JESHI LA POLISI LIMELAZIMIKA KUVUNJA CHUMBA KUTOA MWILI WA MTU ALIYEKUFA SIKU NNE ZILIZOPITA.


Mtu mmoja Timotheo kweka (30) mkazi wa kiwanja cha ndege manispaa ya Morogoro amekutwa chumbani kwake amefariki dunia siku nne ziizopita na jeshi la polisi limelazimika kuvunja mlango na kutoa mwili huo .
Akizungumza na ITV mmiliki wa nyumba alikokuwa amepanga Leonard Benedicti amesema kwa mara ya mwisho marehemu alionekana nje siku ya jumamosi hadi leo walipohisi harufu nzito chumbani kwake ndipo walitoa tarifa kwa jeshi la polisi na kumkuta ndani amefariki na kichwa kikiwa kimebanwa kwenye stuli.
Wakizungumzia tukio hilo ndugu wa marehemu wamesema hawanawasiwasi na kifo cha ndugu yao kwani alikuwa mlevi wa pombe kwa muda mrefu ambapo wamesema siku ya jumamosi walikuwa na sherehe ya ukoo lakini marehemu hakuweza kufika ingawa hawakujua kama amefariki.
Jeshi la polisi mkoa wa Morogoro limedhibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo mwili wa marehemu umehifadhiwa kwenye chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya mkoa wa morogoro.

Comments

Popular posts from this blog