KAULI YA MNYIKA BAADA YA LOWASSA KUPENDEKEZWA KUWANIA URAIS KUPITIA CHADEMA


  Ikiwa ni siku Chache tangu lowassa ajiunge na chama cha chadema kumekuwepo uvumi kuwa MBUNGE wa Ubungo, John Mnyika, amekiama chama chake kutokana na chama hicho kumkalibisha Lowassa na kumpa nafasi ya juu kabisa
Ukweli wa madai haya umethibitishwa leo hii baada ya Mnyika kuhudhulia katika mkutano wa kamati kuu (CC) ya chama cha demokrasia na maendeleo
Licha ya Lissu kutoa taarifa kuwa hakuna hali ya sitofahamu ndani ya chama icho ila bado watu wamekuwa wakivumisha mambo kuwa chama icho kimevurugika baada ya wanachama kutounga ujio wa aliyekuwa waziri mkuu Edward Lowassa
Taarifa kutoka ndani ya kikao cha CC kinachofanyika katika hoteli ya Bahari Beach zilizotufikia dawati la habari clansmedia zinasema, Mnyika amehudhuria mkutano huo na kueleza kuwa kutoonekana kwake, kumetokana na matatizo ya kifamilia.
Mwanasheria mkuu wa Chadema, Tundu Lissu amethibitisha Mnyika kuhudhuria mkutano huo.
“Mnyika yupo ndani ya ukumbi wa mkutano. Anashiriki kikao cha kamati kuu. Waliokuwa wanadhani chama chetu kimepata mpasuko kutokana na ujio wa Lowassa, walikuwa wanajidanganya.” alisema Lissu
Lissu amesema, ndani ya Chadema wako wamoja, yote yaliyotokea yalikuwa mapambano yanayotokana na ukomavu wa kidemokrasia uliyopo Endelea kutufatilia kwa kila habari inayofika juu ya dawati letu la clansmedia..

Comments

Popular posts from this blog