Taiwan: Wabunge Wavurugana Bungeni, Wachapana Live

Wabunge wakizichapa kavukavu.
WABUNGE wa Taiwan leo walichapana makonde, wakarushiana viti na mabaluni ya maji baada ya kutofautiana kuhusu mradi mmoja wa miundombinu. Tukio hilo ni mwendelezo wa matukio yaliyoanza jana ambapo katika kubishana, wabunge hao walikwidana mashati na kuchapana wakati wa kupitia bajeti ya mradi huo.
Mpango huo ni moja ya miradi mikubwa iliyopendekezwa na Rais Tsai Ing-wen ambayo inajumuisha ujenzi wa reli za kutoa huduma ndogondogo, hatua za kuthibiti mafuriko na mazingira yanayosababishwa na viwanda.
Hata hivyo, chama cha upinzani cha Kuomintang kinapinga mradi huo kikisema unapendelea miji na wilaya ambazo zinaunga mkono chama cha Democratic Progressive (DPP) ambako kina uhakika wa kuungwa mkono katika uchaguzi wa mikoa mwaka kesho. Isitoshe, wapinzani wanapinga kiasi kikubwa mno cha Dola bilioni 13.8 ambazo zitatumika katika mradi huo.
Waziri Mkuu Lin Chuan alishindwa kutoa ripoti ya bajeti hiyo Alhamisi baada kutupiwa baluni la maji na kumfanya aondoke bungeni ambalo liliahirishwa. Leo, Lin aliingia tena bungeni lakini akiwa bado hajasema chochote vurugu ziliibuka.
Wapinzani waliinua viti juu na kulizunguka jukwaa la kutolea hotuba huku wakishikana mashati na mahasimu wenzao na hivyo kumfanya Lin ashindwe kusema chochote ambapo mabaluni ya maji yalikuwa yakitupwa kuelekea eneo hilo.

Comments

Popular posts from this blog