Posts

HII NDO KAULI YA DIAMOND BAADA YA KUHUSISHWA NA BIASHARA YA MADAWA YA KULEVYA

Image
Msanii Wa Muziki wa Bongofleva mwenye jina kubwa Town na mwenye Mkwanja mkubwa hapa nchini Nasseeb Abdulmaliki “Diamond” amejitokeza na kukanusha kuwa hahusiki na biashara ya madawa ya kulevya.   Kwa muda mrefu sasa kumekuwa na taarifa za Diamond kujihusisha na biashara hiyo hasa kutokana na ukaribu wake na wafanyabiashara wakubwa wa dawa za kulevya wenye maskani yao nchini Afrika Kusini.  Taarifa zaidi zinasema ni wafanyabiashara hao waliohusika kwa karibu kuusafirisha mwili wa marehemu Albert Mangwair, aliyefia huko huko Afrika Kusini ambaye taarifa za kifo chake ziligubikwa na matumizi ya madawa ya kulevya. Akikanusha taarifa hizo Diamond amesema  :   “ Ni kweli mimi nina pesa za kutosha kuniwezesha kuishi maisha ninayotaka lakini sijawahi kujihusisha na biashara hiyo . ... "Kufanya kazi kwa bidii kunalipa na kazi yangu inaonekana na ndiyo inayoniwezesha kuwa na fedha ambazo leo watu wameanza kuzitilia shaka. Sielewi nia ya watu hawa ni nini?”

ALHAJ MWINYI NA MZEE MKAPA WAWASILI ZIMBABWE KUHUDHURIA SHEREHE ZA KUAPISHWA KWA RAIS MUGABE

Image
Marais Wastaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi na Benjamin William Mkapa pamoja na wake zao, Mama Sitti Mwinyi na Mama Anna Mkapa, wakiwasili katika Uwanja wa  Ndege wa Kimataifa wa Harare, Zimbabwe, walikoalikwa kushiriki katika sherehe ya kuapishwa kwa Rais wa Zimbambwe, Mhe. Robert Mugabe, inayotarajiwa kufanyika kesho Alhamisi Agosti 21, 2013.   (PICHA NA IKULU)

GODLESS LEMA AUGUA GHAFLA, KESI YAKE YAAHIRISHWA

Image
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Arusha jana imeshindwa kuanza kusikiliza kesi ya uchochezi inayomkabili Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, dhidi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo, kutokana na mbunge huyo kuwa mgonjwa. Wakili wa Lema, Method Kimomogoro, aliieleza mahakama hiyo mbele ya Hakimu Mkazi, Hawa Mguruta, anayesikiliza shauri hilo kuwa Lema anaumwa na alikuwa amelazwa katika Hospitali ya AICC tangu Agosti 14 hadi 19, mwaka huu aliporuhusiwa kutoka hospitali, hivyo ametakiwa apumzike kwa muda wa siku 10 kuanzia Agosti 19, mwaka huu.   Wakili Kimomogoro aliomba shauri hilo liahirishwe hadi siku nyingine, ombi lililokubaliwa na hakimu aliahirisha kesi hiyo hadi Oktoba 1 na 2 mwaka huu, ambapo mashahidi tisa wanatarajiwa kutoa ushahidi wao. Wakili wa Serikali, Elizabeth Swai, anayesaidiana na Mary Lucas, alikubaliana na ombi hilo na kuongeza kuwa mashahidi wanne miongoni mwa tisa walikuwapo mahakamani hapo kutoa ushahidi wao jana ambao ni Mkuu

ANGALIA PICHA ZA MSAFARA WA MBIO ZA MWENGE ULIVYOPATA AJALI MKOANI DODOMA:

Image
MBIO za Mwenge wa Uhuru uliokuwa ukikimbizwa katika Wilaya ya Dodoma mjini zimeingia Dosari baada ya kupata ajali kilometa 3 kabla ya kukabidhiwa wiliya ya Mpwapwa. Ajali hiyo iliyotokea jana majira ya 2;24 asubuhi katika mtelemko wa mlima fufu wilayani Chamwino na kusababisha watu 5 kujeruhiwa na kukimbizwa katika hospital ya mkoa wa dodoma. Watu hao ambao majina yao Bado hayajatambulika walipata majeraha katika maeneo mbali mbali ya miili yao ikiwemo kichwani, kifuani, mguuni na mikononi. Kaimu Kamanda wa polisi Suzan Kaganda aliyefika na kujione hali ilivyokuwa katika eneo hilo alisema chanzo cha ajali hiyo ni Matuta yaliwekwa kwenye Barabara hiyo inayojengwa kwa kiwango cha lami toka fufu hadi Dodoma bila kuwa na alama yoyote.  majeruhi akisaidiwa kupekwa kwenye gari tayari kukimbizwa hospital  gari iliyokuwa imembeba kiongozi wa mbio za mwenge ikiwa imeumia vibaya  majeruhi wakipatiwa hud

Basi la Turu lachomwa moto na wanakijiji....Abiria 60 wamenusurika

Image
  Abiria wapatao 60 waliokuwa wanasafiri na basi la Turu linalofanya safari zake kati ya mkoa wa Singida na Haidom mkoani Manyara, wamelazimishwa kuteremka toka ndani ya basi hilo na wananchi zaidi ya mia mbili ( 200 ) wa vijiji vitatu, na kisha kulichoma moto basi hilo. Taarifa toka eneo la tukio zinasema wananchi hao ni wa vijiji vya Singa, Idabagadu na Nkungi mkoani Singida, ambao baada ya kuhakikisha abiria wote wameshuka, walilichoma moto basi hilo ambalo limetekea sehemu kubwa. Sababu ya wananchi hao kuchukua uamuzi huo ni kutokana na basi hilo kumgonga mwanakijiji mmoja na kufa wiki tatu zilizopita

MERKEL APENDEKEZA MARUFUKU YA SILAHA MISRI

Image
Ujerumani imependekeza kupiga marufuku upelekaji wa silaha nchini Misri kama hatua itakayoratibiwa kwa pamoja na Umoja wa Ulaya kupinga hatua ya serikali ya Misri ya kuvunja maandamano kwa kutumia nguvu na kusababisha umwagaji damu. Kansela Angela Merkel wa Ujerumani ametowa wazo hilo katika mahojiano na televisheni la taifa hapo jana. Kansela Merkel amesema hatua zote zinaweza kuchukuliwa ikiwa ni pamoja na kupiga marufuku kupeleka silaha nchini Misri zikiwemo zile ambazo tayari zimeidhinishwa kwa serikali ya Misri. Amesema suala hilo litajadiliwa kati ya Ujerumani na washirika wenzake wa Umoja wa Ulaya katika mkutano utakaofanyika siku chache zijazo. Umoja wa Ulaya utakuwa na kikao chake cha kwanza cha mazungumzo ya dharura kutokana na umwagaji damu nchini Misri uliozusha wasiwasi mkubwa huku ukionya kwamba utaangalia upya uhusiano wake na nchi hiyo iliokumbwa na ghasia.

ANGALIA PICHA ZA MJUSI MKUBWA WA TANZANIA ALIEKO UJERUMANI ANAYETAKA KURUDISHWA

Image
  The governments of Tanzania and Germany will soon strike an agreement for the return to Lindi region of the remains of huge lizard species known as a dinosaur, which were taken to the European country during the colonial era, Parliament heard yesterday. The dinosaur remains were discovered in 1912 at Tandeguru village, Mipingo ward in Lindi region, and were taken for preservation in Humbolt museum. Dinosaur Skeleton

HII NDIO HISTORIA FUPI YA MAISHA YA ANTI EZEKIEL ALIKO ANZIA MPAKA SASA.ISOME HAPA

Image
JINA la Aunt Ezekiel siyo geni  kwa wadau mbalimbali wa burudani hapa nchini, ni staa ambaye hivi sasa ana jina kubwa kupitia sanaa yake ya uigizaji wa filamu aliyoianza miaka sita iliyopita. Japokuwa kwa sasa ni staa, amepitia mambo mengi magumu katika safari yake ya maisha mpaka kufikia hapo alipo hivi sasa. Aunt alizaliwa mwaka 1988 mkoani Dar es Salaam, baba yake akijulikana kama Ezekiel Grayson’ Jujuman’ ambaye alikuwa ni mchezaji hodari sana wa timu ya Simba. Alipata elimu yake ya msingi katika Shule ya Bunge mwaka 1993 hadi 1998. Alienda kumalizia darasa la saba katika Shule ya Msingi Chanzige iliyopo Kisarawe, mkoani Pwani. Vipi maisha yalikuwaje baada ya kumaliza shule? “Kwa kweli maisha yalikuwa ni magumu mno kwa maana nilipomaliza shule tu, alijitokeza mwanaume na kutaka kunioa kitu ambacho mimi sikukipenda kabisa lakini baba yangu alitaka hivyo kwa vile uwezo wa kunisomesha hakuwa nao tena na maisha yalikuwa ni magumu sana. “Ba

Ruto tells off CORD over calls for referendum

Image
Deputy President William Ruto Kenya: Deputy President William Ruto has told off politicians calling for a referendum to determine how the president will be elected in the future. Ruto the calls coming just four months after Kenyans went to the ballot are ploys to frustrate the new government. He said it is a shame that Cord leaders are engaging in unnecessary debates instead of serving Kenyans. “This is time to serve the nation and not engage in petty politics. We cannot start another campaign just after we held the General Election,” he said. He said the public is not ready for a referendum and asked Kenyans to ignore the calls. He said Cord leaders are hell-bent on frustrating the Government’s activities especially on devolution, adding such efforts are uncalled for. “We want service delivery and not calls for another referendum. Kenyans are tired of elections and thus should ignore this call by the opposition to destabilise u

ULIMWENGU MZIMA WALAANI MAUAJI YA RAIA NCHINI MISRI

Image
Baada ya polisi wa Misri kutumia nguvu kuvunja mikusanyiko ya wafuasi wa rais aliyepinduliwa Muhammad Musri na kuua mamia ya watu na kujeruhi maelfu ya wengine mjini Cairo, walimwengu wameonesha wasiwasi mkubwa na kulaani mauaji hayo.  Umoja wa Mataifa umelaani vikali ukandamizaji huo wa polisi wa Misri dhidi ya waandamaji wanaotaka kurejeshwa madarakani Rais Muhammad Mursi, suala ambalo limesababisha maelfu ya watu kuuawa. Jamhuri ya Kiislamu ya Iran pia imelaani vikali mauaji na ukandamizaji wa jeshi la Misri dhidi ya wananchi wa nchi hiyo. Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imetoa taarifa ikisema: "Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inafuatilia kwa karibu matuko ya Misri na inabainisha wasiwasi wake mkubwa kutokana na yanayojiri nchini humo. " Iran imetahadharisha kwamba machafuko ya sasa nchini Misri yanaweza kuitumbukliza nchi hiyo katika vita vya ndani. Wakati huo huo Harakati ya Map

RAIS DKT. KIKWETE ATOA HESHIMA ZA MWISHO KWA NEMELA MANGULA

Image
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Marais wastaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi na Mzee Benjamin William Mkapa, Waziri Mkuu Mhe Mizengo Pinda, Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda, Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana na viongozi wengine wakiwa katika msiba wa binti wa Makamu Mwenyekiti wa CCM Mhe Phillip Mangula nyumbani kwake Oysterbay jijini Dar es salaam leo Agosti 19, 2013. Marehemu Nemela amafariki Jumamosi iliyopita kwa ajali ya gari. mwili wake unatarajiwa kusafirishwa kesho kwenda Njombe kwa mazishi yanayotarajiwa kufanyika Agosti 21, 2013 Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na Mke wake Mama Salma Kikwete wakitoa heshima zao za mwisho kwa marehemu Nemela Phillip Mangula, binti wa  Makamu Mwenyekiti wa CCM Mhe Phillip Mangula nyumbani kwake Oysterbay jijini Dar es salaam leo Agosti 19, 2013. Marehemu Nemela amafariki Jumamosi iliyopita kwa ajali ya gari. mwili wake unatarajiwa kusafirishwa kesho kwenda Njombe kwa mazishi yanayotarajiwa k

Mtandao wa Kagame wadai kuwa Mama Salma Kikwete ni Mnyarwanda

Image
8/20/2013      Mtandao  wa  News  of  Rwanda  umeendelea  kutuchokonoa  watanzania  ili  kuupima  msimamo  wetu..... Baada  ya  kukurupa  na  madai  kwamba  Rais  Kikwete  si  mtanzania  halisi  na  kwamba  ni  mtu  mwenye  asili  ya  Burundi, mtandao  huo  umekuja  na  kioja  kipya.... Taarifa  iliyotolewa  jana  tarehe  19/08/2013  na  mtandao  huo  inadai  kwamba  mke  wa  Rais  Kikwete  aitwaye  Mama  Salma  Kikiwete  ni   mnyarwanda   wa  kabila  la  wahutu ( mhutu ).. Katika  maelezo  yake, mtandao  huo  umeenda  mbali  na  kudai  kuwa  Mama  Salma  Kikwete  ni  binadamu  wa  rais  wa zamani wa Rwanda, Juvenal Habyarimana  na  ndo  maana  rais Kikwete  alitoa  ushauri  wa   mazungumzo  ya  amani  kati  ya  Kagame  na  waasi.... ............................................................. HII  NDO  POST  YAO  WALIYOTOA --------------------------------------------- New details obtained by News of Rwanda may give insight into why Tanzania’s President

Bibi kizee mchawi adondoka wakati akiwanga saa mbili usiku

Image
    Watu wakimshangaa bibi aliyedaiwa kuwa mchawi. Ni aliyekaaa katikati. ...Akipewa chakula, wali na maharage kutoka kwa wasamaria wema.   Akiwa kapakatia sahani la wali aliopewa. Watu waliokusanyika kumshangaa.   BIBI mmoja ambaye hakuweza kupatikana jina lake mara moja, jana majira ya saa mbili usiku maeneo ya Chanika, jijini Dar es Salaam alidaiwa kuanguka wakati akiwa katika harakati za kuwanga ambapo wakazi wa hapo walimkamata na kuanza kumhoji kwa maswali mbalimbali kama anavyoonekana pichani.

Huyu ndo Mangunga aliyewatoroka akina Masogange baada ya polisi kuwanasa

Image
Waziri wa uchukuzi Prof. Harrison Mwakyembe alimtaja mshukiwa mmoja wa dawa za kulevya aitaye Nassoro Mangunga  na  kuwataka  polisi  wamtie  nguvuni  popote  atakapoonekana.... Hata  hivyo, mshukiwa huyu pamoja na picha zake alishaandikwa na gazeti la SANI katika toleo lake la Agosti 7-9, 2013 (toleo la 1042) pamoja na namna alivyosafirisha mzigo pamoja na akina Masogange. Hii  ni  taarifa  ya  gazeti  hilo: Unaweza kukimbia lakini huwezi kujificha. Msemo huu unaonekana kutimia kwa kijana anayedaiwa kuambatana na watuhumiwa wa dawa za kulevya waliokamatwa Julai 5 mwaka huu nchini Afrika Kusini, Agness Gerald 'Masogange' (25) na Melisa Edward (24), kunaswa na gazeti hili.   Kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa na gazeti hili, wasichana hao, Masogange na Melisa walisafiri ndege moja na kijana anayejulikana kwa jina la Nassoro Mangunga wakitoka Dar es Salaam kwenda Afrika Kusini, wakisafiri na ndege ya Shirika la Ndege la Afrika Kusini (SAA), yenye namba SA

Mtoto apigwa na kulishwa Mavi na baba yake mzazi huko Mara

Image
8/20/2013   MWALIMU wa Shule ya Msingi Morotonga, wilayani Serengeti, Mkoa wa Mara, Karata Mugunda, anashikiliwa na Jeshi la Polisi wilayani hapa, kwa tuhuma za kumpiga na kumlisha kinyesi mtoto wake wa kumzaa mwenye umri wa miaka 10.  Mwenyekiti Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu, Wilaya ya Serengeti, Samwel Mewama, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba mtoto huyo alilishwa kinyesi alichokuwa amejisaidia ndani ya nyumba yao. Kwa mujibu wa Mewana, tukio hilo la kusikitisha lilitokea Agosti 14, mwaka huu saa 12 alfajiri. “Chanzo cha tukio hili la kikatili ni mtoto huyo kujisaidia haja kubwa ndani ya nyumba, baada ya kuogopa kutoka nje usiku wa manane. “Baada ya kujisaidia, baba yake ambaye ni mwalimu, alikasirika na kuamua kumwadhibu kwa kumchapa fimbo sehemu za makalio na kumsababishia majeraha ya kutisha. “Pamoja na kumwadhibu kwa fimbo, alimlazimisha ale kinyesi chote alichojisaidia kisha akamlazimisha anywe maji kwa wingi,” ali

Mwanamke avunjwa nyonga na kunyolewa nywele kwa kisu na mume wake

Image
8/20/2013   Tajiri ambaye ni mfanyabishara mkubwa katika maduka ya Kariakoo, Dar aliyetajwa kwa jina moja la Urio anadaiwa kumvunja nyonga na kumjeruhi mkewe Eva Pascal anayeuguza majeraha kwenye Hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Akizungumza kwa uchungu akiwa wodini hospitali hapo, Eva au mama Tina alisema kuwa tukio hilo lilitokea hivi karibuni nyumbani kwao Kimara-Temboni, Dar. Mama Tina alisimulia kuwa siku ya tukio mumewe alikuwa ana siku kadhaa hajarudi nyumbani hivyo akamfuata katika Baa ya Temboni Resort kwa ajili ya kumuuliza sababu za kushindwa kurudi nyumbani. Alisimulia huku akitokwa machozi: “Nilipofika tu nikamuuliza swali hilo, alinitandika kofi kisha akanipiga ngumi ya jicho hadi nikazimia. “Nilishangaa nilipozinduka na kuwakuta manesi wamenizunguka. Nilipomuuliza mume wangu imekuwaje aliniambia eti nililewa na kuanguka ndiyo sababu nipo hapa. “Kiukweli baba Tina ananinyanyasa sana, ananipiga hadi kufikia hatua ya kuniunguza na

Mume wa mtu afumaniwa Gesti akingonoka na binti yake

Image
Mwanaume aliyetajwa kwa jina moja la Temba, mkazi wa Kimara-Rombo, Dar ambaye ni dereva wa daladala amefumaniwa laivu na mkewe akiwa gesti na binti yao wanayemlea. Tukio hilo la aina yake lilijiri wiki iliyopita kwenye gesti hiyo iliyopo maeneo hayohayo ya Kimara-Rombo, majira ya saa 10:00 jioni ambapo Temba ambaye ni dereva wa daladala inayofanya safari kati ya Kimara na Kariakoo alinaswa kiulaini baada ya kuwekewa mtego. Baada ya mke wa Temba kuweka mambo vizuri aliitaarifu wanahabari  ambapo alihojiwa maswali muhimu kisha kutakiwa kuwajulisha polisi ili kuhakikisha kuna usalama wa kutosha. Kwa mujibu wa mke wa Temba, siku kadhaa nyuma aligundua kuwepo kwa mawasiliano ya kimapenzi kati ya mumewe na binti yao hivyo akalazimika kufanya uchunguzi wa kina. Mama Temba alisema kuwa katika harakati zake, siku ya tukio alifuma ujumbe wa simu ‘SMS’ kwenye simu ya binti huyo, aliposoma alishtuka kuona ujumbe wa kimapenzi kutoka kwa mumewe. Kwa kuwa hakuamini a

Haya ndo mashitaka matatu aliyosomewa Sheikh Ponda mahakamani jana

Image
  Kiongozi wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Issa Ponda leo amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mfawidhi mkoa wa Morogoro kujibu mashitaka matatu yanayomkabili ambayo ni kutotii amri halali, kutoa maneno yenye nia ya kuharibu imani za dini na kushawishi  kutenda kosa.    Sheikh Ponda amefikishwa mjini Morogoro na helkopta ya jeshi la polisi majira ya saa tano asubuhi  chini ya ulinzi mkali ambapo askari waliimarisha ulinzi kwa muda wote huku kikosi cha kutuliza ghasia FFU wakiwa na silaha mabomu na mbwa ambapo hali hiyo imesababisha kusimama kwa baadhi ya shughuli zingine za kiofisi katika ofisi zilizopo jirani na mahakama ya hakimu mkazi wakati kesi hiyo ikiendelea ... Akisoma shataka mbele ya hakimu mkazi Richard Kabate , wakili mkuu wa serikali kanda ya Morogoro Benard  Kongola amedai kuwa shekh Ponda anadaiwa kutenda makosa hayo matatu Agosti 10 mwaka huu majira ya jioni katika viwanja vya shule ya msingi kiwanja cha nd