Prof. Lipumba Akana Kuhusika na Vurugu Mkutano wa CUF

prof+LipumbaAliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Prof. Ibrahim Lipumba amesema kuwa hausiki na vurugu zilizoibuka katika mkutano mkuu wa chama hicho uliovunjika juzi Jumapili, Agosti 21, wakati wa uchaguzi wa kujaza nafasi zilizo wazi.
Akieleza hayo jana Jijini Dar es Salaam, Prof. Lipumba amekiri kuwa hakualikwa katika mkutano huo lakini aliombwa na baadhi ya wajumbe kwenda kutoa maelezo ya kwanini aliachia nafasi hiyo ya uenyekiti jambo ambalo viongozi waliokuwepo ukumbini hapo hawakulitaka.
Prof. Lipumba amesema kuwa anaheshimu maamuzi ya pande zote mbili kwa wanaomtaka arejee nafasi ya uenyekiti lakini pia maamuzi ya chama endapo utaratibu utafuatwa kwa kufuata katiba ya chama na demokrasia ya kweli ndani ya chama hicho.
Prof. Lipumba amekataa kuhusika na kukana kutumika na kisiasa na baadhi ya watu ili kukivuruga chama hicho na kusema kuwa viongozi wa chama hicho waepuke maneno ambayo yataweza kukigawanya chama hicho na badala yake wajikite katika kudumisha demokrasia ndani ya chama hicho.

Comments

Popular posts from this blog