Sheddy Clever: Nimelipwa pesa nyingi sana kutayarisha wimbo wa Diamond na Ne-Yo


sheddy na Ne-yo
Producer Sheddy Clever wa Burn Records amesema kuwa amepata pesa nyingi alizolipwa na Diamond kutengeneza collabo yake na Ne-Yo, kiasi ambacho ingemchukua miezi mitatu kuipata kwa kazi zake za kawaida za production.
Sheddy ambaye ndiye producer anayepika collabo ya Diamond na Ne-Yo inayosubiriwa kwa hamu na mashabiki wa muziki wa Afrika, ameiambia phars kuwa hajawahi kulipwa kiasi hicho cha pesa toka ameanza kufanya production.
“Hii kazi tuliyoenda kufanya juzi nimelipwa, na nimelipwa vizuri tu...sijawahi kulipwa hivyo kwakweli yaani nafurahi sana,” alisema kwa furaha.
“Diamond ni msanii tofauti sana na haogopi kuwekeza katika kazi zake kwasababu anajua nini anachokifanya...Nimelipwa vizuri japokuwa kazi bado sijamaliza lakini nimelipwa pesa nyingi tu nzuri nimefikia hoteli nzuri.” alisema Sheddy.
Sasabu wengi huwa hawapendi kusema kiwango wanacholipwa, nilipomuuliza kama amelipwa zaidi ya shilingi milioni 1 alijibu;
Sheddy:[kicheko] Inazidi milioni 1 hata milioni 3 inazidi kabisa nimelipwa vizuri
Nikaendelea kumuuliza kama amelipwa zaidi ya shilingi milioni 5?
Sheddy:[kicheko na kigugumizi] labda nisiongelee sana hilo ila nimelipwa pesa nyingi kwakweli nisiwe muongo wala nisiwe mnafiki, mwenyezi Mungu ananiona hata kama nikiongea uongo nimelipwa pesa nyingi SANA (akasisitiza) kiasi cha kwamba ninaweza nikakaa studio kwa muda hata wa miezi miwili au mitatu ndo nikaipata pesa hiyo lakini nimeipata kwa kazi moja na kazi bado sijamaliza na kuwakabidhi bado sijawakabidhi.

Comments

Popular posts from this blog