Posts

Wanafunzi Wadaiwa Kuwacharaza Viboko Walimu Wao

Image
Wanafunzi wa Kidato cha Sita Shule ya Sekondari Usevya wilayani Mlele Mkoa wa Katavi, wanadaiwa kuwashambulia kwa kuwacharaza viboko walimu wao wawili miongoni mwao akiwemo Makamu Mkuu wa Shule hiyo, Makonda Ng’oka “Membele’‘ (34) ambaye ameng’olewa meno matano kwa kipigo hicho. Walimu hao wawili wamedai kuwa hawako tayari kuendelea kufundisha katika shule hiyo huku wakisisitiza kuwa ni fedheha kwao kucharazwa viboko na wanafunzi wao wenyewe ambapo Mwalimu Gabriel Kambona aliachwa na ngeu kichwani. Mei mwaka huu, Ng’oka “Membele” alifikishwa katika Mahakama ya Mkoa wa Katavi kwa tuhuma za kumlawiti mwanafunzi wake akidaiwa kutenda kosa hilo kati ya Novemba 2015 na Aprili mwaka huu. Ilisemekana kukamatwa na kufikishwa mahakamani kwa Makamu Mkuu huyo wa shule hiyo kulifuatia wanafunzi wa kiume wanaosoma Kidato cha Tano sasa wako Kidato cha Sita katika shule hiyo kumkataa na kutishia kuandamana kupinga vitendo vyake vya kuwalawiti wanafunzi wake. Wanafunzi ha

RUBY AKANUSHA KUWA NA TATTO YA FREEMASON

Image
Ruby alikanusha kuwa katika imani hiyo na kusema kila kuwa mtu ana jicho na hana maana ya kuwa kwenye imani hiyo ya Freemason bali yeye ni Mkristo na anamuamini Mungu. “Hakuna binadamu bila macho, na mimi ni mkristo namuamini Mungu so sijawahi kuingia kwenye Freemason so hizo ni imani za watu na hiyo tattoo sijachora kwa ajili ya Freemason.” Amesema Ruby. Pia kuhusu uongozi Ruby ameweka wazi kuwa kwa sasa anajisimamia yeye mwenyewe, “Nimeamua kubadili uongozi na sasa najisimamia mwenyewe kwa ajili ya mashabiki wangu”.

MAGAZETI YA LEO JUMATANO TAREHE 14.06.2016

Image
Posted by JAFE MALIBENEKE at Wednesday, September 14, 2016 Email This BlogThis! Share to Twitter Share to Facebook

MAKAMU WA RAIS SAMIA SULUHU ASHIRIKI SHEREHE ZA KUAPISHWA KWA RAIS WA ZAMBIA EDGAR LUNGU

Image
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan akiwasili kwenye uwanja wa Taifa wa Mashujaa (National Heroes Stadium) jijini Lusaka kumwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kwenye sherehe za kuapishwa kwa Rais wa Awamu ya 6 wa Zambia Mhe Edgar C. Lungu leo Septemba 13, 2016   Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan akipungia mkono maelfu ya wananchi waliokuwa wakimshingilia wakati akiingia kwenye uwanja wa Taifa wa Mashujaa (National Heroes Stadium) jijini Lusaka kumwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kwenye sherehe za kuapishwa kwa Rais wa Awamu ya 6 wa Zambia Mhe Edgar C. Lungu leo Septemba 13, 2016  Rais Robert Mugabe akisalimiana na Rais wa Kwanza wa Zambia Dkt Kenneth Kaunda Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Rais wa Botswana Luteni Jenerali Seretse Khama baada ya kuwasili

WABUNGE WATOA POSHO KUSAIDIA MAAFA KAGERA

Image
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, (Tamisemi) George Simbachawene amesema madaktari bingwa zaidi ya 15 kutoka Mwanza wamepelekwa Kagera kwa ajili ya kuongeza huduma kwenye hospitali. Kadhalika, wabunge wameunga mkono juhudi za serikali na wameridhia kukatwa posho ya siku moja ili kuchangia kusaidia maafa yao. Hatua hiyo inafuatia muongozo wa mbunge wa Mlalo CCM, Rashid Shangazi aliyeomba kiti kutoa muongozo ili wabunge watoe fedha hizo kama sehemu ya kuomboleza pamoja na waathirika. Hoja hiyo iliungwa mkono na wabunge wa pande zote bila kuangalia itikadi zao. Hata hivyo, Mbunge wa Tarime vijijini Chadema John Heche alisema chama chake kilishatoa Sh 100,000 kila mbunge lakini kufuatia hoja hiyo na wao wapo tayari kuchangia posho zao.

SELECTION ZA VYUO VIKUU KWA WANAFUNZI WALIOOMBA KUJIUNGA NA VYUO MBALIMBALI MWAKA HUU ZIMETOKA

Image
Selection za TCU kwa walioomba kujiunga na vyuo mbalimbali kwa mwaka wa masomo 2016/2017  z imetoka. Bofya hapa  kuangalia     Selection Status  NB:  Tumia index number yako na password

MAAJABU: HUYU NDIYE BINADAMU MWENYE VIDOLE 12 MIGUUNI NA MIKONONI!

Image
Vijay akionesha vidole vyake 12 vya mikono.  Mchapaji wa India Vijay Singh anaweza kuchapa zaidi ya maneno 100 kwa dakika kwa kutumia vidole vyake 12.  Lakini Vijay, ambaye pia ana vidole 12 vya miguuni kutokana na dosari yake hiyo ya kimaumbile, anasema hawezi kupata kazi katika nchi yake aliyozaliwa sababu waajiri wanataka tu wanawake wenye mvuto. Sasa anapanga kuhamia Uingereza kwa lengo la kutafuta ajira baada ya kuwa amekataliwa maombi yake ya kazi zaidi ya 50. Mwanaume huyo mwenye umri wa miaka 48, anayetokea Agra kaskazini mwa India, alisema: "Wanataka wanawake wenye mvuto, si wanaume wenye vidole 12." Miguuni pia, Vijay ana vidole 12.  Watu wenye dosari za kimaumbile wanaonekana wenye bahati nchini India na Vijay yuko kwenye hali nadra kutokana na vidole vyake vya ziada kufanya kazi kama kawaida.  Watu wengi wenye hali hiyo wana vipande vichache vya tishu laini ambazo zinaweza kuondolewa na mara chache huwa na mfupa