Nape amtaka Rais Magufuli aunde tume


Mbunge wa Jimbo la Mtama mkoani Mtwara kupitia tiketi ya CCM, Mhe. Nape Nnauye amtaka Rais Magufuli aunde tume huru ambayo itaweza kuchunguza matukio ya uhalifu ya uvamizi wa studio unaoendelea nchini.
Mbunge Nape Nnauye akilia kwa furaha baada ya wananchi wa jimbo lake wakimtaka kupita juu ya migongo ya wamama ambao walijipanga ili kiongozi wao huyo apite juu yao, kwa heshima.
Hatua hiyo inatokana na matukio ya kiuhalifu yanayoendelea Tanzania na kuacha maswali mengi vichwani mwa wananchi kushindwa kufahamu kuwa watu hao na vikundi hivyo vya kihuni vinavyofanya vitendo hivyo vinapata wapi mamlaka hayo kuwa na nguvu kushinda Dola.
“Ombi langu kwa Rais namuomba aunde tume huru ichunguze matendo haya yasijirudie tena kwa sababu yasipochukuliwa hatua yataharibu sura ya Tanzania pia yataweza kuibuka makundi ya wahuni kuanza kuteka watu nao kwa kuwa hakuna hatua zinazochukuliwa. Tumsaidie Rais Magufuli kwa kumwambia ukweli naimani atasikia na atafanyia kazi kwa kuwa Rais wetu anapenda kusikiliza watu”. Alisema Nape 
Aidha Mbunge huyo amesema watu wanaofanya mambo hayo wanalengo la kuwagombanisha wananchi na Rais wao jambo ambalo sio zuri kwa taifa.
 "Juzi amepotea msanii Roma Mkatoliki na wengine lakini mpaka sasa haifahamiki wapo wapi, yaani kama vile amepotea Nzi, tulisikia kijana mmoja wa CHADEMA anaitwa Ben Sanane amepotea saizi miezi mitano imepita, matendo haya ya kina Ben Sanane, Roma Mkatoliki, na wengine yanajenga chuki ya wananchi kwa Rais, lakini pia yanajenga chuki kwa wananchi na Chama Cha Mapinduzi (CCM) ". Alisema Nape Nnauye
Vile vile Nape amesema yeye mpaka sasa haamini yule mtu aliyemtolea silaha siku ya mkutano wake na wanahabari kama alitumwa ila shida aliyokuwa nayo ni kutaka kujua vyombo vya ulinzi na usalama vinafanya nini mpaka matukio yote yanatokea.

Comments

Popular posts from this blog