Posts

HALI NI MBAYA PICHA ZA NUSU UCHI BLOGER ZASAMBAA

Image
  Ama kwa hakika wadau nahisi bado hali si swari kwa taifa letu haswa kwa hii hali inayoendelea kuteka akili za wasichana kwa wavulana kwa kujipiga picha za utupu ambazo baadae huwa ni aibu na fedheha kwa familia zao huku wao wakiwa hawana jipya zaidi ya heshima zao kushuka Kusema kweli haya mambo kwetu bado ni mageni tofauti na mataifa mengine ambapo hicho ni kitu cha kawaida na mtu hulipwa pesa nyingi sana kupiga picha za namna hiyo.  Mwanadada aliyewahi kutengeneza kichwa cha habari gazetini akidai kubakwa na mbunge wa CHADEMA mheshimiwa Godbless Lema ambaye ni blogger pia Flora Lyimo a.k.a Mbuta Nanga ametengeneza kichwa cha  habari kwa mara nyingine tena baada ya kujipiga picha za uchi na kutupia kwenye blog yake. Mara baada ya kutumia picha hizi mwadada huyu alijisifu na kujigamba kuwa yeye ni African qeen na anajiamini!. Kwa upande mwingine anaweza kuwa sawa kwa imani yake ila kwa maadili ya nchii hii nadhani sio sahihi kupiga

NISSAN MITSUOKA..FOR SALE,

Image
CONTACT 0716 08 95 00 AU 0759 16 01 06. FOR SALE, CONTACT 0716 08 95 00 AU 0759 16 01 06 NISSAN MITSUOKA ENGINE SIZE 13000 KM USED 128000 IN JAPAN ONLY PRICE: 9,500,000/- YEAR: 1998  AVAILABLE IN ARUSHA TOWN-TANZANIA  SOURCE: 2JIACHIE USIHASAHU KULIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK ILI KUPATA HABARI ZAIDI

TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 LAFANA KATIKA UWANJA WA KARUME MJINI MUSOMA

Image
 Anaitwa Linah Sanga,kutoka nyumba ya vipaji THT akiimba jukwaani usikuwa kuamkia leo  Watu kibao,kila mmoja akijichia kivyake huku jukwaa likiwaka moto vilivyo kwa miondoko ya bandika bandua ya wasanii wanaotumbuiza.   Wakali wengine wanaokuja kwa kasi katika anga bongofleva-hip hop,Stamina na Youngkiller wakilishambulia jukwaa kwa kushusha mistari mikavu live.  Shangwe kila kona za mashabiki zimetawala uwanjani hapa.  Mwanadada Shilole akionesha umahiri wake wa kunengua jukwaani mbele ya maelfu ya  watazamaji waliojitokeza usiku huu kwenye tamasha la Serengeti fiesta  2013. PICHA ZAIDI  LIVE INGIA MICHUZIJR.BLOGSPOT.COM

22 TONS OF FAKE BEEF SEIZED IN CHINA

Image
This week, police in Xi'an province reported that they had found and seized more than 22 tons of fake beef at a local factory. Get this: the "beef" was actually made from pork (which is considerably cheaper than beef) that had been treated with chemicals including paraffin wax and industrial salts to make it look like it came from a cow. Shanghiist reports that the factory sold more than 1,500 kilos (3,000 pounds) of the fake beef to local markets at around 25 to 33 yuan ($4 or $5) per kilo. Six workshops that were producing the fake beef have been discovered and shut down. This isn't the first instance of fake meat being sold in China. In May of this year,Medical Daily reported that 904 people were arrested in China for "meat-related offenses" over three months at the beginning of 2013. Included in these arrests was one gang of meat crooks who made o

FILAMU YA "HE HURTS ME" YAZINDULIWA KWA KISHINDO.

Image
Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu, Bi. Joyce Fissoo akitoa hotuba kwa washiriki na baadhi ya wasanii waliohudhuria wakati wa uzinduzi wa Filamu ya "He hurts Me" iliyotengenezwa na Bi. Hilda Ngaja, filamu iliyozinduliwa katika Ukumbi wa Mbezi Garden jijini Dar es Salaam. Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu, Bi. Joyce Fissoo akionyesha juu filamu ya "He hurts Me" kuhashiria uzinduzi rasmi wa filamu hiyo uliofanyika hivi karibuni katika ukumbi wa Mbezi Garden jijini Dar es Salaam. Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu, Bi. Joyce Fissoo (kushoto) akiwa pamoja na mtengenezaji wa filamu hiyo Bi. Hilda Ngaja (kuli) wakifurahi kwa pamoja wakati wakiangalia kasha la filamu ya "He hurts Me" mara baada ya uzinduzi wa filamu hiyo. Mtengenezaji wa filamu ya "He hurts Me" Bi. Hilda Ngaja (kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na mme wake Mr. Mwambene (kulia) wakati wa uzinduzi wa filamu yake uliofanyika kati

JACKSON KISWAGA AWAKUMBUKA WAJAWAZITO NYUMBANI KWAKE ATOA MSAADA WA VITANDA

Image
Mkazi wa jimbo la Kalenga Bw Jackson Kiswaga kushoto akiwa na wafanyakazi wa Hospital teule ya wilaya ya Iringa -Ipamba Diwani wa viti maalum tarafa ya Kalenga Bi Shakra Kiwanga kulia na wafanyakazi wa Hospital Teule ya Iringa wakipokea msaada wa vitanda viwili vyenye thamani ya Tsh milioni 3 kutoka kwa Bw Jackson Kiswaga ambae ni mkuu wa kitengo cha M- Pesa na ukuzaji wa biashara ,msaada ambao ameutoa yeye binafsi kama mkazi wa jimbo la Kalenga Mkuu wa kitengo cha M-Pesa na ukuzaji wa biashara Voda Com Bw Jackson Kiswaga akimfariji Bi Stella Kalinga ambae amelazwa wodi la wajawazito katika Hospital teule ya wilaya ya Iringa jana alipofika kutoa msaada binafsi wa vitanda viwili kwa ajili ya kuongeza idadi ya vitanda kwa wajawazito hospitalini hapo MKAZI wa Kalenga wilaya ya Iringa mkoani hapa Bw Jackson Kiswaga ametoa msaada wa vitenda viwili vyenye thamani ya Tsh milioni 3.6 kwa Hospital teule ya wilaya ya Iringa Hospital ya Ipamba ili ku

Mnigeria ashinda shindano la urembo la kiisilamu

Image
Mwanadada wa Nigeria ndiye mshindi wa shindano la urembo kwa wasichana wa kiisilamu mjini Jakarta Indonesia. Obabiyi Aishah Ajibola, 21, alishinda shindano la kimataifa la wasichana wa kiisilamu kwa jina Muslimah mwaka 2013 siku ya Jumatano. Washindani 20 walishiriki mashindano hayo kuonyesha mitindo ya kiisilamu pamoja na maadili ya kiisilamu wakati wa mashindano hayo. Mashindano yalifanyika kabla ya shindano kubwa zaidi la mwanamke mrembo zaidi duniani, ambalo limeghadhabisha makundi ya watu wenye msimamo mkali nchini Indonesaia kwa kutaka kuandaliwa huko. Waliofuzu kwa fainali ya mashindano hayo, walichaguliwa kutoka miongoni mwa watu 500 waliochaguliwa kwa kutumia njia ya mtandao. Moja ya vikwazo vya kuruhusiwa kushirki kwenye mashindano ilikuwa kusimulia kisa chako na ambavyo ulianza kuvalia Hijab au mtandio, ambacho kilikuwa kikwazo kwa wote waliotaka kushiriki. Washiriki walitoka Bangla

Picha za Agness Masogange akiwa huru mtaani baada ya kutoka MAHABUSU

Image
Watanzania Agness Masogange na Melisa Edward waliokamatwa kwa kutuhumiwa kubeba dawa za kulevya huko Afrika Kusini wameachiwa kwa dhamana.    Mkuu wa Kitengo cha Dawa za Kulevya Afrika Kusini, Kamishna Toto Mangaleni aliithibitishia Mwananchi jana kuwa watuhumiwa hao wameachiwa kwa dhamana,lakini wataendelea kubaki Afrika Kusini wakati kesi yao ikiendelea. Mangaleni alisema wanawake hao ambao juzi pia walipanda kizimbani, walipata dhamana hiyo jana kutoka Mahakama Kuu ya Gauteng iliyoko eneo la Kempton Park jijini Johannesburg.   Hata hivyo, Kamishna Mangaleni alisema hawezi kuzungumzia zaidi kuhusu kesi hiyo kwa sababu hataki kuharibu uchunguzi ambao unaendelea dhidi ya Watanzania hao, ambao ni wasanii.   Marafiki wa karibu wa Masogange wanaoishi maeneo ya Midland Johannesburg ambao walikataa kunukuliwa majina yao, walithibitisha

Hakimu achomwa kisu mahakamani

Image
Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo iliyopo eneo la Nguzo Nane, Kata ya Kambarage Mjini Shinyanga, Satto Nyangoha amejeruhiwa kwa kuchomwa kisu katika shavu lake la kushoto baada ya kutoa hukumu ya kesi ya wizi wa baiskeli. Kitendo hicho kinadaiwa kufanywa na mlalamikaji katika kesi hiyo, Emmanuel Izengo (28), mkazi wa Tambukareli, Shinyanga baada ya kutokuridhishwa na hukumu iliyotolewa bila ya mshtakiwa, Daniel Makelezia, mkazi wa Lubaga Shinyanga na mdhamini wake, Marko Nkelezia kuwepo mahakamani. Katika hukumu yake, Hakimu Nyangoha alisema mshtakiwa atakapopatikana atatumikia kifungo cha miaka miwili jela baada ya kupatikana na hatia ya wizi wa baiskeli hiyo aina ya Neria yenye thamani ya Sh150,000. Awali, ilielezwa kwamba baada ya tukio hilo la wizi lililotokea Agosti Mosi, mwaka huu katika eneo la Nguzo Nane, mshtakiwa alikamatwa na kuwekwa mahabusu na kufunguliwa kesi namba

ANGALIA YA PICHA MZEE MWENYE NGUVU ANAWEZA KUBEBA MIFUKO 6 YA SIMENTI

Image

AISHA BUI AFUNGUKA JUU YA SHUTUMA ZA KUWA KAFUNGWA UKO BRAZIL

Image
  HUKU kukiwa na madai kuwa msanii wa filamu Bongo, Aisha Bui amekamatwa na kufungwa nchini Brazil kwa kunaswa na unga, mwanadada huyo ameibuka na kufafanua juu ya tuhuma hizo. Akizungumza na gazeti hili mwishoni mwa wiki iliyopita kwa njia ya simu kutokea Brazil, Aisha alisema ameshangazwa na madai hayo wakati yeye yuko nchini humo akiwa amemfuata mchumba wake ambaye jina lake hakuwa tayari kulianika. “Jamani hayo madai ya kwamba nimefungwa huku kwa kesi ya madawa ya kulevya mimi mwenyewe nayashangaa. Niko huku kwa mwezi wa nne sasa, nimekuja kwa mchumba wangu. Hizo taarifa za kwamba eti nimefungwa ni uzushi unaotengenezwa kwa nia ya kunichafua tu. “Wakati naondoka Tanzania ilikuwa kimyakimya kwa kuwa nilijua kuna baadhi ya watu watazusha mambo ya kunipaka matope na ndicho walichokifanya. “Naomba Watanzania wajue niko huru kabisa, naendelea na shughuli zangu kama kawaida. Natarajia kurudi Bongo hivi karibuni,” alisema Aisha .

Rais Jakaya Kikwete atembelea Ubalozi wa Tanzania, Washington, DC

Image
 Rais Dkt Jakaya Kikwete akitembea kwa miguu kutoka hotelini kwake kuja kwenye Ubalozi wa Tanzania Marekani siku ya Jumatano Sept 18, 2013 na kukutana na Mabaozi wa Heshima ambao jana Jumatano wasaini mikataba ya kuwa rasmi Mabalozi wa heshima wataofanyakazi wakiiitangaza Tanzania nchini Marekani kwa ajili ya uwekezaji,  Utalii na mambo mengine yatakayosaidia kuinua uchumi wa Tanzania. Rais Dkat Jakaya Kikwete akisalimiana na Maafisa Ubalozi wakiwemo wafanyakazi mara tu alipoingia Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani uliopo barabra ya 22, Washington, DC Rais Dkt Jakaya Kikwete akitia saidi kitabu cha wageni Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani. Rais Dkt. Jakaya Kikwete akisaini kitabu cha wageni huku Mhe. Waziri Bernard Membe na Mhe. Balozi Liberata Mulamula wakishuhudia.   Raus Dkt. Jakaya Kikwete akisalimiana na Mama William alipokua akiingia chumba cha mikutano cha Nyerere Rais Dkt Jakaya Kikwete akisalimiana

HIVI NDIO OMMY DIMPOZ ALIVYOWASILI JIJI LA MARAHA, WASHINGTON DC

Image
ASEMA YUPOTAYARI KUACHA HISTORIA MAREKANI KUANZIA JUMAMOSI HII WASHINGTON DC ! OMMY DIMPOZ ALIPOWASILI WASHINGTON DC “OMMY DIMPOZ” AKIWA NA PROMOTER WAKE “DMK GLOBAL” DIMPOZ AKIPATA UKODAKI NA PROMOTER WAKE “MR DMK”  PAMOJA NA AKINA DADA WALIOKUWEPO KUMPOKEA KATIKA UWANJA WA NDEGE WA KIMATAIFA WA WASHINGTON DC.KULIA NI MLIMBWENDE ALIYEWAHI KUTWAA TAJI LA MISS TEMEKE NA KUSHOTO NI MLIMBWENDE MWINGINE KUTOKA TZ. OMMY NDANI YA LIMO KUELEKEA HILTON. LUNCH TIME AT THE HILTON. OMMY DIMPOZ AKIWA NA DESIGNER MISS TEMEKE NA GAUNI LAKE LA KWETU FASHION.

Messi amjibu Ronaldo, apiga hat trick, barca ikiua ajax 4-0

Image
Wachezaji wa Baraca wakishangilia pointi tatu Lionel Messi akifunga bao Lionel Messiamejibu mapigo ya mpinzani wake, Cristiano Ronaldo wa Real Madrid baada ya kuifungia hat-trick Barcelona katika ushindi wa 4-0 dhidi ya Ajax katika mchezo wa Kundi H Ligi ya Mabingwa Ulaya, Uwanja wa Nou Camp. Muargentina huyo pamoja na kufunga mabao matatu peke yake usiku, pia alitengeneza bao la nne lililofungwa na Gerard Pique. Haikuwa bahati yao, Ajax kwani walikosa hadi penalti baada ya kipa Victor Valdes kuokoa mkwaju wa Kolbeinn Sigthorsson. Messi alifunga mabao yake katika dakika za 22, 55 na 75, wakati Pique alifunga dakika ya 69. Kikosi cha Barcelona kilikuwa: Valdes, Alves, Pique/Bartra dk80, Mascherano, Adriano, Busquets, Fabregas/Xavi dk72, Iniesta, Sanchez, Messi, Neymar /Pedro dk72.