Batuli: Rushwa ya Ngono iliniondoa Kaole
Msanii wa bongo movie Batuli ameweka wazi kuwa alikimbia kundi la Kaole sanaa Group baada ya kukutana na changamoto nyingi ikiwepo changamoto ya rushwa ya ngono. Batuli alifunguka hayo Jumatano alipokuwa katika kipengele cha Kikaangoni kinachofanyika kila siku ya Jumatano kupitia ukurasa wa facebook wa EATV. Batuli alifunguka na kusema kuwa moja ya sababu kubwa ambayo ilimfanya kuondoka katika kundi hilo ilikuwa kuombwa rushwa ya ngono ili aweze kupewa kipaumbele zaidi kuliko wasanii wengine jambo ambalo kwa upande wake hakuwa tayari kulifanya na kuamua kuondoka katika kundi hilo. Batuli anasema kabla ya kuweza kutoka kupitia mkono wa Kanumba alishasota sana katika kundi hilo na alikuwa akibaniwa nafasi kutokana na kutokubaliana na watu ambao walikuwa wakimtaka kingono ili waweze kumpa kipaumbele zaidi, ndipo hapo alipoamua kuondoka na baadaye msanii Kanumba ndipo alipoamua kumpa nafasi na kuweza kumtoa kisanaa. "Nilijiunga kaole lakini b