuhamia kwenye mjengo mpya wenye vyumba vitano vya kulala na mabafu sita. Mbali na kuhama, mjengo huo bado hauko vibaya maana una sehemu tatu za kupashia moto nyumba (fireplaces), chumba cha kukutana na wahabari, sehemu ya kunywea mvinyo, eneo la kuchezea pool na maporomoko yaliyo sehemu ya kuingilia jumba hilo. Wakala wa Tyson, Ken Lowman, ameeleza kuwa eneo hilo lote limefanyiwa maboresho mapema mwaka huu na lipo katika muonekano mzuri japo linakosa kitu kimoja ambacho ni sehemu ya kufugia chui.