Posts

TUKIO ZIMA KATIKA PICHA: TAZAMA MAZISHI YA MSANII WA BONGO MOVIE RECHO, KATIKA MAKABURI YA KINONDONI JIJINI DAR ES SALAAM.

Image
  Majeneza yenye miili ya Recho na mwanaye.   Miili ya Rachel Haule 'Recho' na mwanaye ikishushwa kwenye gari maalum baada ya kuwasili Viwanja vya Leaders ikitokea nyumbani Palestina, Dar tayari kwa kuagwa.   Waombolezaji wakiwa na simanzi baada ya mwili kuwasili Leaders.

WAZIRI DK. MUKANGARA AWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA HABARI , VIJANA UTAMADUNI NA MICHEZO BUNGENI

Image
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangara akiwasilisha Bungeni makadirio ya mapato na matumizi ya fedha ya Wizara yake kwa mwaka 2014/2015 mjini Dodoma jana. Waziri Mukangara ameomba Wizara yake iidhinishiwe kiasi cha Shilingi, 35,371,884,000 ambapo kati ya hizo jumla ya shilingi 20,371,884,000 ni za matumizi ya kawaida na kiasi kilichobaki ni fedha za miradi.  Viongozi wa Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Habari wakifuatilia Hotuba hiyo.  Baadhi ya wadau wa Habari akiwepo Mkurugenzi wa Kituo cha Redio 5 cha jijini Arusha Francis Robert (kushoto) akifuatilia hotuba hiyo bungeni mjini dodoma leo.  Innocent Mungy kutoka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) akifuatilia mjadala wa Bajeti bungeni mjini Dodoma.  Wadau mbalimbali wa sanaa, Michezo na Utamaduni walikuwepo.  Wasanii wakifuatilia mjadala wa bajeti Bungeni, mtaalm Dude na kule P Funks mwaandaaji wa muziki na pia msaani wa muziki.

RECHO HAULE APUMZISHWA KATIKA NYUMBA YAKE YA MILELE, KINONDONI DAR

Image
Mwenyekiti wa Bongo Muvi, Steven Nyerere akiweka shada la maua katika kaburi la Recho. Ndugu wa marehemu wakiweka mashada. Wasanii wa Bongo Muvi kutoka kushoto Aunt Lulu akiwa na wenzake. Watumishi wa Mungu (katikati) wakifanya maombi baada ya maziko. Mchumba wa marehemu George Saguda (kushoto) akiweka udongo katika kaburi la Rachel na mwanae. Msanii Blandina Chagula 'Johari' akiweka udongo kaburini. Mjomba wa marehemu, Evance Haule (kushoto) akiweka udongo katika kaburi la marehemu. Ndugu wa marehemu wakiweka mchanga katika kaburi la marehemu Rachel Haule. Mafundi wakichanganya zege. Mafundi wakisawazisha zege. (PICHA NA RICHARD BUKOS, DENIS MTIMA, MAYASA MARIWATA, SHANI RAMADHANI, HAMIDA HASSAN, IMELDA TARIMO/GPL)

MWILI WA RACHEL HAULE WAAGWA LEO HII, IRENE UWOYA AZIMIA. PICHA HIZI HAPA

Image
Mwili wa muigizaji wa filamu nchini Rachel Haule umeagwa leo hii katika viwanja vya Leaders na baada ya hapo atazikwa katika makaburi ya Kinondoni. Wasanii wengi ndugu, jamaa na marafiki wamejawa katika simanzi kubwa huku Irene Uwoya akizimia pengine kwa mshituko wa kuondokewa na msanii mwenzao. Angalia picha zikionyesha matukio ya mwili wa Rachel tangu akitolewa Muhimbili, kupelekwa Sinza na Leaders.......... Irene Uwoya akiwa amezimia 

Joseph Mbilinyi 'Sugu' Amlipua Zitto Kabwe

Image
Ni katika Hotuba yake ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni ya Wizara ya Habari,Utamaduni na Michezo aliyoiwasilisha Bungeni leo hii muda mfupi uliopita. Waziri Kivuli Joseph Osmundi Mbilinyi aka Sugu amemtaja Zitto Z. Kabwe kama Mmiliki wa Kampuni ya Leka Dutigite aliyofanya biashara isivyo halali na Mashirika ya Umma ya NSSF na TANAPA.  Sehemu husika ya Hotuba hiyo ni hii: Mheshimiwa Spika, Tarehe 13 Agosti, 2012, Msajili Msaidizi wa Makampuni katika Wakala wa Usajili wa Makampuni na Leseni (BRELA) alitoa Hati ya Usajili (Certificate iof Incorporation) kwa kampuni inayoitwa Leka Dutigite Limited. Kwa mujibu wa nyaraka za BRELA, Leka Dutigite Ltd. ina ofisi zake katika ghorofa ya kwanza ya jengo la City House lililoko katika Mtaa wa Mkwepu, Dar es SalaaM. Mheshimiwa Spika,  Katiba, yaani Memorandum and Articles of Association, ya kampuni ya Leka Dutigite Ltd. iliyosajiliwa BRELA tarehe 13 Agosti, 2012 inaonyesha kwamba mwenye hisa nyingi katika kampuni h

YANAYOENDELEA MUDA HUU KATIKA VIWANJA VYA LEADERS KWAAJILI YA WATANZANIA KUTOA HESHIMA YA MWISHO KWA DADA YETU RACHEL HAULE

Image
 Mchungaji akiendesha Sala kwaajili ya Marehemu Rachel Haule ambaye alipoteza maisha Jumatatu ya Wiki Hii kwa Uzazi  Sehemu lilipo Jeneza lenye Mwili wa Mpendwa Wetu Rachel Haule   Baadhi ya waombolezaji waliofika katika viwanja vya leaders kwaajili ya kutoa heshima za mwisho kabla Mwili wa Marehemu Rachel haujapelekwa kupumzishwa katika Nyumba yake ya Milele MChungaji akiendelea kutoa Neno katika Msiba wa Msanii Rachel Haule aliyefariki Jumatatu, Mwili wa Marehemu unatarajiwa kuagwa muda si mrefu katika viwanja hivi vya leaders na hatimaye kwenda kupumzishwa kwa amani katika Makaburi ya Kinondoni.Picha zote na Josephat Lukaza wa Lukaza Blog. Picha Zaidi zitakujia Baadae

WAZIRI WA NCHI OFISI YA WAZIRI MKUU HAWA GHASIA AUMBUKA KUTOKA KAMBI YA UPINZANI BUNGENI.

Image
LAPF yakana kumdai Mbowe Yaruka kuwasaidia Msigwa, Mbilinyi SIKU chache baada ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Serikali za Mitaa Tawala za Mikoa (Tamisemi), Hawa Ghasia, kusema kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe amekopa kiasi cha sh bilioni moja kwenye Mfuko wa Pensheni kwa Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa (LAPF), Mkurugenzi Mkuu wa mfuko huo, Eliud Sanga, amekanusha. LAPF pia imekana kuwasaidia fedha au vifaa Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi na Iringa Mjini, Peter Msigwa, kama ilivyosemwa bungeni. Juzi, Ghasia alisema kuwa Mbowe anadaiwa sh bilioni moja na LAPF na ametumiwa waraka wa kumkamata ili afikishwe kwenye vyombo vya sheria. Waziri huyo alisema si kosa kwa wabunge kupewa fedha na LAPF, lakini ni kosa kwa mbunge kutorejesha fedha alizokopeshwa. Kauli ya LAPF Mkurugenzi Mkuu wa mfuko  huo, Sanga, alibainisha kuwa LAPF haijawahi kumkopesha Mbowe sh bilioni moja, na kwamba mfuko huo hauna utaratibu wa kuk

HALIMA MDEE AMLIPUA PROF TIBAIJUKA

Image
Adai anamiliki maelfu ya ardhi hapa nchini Wabunge wamshambulia, Makinda amuokoa CCM waitisha kikao cha dharura kumnusuru MBUNGE wa Kawe, Halima Mdee (CHADEMA), amemlipua Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka, kwamba anamiliki maelfu ya ekari za ardhi katika maeneo mbalimbali nchini. Mdee ambaye ni Msemaji wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, alirusha kombora hilo jana bungeni wakati akisoma maoni ya kambi hiyo kwa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa mwaka wa fedha 2014/2015. Makombora hayo ya Mdee, yalimfanya Waziri Tibaijuka, kutumia muda mrefu zaidi kujibu mashambulizi badala ya hoja za wabunge wakati akihitimisha hoja yake. Majibu hayo yalimfanya Spika wa Bunge, Anne Makinda, kila mara kumtaka Waziri Tibaijuka ajibu hoja za wabunge badala ya kujikita kumjibu Mdee, katika masuala yanayoonekana ni binafsi. Waziri Tibaijuka, alisema kuwa Mdee amekuwa bingwa wa kuiba siri za serikali ikiwemo mwaka jana k